Scripture Stories
Mlango wa 28: Wazoramu na Rameumtomu


Sura ya 28

Wazoramu na Rameumtomu

Picha
Wazoramu wakiabudu sanamu

Wazoramu kwa wakati fulani walikuwa waumini wa Kanisa la Mungu lakini walikuja kuwa waovu na walikuwa wakiabudu sanamu.

Picha
Alma na wamisionari wengine

Wanefi walitaka kuwazuia Wazoramu kujiunga na Walamani, kwa hivyo Alma na baadhi ya waisionari wengine walienda kuhubiri neno la Mungu kwa Wazoramu.

Picha
wamisionari na Wazoramu

Wamisionari hawa walishangazwa na kukasirishwa na jinsi ambavyo Wazoramu walikuwa wakiabudu katika makanisa yao, yaliyoitwa sinagogi.

Picha
mtu akiwa amesimama katika jukwaa

Katikati ya Kanisa, Wazoramu walikuwa wamejenga jukwaa refu lililoitwa Rameumtomu. Kulikuwa na nafasi ya mtu mmoja tu kusimama juu yake.

Picha
mtu akiwa amenyosha mikono

Wazoramu walifanya zamu kusimama pale, walinyosha mikono kuelekea mbinguni na kwa sauti kubwa kukariri sala inayofanana.

Picha
mtu akiwa amenyosha mikono hewani

Katika sala hii, Wazoramu walisema Mungu hana mwili; yeye ni roho tu. Pia walisema kwamba hakungekuwepo na Kristo.

Picha
mtu akisali juu ya jukwaa

Wazoramu walidhani kwamba Mungu alikuwa amewachagua wao pekee kuokolewa katika ufalme wa Mungu. Walishukuru kwa kuwa watu wake wapendwa.

Picha
Wazoramu wakitembea

Baada ya kila Mzoramu kusali, walienda nyumbani na hawakusali au kuzungumza tena kuhusu Mungu kwa wiki mzima.

Picha
Wazoramu walio na mali

Wazoramu matajiri walipenda dhahabu na fedha, na walijigamba kuhusu utajiri wao hapa duniani. Alma alihuzunika kuona jinsi walivyokuwa waovu.

Picha
Alma akisali

Alma alisali kwa ajili yake na wamisionari wake kuwa na nguvu, faraja, na mafanikio katika kazi yao.

Picha
Wamisionari wakisali

Baada ya kuomba msaada kwa ajili ya kuwarejesha Wazoramu kwenye ukweli, Alma na wale wamisionari wengine walijazwa na Roho Mtakatifu.

Picha
mmisionari akipata chakula

Wamisionari kisha walielekea katika sehemu tofauti kuhubiri. Mungu aliwabariki kwa chakula na mavazi na kuwaimarisha katika kazi yao.

Picha
mmisionari akiwafundisha watu maskini

Wazoramu waliokuwa maskini hawakukubaliwa ndani ya makanisa. Watu hawa walianza kuwasikiliza wamisionari.

Picha
Alma akihhubiri

Wengi walimwuliza Alma kile walichopaswa kufanya. Alma aliwaambia kwamba hawakuhitaji kuwa ndani ya kanisa ili wasali au wamwabudu Mungu.

Picha
Amuleki akiwafundisha watu

Aliwaambia wawe na imani kwa Mungu. Kisha Amuleki akawafundisha kuhusu Yesu Kristo na mpango wa Mungu kwa ajili ya watoto wake.

Picha
waaminifu wanaondoka mjini

Wamisionari waliondoka, na Wazoramu waliokuwa wamewaamini wakafukuzwa kutoka mjini. Waaminifu walienda kuishi katika nchi ya Yershoni na watu wa Amoni.

Picha
watu wakiwatazama wengine wakiondoka

Ingawaje Wazoramu waovu waliwatolea vitisho watu wa Amoni, watu wa Amoni waliwasaidia Wazoramu wenye haki na kuwapa chakula, mavazi, na ardhi.

Chapisha