Njoo, Unifuate
Julai 6–12. Alma 30–31: “Nguvu za Neno la Mungu”


“Julai 6–12. Alma 30–31: ‘Nguvu za Neno la Mungu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Julai 6–12. Alma 30–31,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Watu Binafsi na Familia: 2020

Picha
Alma anamfundisha Korihori

Vitu Vyote Vinashuhudia Kuwa Kuna Mungu (Alma na Korihor), na Walter Rane

Julai 6–12

Alma 30–31

“Uwezo wa Neno la Mungu”

Alma alishuhudia juu ya “matokeo ya nguvu” za neno la Mungu (Alma 31:5). Unaposoma Alma 30–31, andika misukumo yako unapohisi matokeo ya nguvu za neno la Mungu juu yako.

Andika Misukumo Yako

Maelezo katika Alma 30–31 yanadhihirisha wazi uwezo wa maneno—kwa ajili ya uovu na kwa ajili ya wema. “Maneno ya kusifu” na “maneno kwa sauti kubwa” ya mwalimu wa uongo aliyeitwa Korihori yalitishia kuleta “roho nyingi kwenye maangamizo” (Alma 30:31, 47). Vile vile, mafunzo ya Mnefi muasi aliyeitwa Zoramu yalisababisha kundi zima la watu kufanya “makosa makubwa” na “waliharibu njia za Bwana” (Alma 31:9, 11).

Kinyume cha hayo, Alma alikuwa na imani isiyotikisika kwamba neno la Mungu lingekuwa na “maelekezo ya nguvu zaidi kwa akili za watu kuliko upanga au kitu chochote kingine” (Alma 31:5)—ikiwa ni pamoja na maneno ya Korohori na Zoramu. Maneno ya Alma yalionyesha kweli za milele na alitegemea nguvu za mbinguni kumnyamazisha Korihori (ona Alma 30:39–50), na waliomba baraka za mbinguni juu ya wale walioenda pamoja naye kuwaleta Wazoramu tena kwenye ukweli (ona Alma 31:31–38). Hii ni mifano yenye thamani kwa wafuasi wa Kristo leo hii, wakati “maneno kwa sauti kubwa” na “makosa makubwa” kwa mara nyingine yana matokeo yenye nguvu zaidi kwenye akili za watu (Alma 30:31; 31:9). Lakini tunaweza kupata ukweli kwa kuamini, kama alivyofanya Alma, “uwezo wa neno la Mungu” (Alma 31:5).

Picha
ikoni ya kujifunza kibinafsi

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kibinafsi

Alma 30:6, 12

Mpinga-Kristo ni nani?

Katika Alma 30:6, Korihori anaitwa “Mpinga-Kristo.” Mpinga-Kristo ni “mtu anayemwiga Kristo lakini kwa kweli yuko kinyume na Kristo (1 Yohana 2:18–22; 4:3–6; 2 Yohana 1:7). Kwa upana ni mtu yeyote au kitu chochote ambacho kinaiga injili ya kweli au mpango wa wokovu na kwamba kwa wazi au kwa siri kinampinga Kristo” (Kamusi ya Biblia, “Mpinga Kristo”).

Je, ni “injili zipi za bandia [za] injili ya kweli” unazoziona katika ulimwengu wa leo? Kwa mfano, Dada Julie B. Beck, aliyekuwa Rais Mkuu wa Muungano wa Usaidizi wa Akina mama , alifundisha, “Mafundisho au kanuni yoyote tunayoisikia [sisi] kutoka duniani ambayo inaipinga familia pia ni mpinga-Kristo” (“Kufundisha Mafundisho ya Familia,” Ensign, Mac. 2011, 15).

Picha
Korihori anazungumza na Alma

Korihori Anamkabili Alma, na Robert T. Barrett

Alma 30:6–60

Kitabu cha Mormoni kinaweza kunisaidia kuupinga ushawishi wa wale wanaojaribu kunidanganya.

Unaposoma Alma 30:6–31, mafundisho ya Korihori yanaweza kuonekana kama yanajulikana. Hiyo ni kwa sababu, kama vile alivyofundisha Rais Ezra Taft Benson, Kitabu cha Mormoni kinafunua na kinaweza kutuimarisha dhidi ya “miundo ya uovu, mikakati, na mafundisho ya shetani katika siku zetu. Aina ya wakengeufu katika Kitabu cha Mormoni ni sawa na aina tuliyo nayo leo. Mungu, kwa uelewa wake wa kabla na usio na mipaka, ndipo akakitengeneza Kitabu cha Mormon ili tuweze kuona makosa na kujua jinsi ya kupambana na elimu ya uongo, kisiasa, kidini na falsafa za wakati wetu (Mafundisho ya Marais wa Kanisa: Ezra Taft Benson, [2014], 132).

Fikiria kutengeneza orodha ya mafundisho ya uongo Korihori aliyofundisha katika Alma 30:6–31. Nini baadhi ya matokeo ya kuamini baadhi ya mafundisho haya? Kwa mfano, ni nini matokeo ya kuamini kwamba “mtu akifa huo ndio mwisho wake”? (Alma 30:18). Ni mafundisho gani ya uwongo yaliyofundishwa na Korihori yanafanana na mafundisho ya uwongo ambayo umeyaona katika ulimwengu wa sasa?

Kusoma kuhusu mazungumzo kati ya Korihori na Alma kunaweza kukusaidia kujitayarisha kwa ajili ya hali ambazo wengine wanaweza kujaribu kukudanganya. Yaweza kusaidia kujifunza Alma 30:29–60 kuelewa jinsi Korihori alivyodanganywa (ona hasa mistari 52–53). Unaweza kujifunza nini kutokana na majibu ya Alma kwa mafundisho ya Korihori? (ona Alma 30:31–35).

Alma 31

Neno la Mungu lina uwezo wa kuongoza watu kufikia haki.

Tatizo la Wazoramu kujitenga na Wanefi linaweza kuwa lilionekana kwa baadhi kama lilihitaji suluhisho la kisiasa au kijeshi (ona Alma 31:1–4). Lakini Alma alikuwa amejifunza kuamini “uwezo wa Neno la Mungu” (Alma 31:5). Unajifunza nini kutoka Alma 31:5 kuhusu uwezo wa neno la Mungu? Ni jinsi gani umeona neno la Mungu likiwaongoza “watu kufanya yale ambayo ni ya haki?? (Alma 31:5). Tafakari jinsi unavyoweza “kujaribu” (kutumia au kupima) neno la Mungu kumsaidia mtu unayempenda.

Ili uweze kuelewa zaidi mbinu ya Alma kuwaokoa wengine, unaweza kulinganisha tabia, hisia, na vitendo vyake na vile vya Wazoramu, kama ilivyoelezewa katika Alma 31. Jedwali sawa na linalofuata linaweza kukusaidia. Umegundua tofauti zipi? Unahisi vipi kuwa unaweza kuwa zaidi kama Alma?

Wazoramu

Alma

Wazoramu

Waliamini kwamba wale waliokuwa nje ya kundi lao walikuwa wamehukumiwa jahanamu (Alma 31:17).

Alma

Aliamini kwamba Wazoramu walikuwa “ndugu” zake na nafsi zao zilikuwa zenye “thamani” (Alma 31:35).

Wazoramu

Waliweka mioyo yao katika utajiri (Alma 31:24, 28).

Alma

Alitaka kuleta nafsi kwa Yesu Kristo (Alma 31:34).

Wazoramu

Alma

Picha
ikoni ya kujifunza kifamilia

Mawazo kwa ajili ya Kujifunza Maandiko Kifamilia na Jioni ya Familia Nyumbani

Unaposoma maandiko na familia yako, Roho anaweza kukusaidia kujua kanuni zipi zisisitizwe na kujadiliwa ili kukidhi mahitaji ya familia yako. Haya ni baadhi ya mawazo.

Alma 30:44

Fikiria kusoma na kujadiliana Alma 30:44 pamoja mnapoenda nje kwa matembezi au mnapotazama picha za uumbaji wa Mungu. Wana familia wanaweza kushiriki kile wanachofikiri kinatoa ushuhuda juu ya Mungu. Je, ni kwa jinsi gani vitu hivi—au uzoefu mwingine ambao tumekuwa nao—unatutusaidia kujua Mungu ni halisi?

Alma 30:56–60

Tunajifunza nini kutoka Alma 30:56–60 kuhusu jinsi ambavyo ibilisi anawatendea wafuasi wake? Tunaweza kufanya nini kulinda nyumba yetu dhidi ya ushawishi wake?

Alma 31:20–38

Baada ya kusoma Alma 31:20–38 pamoja na familia yako, mnaweza kujadili maswali yafuatayo: Ni kwa jinsi gani sala ya Alma ilikuwa tofauti na sala ya Wazoramu? Ni kwa jinsi gani tunaweza kuiga mfano wa Alma katika sala zetu za binafsi na za familia?

Watoto wadogo wanaweza kuweka jiwe chini ya mito yao ili kuwasaidia kukumbuka kusali kila asubuhi na usiku. Wanaweza pia kufurahia kupamba jiwe lao.

Alma 31:23

Je, tunafanya nini kila siku nyumbani kwetu ili kujifunza kuhusu na kuzungumza juu ya Mungu?

Kwa mawazo zaidi kwa ajili ya kufundisha watoto, ona muhtasari wa wiki hii katika katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi.

Kuboresha Kujifunza Binafsi

Andaa Mazingira yako. “Mazingira yetu kwa kiasi kikubwa yanaweza kuathiri uwezo wetu wa kujifunza na kuhisi ukweli” (Kufundisha Katika Njia ya Mwokozi, 15). Jaribu kutafuta mahali pa kujifunza maandiko ambapo pataalika ushawishi wa Roho Mtakatifu. Muziki wenye kutia moyo na picha vinaweza pia kumwalika Roho Mtakatifu.

Picha
Mzoramu akisali juu ya Rameumtomu

Rameumtomu, na Del Parson

Chapisha