Sura ya 28
Wazoramu na Rameumtomu
Wazoramu kwa wakati fulani walikuwa waumini wa Kanisa la Mungu lakini walikuja kuwa waovu na walikuwa wakiabudu sanamu.
Wanefi walitaka kuwazuia Wazoramu kujiunga na Walamani, kwa hivyo Alma na baadhi ya waisionari wengine walienda kuhubiri neno la Mungu kwa Wazoramu.
Wamisionari hawa walishangazwa na kukasirishwa na jinsi ambavyo Wazoramu walikuwa wakiabudu katika makanisa yao, yaliyoitwa sinagogi.
Katikati ya Kanisa, Wazoramu walikuwa wamejenga jukwaa refu lililoitwa Rameumtomu. Kulikuwa na nafasi ya mtu mmoja tu kusimama juu yake.
Wazoramu walifanya zamu kusimama pale, walinyosha mikono kuelekea mbinguni na kwa sauti kubwa kukariri sala inayofanana.
Katika sala hii, Wazoramu walisema Mungu hana mwili; yeye ni roho tu. Pia walisema kwamba hakungekuwepo na Kristo.
Wazoramu walidhani kwamba Mungu alikuwa amewachagua wao pekee kuokolewa katika ufalme wa Mungu. Walishukuru kwa kuwa watu wake wapendwa.
Baada ya kila Mzoramu kusali, walienda nyumbani na hawakusali au kuzungumza tena kuhusu Mungu kwa wiki mzima.
Wazoramu matajiri walipenda dhahabu na fedha, na walijigamba kuhusu utajiri wao hapa duniani. Alma alihuzunika kuona jinsi walivyokuwa waovu.
Alma alisali kwa ajili yake na wamisionari wake kuwa na nguvu, faraja, na mafanikio katika kazi yao.
Baada ya kuomba msaada kwa ajili ya kuwarejesha Wazoramu kwenye ukweli, Alma na wale wamisionari wengine walijazwa na Roho Mtakatifu.
Wamisionari kisha walielekea katika sehemu tofauti kuhubiri. Mungu aliwabariki kwa chakula na mavazi na kuwaimarisha katika kazi yao.
Wazoramu waliokuwa maskini hawakukubaliwa ndani ya makanisa. Watu hawa walianza kuwasikiliza wamisionari.
Wengi walimwuliza Alma kile walichopaswa kufanya. Alma aliwaambia kwamba hawakuhitaji kuwa ndani ya kanisa ili wasali au wamwabudu Mungu.
Aliwaambia wawe na imani kwa Mungu. Kisha Amuleki akawafundisha kuhusu Yesu Kristo na mpango wa Mungu kwa ajili ya watoto wake.
Wamisionari waliondoka, na Wazoramu waliokuwa wamewaamini wakafukuzwa kutoka mjini. Waaminifu walienda kuishi katika nchi ya Yershoni na watu wa Amoni.
Ingawaje Wazoramu waovu waliwatolea vitisho watu wa Amoni, watu wa Amoni waliwasaidia Wazoramu wenye haki na kuwapa chakula, mavazi, na ardhi.