Njoo, Unifuate 2024
Aprili 1–7: “Patanishweni na Mungu kwa Upatanisho wa Kristo.” Yakobo 1–4


“Aprili 1–7: ‘Patanishweni na Mungu kwa Upatanisho wa Kristo’. Yakobo 1–4,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Nyumbani na Kanisani: Kitabu cha Mormoni 2024 (2024)

“Aprili 1–7. Yakobo 1–4,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Nyumbani na Kanisani: 2024 (2024)

Picha
mwanamke akiwa amepiga magoti miguuni pa Yesu

Kusamehewa, na Greg Olsen. Imetumika kwa ruhusa. www.GregOlsen.com

Aprili 1–7: Patanishweni na Mungu kwa Upatanisho wa Kristo

Yakobo 1–4

Wanefi walimchukulia Nefi kama “mlinzi wao mkuu” (ona Yakobo 1:10). Pia alikuwa amewalinda dhidi ya hatari za kiroho, akiwaonya dhidi ya dhambi na akiwasihi sana waje kwa Kristo. Sasa kazi hiyo ilimwangukia Yakobo, ambaye Nefi alikuwa amemweka wakfu kuwa kuhani na mwalimu (ona Yakobo 1:18). Yakobo alibeba jukumu la kuwaonya kwa ujasiri wale ambao “walikuwa wameanza kutenda dhambi” wakati pia akitoa faraja kwa “nafsi” za wale walioumizwa na dhambi za wengine (ona Yakobo 2:5–9). Je, ni kwa namna gani angeweza kufanya yote mawili? Yeye angewaelekeza kwa Yesu Kristo—kwa sababu makundi yote mawili yalihitaji uponyaji wa Mwokozi (ona Yakobo 4). Kama ujumbe wa Nefi kabla yake, ushuhuda wa Yakobo ulikuwa wito wa “kupatanishwa na [Mungu] kwa upatanisho wa Kristo” (Yakobo 4:11).

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Nyumbani na Kanisani

Yakobo 1:6–8, 15–19; 2:1–11

Ninayo “kazi kutoka kwa Bwana.”

Kwa Yakobo, kufundisha neno la Mungu ilikuwa ni “kazi kutoka kwa Bwana,” hivyo alifanya kazi kwa bidii “kuadhimisha ofisi [yake]” (Yakobo 1:17, 19). Je, vifungu hivi vya maneno ambavyo Yakobo alivitumia vina maanisha nini kwako wewe? Fikiria kuhusu vile lenzi inavyofanya kazi. Je, hii inakupa wazo lolote? Unapotafakari Yakobo 1:6–8, 15–19 na 2:1–11, fikiria kuhusu kazi ambazo Bwana anaweza kuwa nazo kwa ajili yako. Unahisi kuvutiwa kufanya nini ili “kuzikuza” kazi hizo?

Ona pia “Whom the Lord Calls, the Lord Qualifies,” katika Teachings of Presidents of the Church: Thomas S. Monson (2022), 209–20; “Rise to Your Call” (video), ChurchofJesusChrist.org.

Yakobo 2:12–21

“Msiache kiburi hiki cha mioyo yenu kiharibu nafsi zenu!”

Wanefi walikuwa na tatizo la kiburi na kufokasi kwenye utajiri (ona Yakobo 2:13), na tatizo hili halikuwa la kwao peke yao au katika siku yao. Je, ni kwa namna gani adui mwovu anachochea kupenda utajiri hivi leo? Baada ya kusoma Yakobo 2:12–21, eleza kwa maneno yako mwenyewe ni kwa namna gani Mungu anakutaka utazame utajiri wa vitu. Wimbo wa dini kama “Because I Have Been Given Much” (Hymns, na. 219) ungeweza kutoa nyongeza ya mawazo. Unahisi kushawishika kufanya kipi kuhusu yale uliyojifunza?

Picha
ikoni ya Seminari

Yakobo 2:22–35; 3:10–12

Bwana hufurahia usafi wa kimwili.

Unaposoma Yakabo 2:22–35; 3:10–12, unapata kipi ambacho kinakusaidia uelewe kwa nini usafi wa kimwili ni jambo muhimu sana kwa Mungu? Je, ni yapi baadhi ya matokeo hasi ya utovu wa maadili —katika siku ya Yakobo na katika siku yetu? Je, ni zipi baraka za kuishi maisha ya usafi wa kimwili?

Mzee David A. Bednar alifundisha kwamba tunaishi “katika ulimwengu ambao umekithiri kejeli juu ya utakatifu wa kuzaa watoto” (“We Believe in Being Chaste,” Liahona, May 2013, 41–44). Je, unawasaidiaje wengine waelewe kwa nini unatii sheria ya usafi wa kimwili? Mahali pazuri pa kuanzia ni maelezo ya viwango vya Mungu kuhusu hisia na uhusiano wa kimapenzi katika “Mwili wako ni mtakatifu” kwenye Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana: Mwongozo wa Kufanya Chaguzi (kurasa 22–29). Kipi kingine ambacho unakipata kwenye nyenzo hii ambacho kingeweza kukusaidia ufafanue kwa nini unaishi sheria ya usafi wa kimwili?

Ungeweza pia kupata nyongeza ya majibu katika ujumbe wa Mzee Bednar uliorejelewa hapo juu au katika video “I Choose to Be Pure” (Gospel Library).

Je, kiwango cha Mungu kuhusu usafi wa kimwili kinatofautiana vipi na ujumbe ambao unaweza kukutana nao? Je, ni zipi baraka za kuishi maisha ya usafi wa kimwili?

Ona pia Mada za Injili, “Wema,” Gospel Library; “Same-Sex Attraction” kwenye mkusanyiko wa “Life Help” kwenye Gospel Library.

Yakobo 4

Ninaweza kupatanishwa na Mungu kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo.

Yakobo aliwasihi watu wake “wapatanishwe na [Mungu] kwa upatanisho wa Kristo” (Yakobo 4:11). Maana moja ya kupatanisha ni kurudisha urafiki au kuweka hisia za pande mbili tofauti ziwe sawa. Unapotafakari maisha yako mwenyewe, fikiria kuhusu wakati ulipohisi uko mbali na Baba wa Mbinguni. Mwokozi anakusaidiaje urudishe uhusiano huu? Ni ushauri upi unaupata kweye mlango huu ambao unakusaidia upatanishwe na Mungu? (ona mistari 4–14).

Je, ni umaizi upi wa ziada unaupata kutoka Mathayo 5:23–24? Je, ni kwa jinsi gani Mwokozi anaweza kukusaidia upatanishwe na Mungu—na wengine?

Ona pia 2 Nefi 10:24.

Yakobo 4:8–18

Ninaweza kuepuka upofu wa kiroho kwa kufokasi kwa Mwokozi.

Yakobo alipokuwa akitafuta kuwarudisha watu wake kwa Bwana kikamilifu, aliwaonya kwamba wasiwe vipofu kiroho na kwamba wasidharau “maneno yaliyokuwa wazi” ya injili (ona Yakobo 4:13–14). Kulingana na Yakobo 4:8–18, tunaweza kufanya kipi ili tuepuke upofu wa kiroho?

Ona pia Quentin L. Cook, “Looking Beyond the Mark,” Ensign, Machi 2003, 40–44.

Alipofundisha, Mwokozi alitumia ulinganifu wa maisha ya kila siku. Mafumbo ya Yesu yaliwasidia watu watafute kweli za kiroho kwenye uzoefu wao wa kawaida. Jaribu kufanya kama hivyo wakati unapofundisha. Kwa mfano, wakati unafundisha Yakobo 4:8–18, ungeweza kuwauliza wanafunzi ikiwa wamewahi kufanyiwa uchunguzi wa macho. Ni kwa namna gani daktari alifanyia tathmini uoni wao? Tunawezaje kufanyia tathmini uoni wetu wa kiroho?

Kwa mawazo zaidi, ona toleo la mwezi huu la Liahona na magazeti ya Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana.

Mawazo kwa ajili ya Kuwafundisha Watoto

Yakobo 2:8

Mungu huponya nafsi iliyojeruhiwa.

  • Ili kuwasaidia watoto wako waelewe jinsi “nafsi iliyojeruhiwa” inavyoweza kuponywa, mngeweza kujadiliana pamoja jinsi miili yetu inavyoumia na nini kinaisaidia ipone. Pengine watoto wako wangeweza kushiriki nyakati ambapo waliumia na nini kiliwasaidia wapone. Ungeweza hata kuwaonesha bandeji au dawa kama sehemu ya mazungumzo haya. Labda ungeweza kushiriki nao ni kwa jinsi gani Mwokozi amekusaidia wewe wakati roho yako ilipohitaji uponyaji.

Yakobo 2:17–19

Ninaweza kuwasaidia wengine wenye uhitaji pale ninaposhiriki nao.

  • Baadhi ya watu katika wakati wa Yakobo walikuwa matajiri sana, lakini hawakutaka kushiriki na wengine kile walichokuwa nacho. Wakati unasoma mafundisho ya Yakobo katika Yakobo 2:17–19, ungewapa watoto wako picha au vitu vya kushikilia ambavyo vinaendana na maneno au vifungu vya maneno katika mistari hii. Ungeweza kueleza kwamba unashiriki vitu hivi na wao; na kisha ungeweza kuwaalika washiriki vitu na wewe au wao kwa wao. Zungumza kuhusu jinsi gani wewe unahisi wakati unaposhiriki. Je, ni kipi kingine tungeweza kushiriki na wengine ili kuwasaidia wahisi furaha?

  • Baada ya kusoma pamoja Yakobo 2:17, pengine watoto wako wangeweza kutaja baadhi ya baraka ambazo Baba wa Mbinguni ameshiriki nao. Kwa nini Yeye anatutaka sisi tushiriki na wengine?

Yakobo 4:6, 10–11

Ninaweza kuimarisha imani yangu katika Yesu Kristo.

  • Imani ya Yakobo katika Kristo ilikuwa thabiti sana haingeweza kutingishwa. Ili kuwafundisha watoto wako jinsi ya kujenga imani kama hiyo, ungeweza kuwauliza kuhusu vitu ambavyo tunavifanya kuifanya miili yetu iwe na nguvu. Tunaweza kufanya nini ili kuifanya imani yetu katika Yesu Kristo iwe imara zaidi? Someni Yakobo 4:6 pamoja na wasaidie watoto wagundue kitu ambacho Yakobo na watu wake walikifanya ili kuifanya imani yao iwe “isiyotingishwa.”

  • Njia nyingine ya kuwasaidia watoto wako waelewe maana ya “ kutotingishwa” katika imani yao inaweza kuwa kutafuta mti mkubwa na kuwaomba watikise tawi moja moja. Kisha waruhusu wajaribu kutikisa shina la mti. Kwa nini ni vigumu zaidi kutikisa shina la mti? Ni vifungu vipi vya maneno katika Yakobo 4:6, 10–11 hueleza kile tunachoweza kutenda kuifanya imani yetu kwa Yesu Kristo iwe isiyotingishwa?

    Picha
    mti mkubwa katika bustani

    Kama vile shina la mti, imani yetu katika Kristo inaweza kuwa “isiyotingishwa.”

  • Kwa ajili ya ulinganifu mwingine ili kuwafundisha watoto wako kuhusu imani isiyotingishwa, ona Neil L. Andersen, “Vimbunga vya Kiroho” (Liahona, Mei 2014, 18–21; na video “Spiritual Whirlwinds“) au “The Wise Man and the Foolish Man” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 281; ona pia Mathayo 7:24–27).

Kwa ajili ya mawazo zaidi, ona toleo la mwezi huu la gazeti la Rafiki

Picha
Yakobo akiandika kwenye mabamba ya dhahabu

Nitayatuma Maneno Yao (Yakobo Mwalimu), na Elspeth Caitlin Young

Chapisha