Njoo, Unifuate
Julai 6–12. Alma 30–31: “Nguvu za Neno la Mungu”


“Julai 6–12. Alma 30–31: ‘Nguvu za Neno la Mungu,’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Kitabu cha Mormoni 2020 (2020)

“Julai 6–12. Alma 30–31,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2020

Picha
Alma akimfundisha Korihori

Vitu Vyote Vinaonyesha kwamba Kuna Mungu (Alma na Korihori), na Walter Rane

Julai 6–12

Alma 30–31

“Nguvu za Neno la Mungu”

Soma Alma 30–31 ukiwa na watoto unaowafundisha akilini. Unapotafakari uwezo wao na mahitaji yao, Roho Mtakatifu atakusaidia kujua jinsi ya kuwafundisha.

Andika Misukumo Yako

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike watoto kushiriki majibu ya maswali kama yafuatayo: Ni wakati gani tunapaswa kusali? Tunasema nini tunaposali? Je, mtu yoyote anaweza kushiriki kuhusu jinsi Wazoramu walivyosali au jinsi Alma alivyosali?

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Alma 30:44

Vitu vyote vinashuhudia kuhusu Mungu.

Alma alionyesha vitu angani na duniani ili kushuhudia kwamba Mungu anaishi na anaongoza ulimwengu. Ni vitu gani unaweza kuwasaidia watoto kuona ambavyo viko katika mazingira yao vinavyoshuhudia kuhusu Mungu?

Shughuli za Yakini

  • Soma Alma 30:44 kwa watoto, na uwaombe wasikilize vitu ambavyo Alma alisema vinatusaidia kujua Mungu ni halisi. Onyesha picha ya baadhi ya vitu hivi, na waombe watoto kuonyesha picha wakati ukisoma kuzihusu katika mstari. Waalike watoto wachore picha za vitu vinavyowasaidia kumwamini Mungu.

  • Kama inawezekana, fanya matembezi ya nje pamoja na watoto au waombe wasimame dirishani wakati ukisoma Alma 30:44. Waombe waonyeshe vitu wanavyoona ambavyo vinawasaidia kujua Mungu ni halisi. Ukurasa wa shughuli ya wiki hii pia unaweza kusaidia.

  • Waombe watoto wakae katika duara na kuimba pamoja wimbo kuhusu uumbaji wa Mungu, kama vile “My Heavenly Father Loves Me” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 228–29). Wakati watoto wakiimba, waalike kuzungusha kitu kama vile mpira. Muziki unaposimama, muombe mtoto aliyeshikilia kitu kushiriki kitu kimoja ambacho Baba wa Mbinguni aliumba ambacho anashukuru kwa ajili yake.

Alma 31:5

Neno la Mungu lina nguvu.

Watoto wanapofikiria kuhusu nguvu, wanaweza kufikiria vitu kama mashujaa, malkia, au wafalme. Unaweza kuwasaidia kuelewa kwamba neno la Mungu lina nguvu zaidi kuliko “kitu kingine chochote” (Alma 31:5).

Shughuli za Yakini

  • Chora upanga ubaoni. Soma Alma 31:5 kwa watoto, na waalike wasikilize kile ambacho Alma anasema kina nguvu kuliko upanga. Shiriki uzoefu ambapo neno la Mungu lilikuwa na ushawishi wenye nguvu kwako.

  • Imbeni pamoja wimbo kuhusu maandiko, kama vile “Scripture Power” (music.ChurchofJesusChrist.org), na waombe watoto wasikilize jinsi gani maandiko yanatusaidia. Rudia kifungu cha maneno “Neno la Mungu lina nguvu zaidi ya …” mara kadhaa, na waombe watoto wakusaide kumalizia kifungu cha maneno.

Alma 31:8–35

Baba wa Mbinguni husikia sala zangu.

Alma alihisi huzuni wakati alipoona jinsi Wazoramu walivyosali (ona Alma 31:24)—hawakuamini katika Yesu Kristo na mara nyingi walirudia sala ile ile mahali ambapo kila mtu angeweza kuwaona (Alma 31:13–14). Lakini sala ya Alma ilikuwa ya unyenyekevu na iliyoonyesha imani katika Kristo.

Shughuli za Yakini

  • Toa muhtasari wa hadithi ya Alma na Wazoramu kwa watoto ukitumia mistari kutoka Alma 31:8–35. Ungeweza pia kutumia “Mlango wa 28: Wazoramu na Rameumptomu” (Hadithi za Kitabu cha Mormoni, 78–80, au video zinazohusiana katika ChurchofJesusChrist.org). Onyesha tofauti kati ya sala ya Wazoramu na sala ya Alma. Waalike watoto kufikiria wamekutana na mmoja wa watoto wa Wazoramu. Ni nini wangesema ili kumfundisha jinsi ya kusali?

  • Wasaidie watoto kutambua mambo wazoramu waliyosema katika sala zao (ona Alma 31:15–18) wakati wakikusaidia kujenga mnara wa Rameumptomu kwa kutumia matofali au mawe. Elezea kwamba hivi si jinsi tunavyopaswa kusali. Waulize watoto jinsi tunavyopaswa kusali, na waache waondoe tofali au jiwe kwa kila kitu wanachotaja.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Alma 30

Kitabu cha Mormoni kinanionya dhidi ya mafundisho ya uongo.

Mafundisho ya uongo ya Korihori yameelezewa katika Kitabu cha Mormoni ili kutusaidia kutambua na kukataa mafundisho yanayofanana na hayo katika siku yetu.

Shughuli za Yakini

  • Onyesha baadhi ya vitu (kama vile pesa au chakula) na mfano bandia wa vitu hivi. Ni vitu vipi watoto wangependa kuwa navyo? Wasaidie watoto kutafuta Alma 30:12–18 ili kupata mafundisho ya uongo ambayo Korihori alifundisha kuhusu Mungu.

  • Wasaidie watoto kutambua uongo aliofundisha Korihori na wauandike kwenye vipande vya karatasi ili kuviweka ubaoni (ona Alma 30:12–18, 24). Waombe watoto wachunguze Alma 30:32–35, ili kutafuta jinsi ambavyo Alma alijibu uongo wa Korihori. Waulize watoto jinsi wanavyoweza kujua kwamba mambo aliyofundisha Alma ni ya kweli.

    Picha
    Korihori anazungumza na Alma

    Korihori Anamkabili Alma, na Robert T. Barrett

Alma 31:5

Neno la Mungu lina nguvu zaidi ya kitu kingine chochote.

Ni wakati gani umetambua nguvu ya neno la Mungu? Fikiria ni kwa jinsi gani uzoefu wako ungeweza kuwavuvia watoto unaowafundisha.

Shughuli za Yakini

  • Waalike watoto kufikiria kitu au mtu mwenye nguvu, au kuonyesha picha ya baadhi ya vitu vyenye nguvu. Nini huvifanya vitu hivi viwe vyenye nguvu? Someni Alma 31:5 kwa pamoja, na waulize watoto kile wanachodhani mstari huu unamaanisha. Ni kwa jinsi gani neno la Mungu lina nguvu kuliko upanga? Je, lina nguvu ya kufanya nini?

  • Wasiliana na watoto kadhaa kabla, na waombe wafikirie kuhusu uzoefu wa kushiriki darasani pale maandiko au hotuba kutoka kwa kiongozi wa Kanisa ilipowasaidia kufanya jambo jema. Ni kwa nini neno la Mungu liliwafanya watake kufanya mambo mema?

  • Imba wimbo pamoja na watoto kuhusu neno la Mungu, kama vile “Search, Ponder, and Pray” au “Follow the Prophet” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 109, 110–11). Wangeweza pia kuimba “Scripture Power” (music.ChurchofJesusChrist.org).

Alma 31:8–35

Naweza kuwa mnyenyekevu.

Kati ya makosa yote ambayo Wazoramu walifanya, ilikuwa ni kiburi chao ambacho kilionekana kumfanya Alma ahuzunike hasa. Hii ingeweza kuwa fursa ya kuwafundisha watoto umuhimu wa unyenyekevu.

Shughuli za Yakini

  • Wasaidie watoto kuelewa tofauti kati ya kiburi na unyenyekevu (ona “Kiburi” and “Nyenyekea, Unyenyekevu” katika Mwongozo wa Maandiko). Waombe watoto kufanya zamu kusoma Alma 31:24–28. Au someni pamoja “Mlango wa 28: Wazoramu na Rameumptomu” (Hadithi za Kitabu cha Mormoni, 78–90). Mnaposoma, waombe kugundua jinsi Wazoramu walivyoonyesha kuwa na kiburi. Ni kwa jinsi gani Alma alionyesha kwamba alikuwa mnyenyekevu? (ona Alma 31:30–33).

  • Wagawe watoto katika makundi, na liombe kila kundi kuamua juu ya jibu la maswali kama haya: Wazoramu waliweka mioyo yao kwenye nini? (ona Alma 31:24, 28). Ni nini baadhi ya vitu vya dunia ambavyo watu huweka mioyo yao juu yake leo? Kwa nini watu wanaweza kudhani kwamba wao ni bora kuliko wengine? Pale kila kundi linaposhiriki jibu, waache wachore sehemu ya mnara wa Rameumptomu ubaoni. Kisha waombe kufuta sehemu za mnara kila mara wanapofikiria jinsi wanavyoweza kuonyesha unyenyekevu.

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Waalike watoto kufundisha familia zao kitu walichojifunza kuhusu nguvu ya neno la Mungu leo.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie watoto kujifunza kutoka kwenye maandiko. Watoto wadogo wanaweza kushindwa kusoma sana, lakini bado unaweza kuwahusisha katika kujifunza kutoka kwenye maandiko. Kwa mfano, ungeweza kusoma kifungu cha maneno na kuwaalika kusimama au kuinua mikono wakati wanaposikia neno au kifungu cha maneno husika. Kisha wasaidie kuelewa neno au kifungu cha maneno. (Ona Kufundisha katika Njia ya Mwokozi, 20–21.)

Chapisha