Sura ya 34
Helamani na Vijana Mashujaa 2000
Watu wa Amoni walikuwa wamemuahidi Mungu kwamba hawangepigana tena. Waliishi karibu na Wanefi, na Wanefi waliwalinda.
Wakati maadui wa watu wa Amoni walipowashambulia Wanefi, watu wa Amoni walitaka kuvunja ahadi yao na kuwasaidia Wanefi.
Helamani na viongozi wengine wa Wanefi hawakutaka watu wa Amoni kuvunja ahadi yao kwa Mungu.
Vijana wadogo wa watu wa Amoni walikuwa hawajaweka ahadi. Walitaka kulisaidia jeshi la Wanefi kupigania uhuru.
Elfu mbili kati ya hao vijana walichagua kuilinda nchi yao. Walimuomba Helamani kuwa kiongozi wao.
Vijana hawa walikuwa thabiti, mashujaa na wenye nguvu. Pia walikuwa wakweli na wa kuaminika, na walitii amri za Mungu.
Helamani aliongoza vijana mashujaa 2000 kwenye vita. Aliwaita wanawe, na wao walimwita baba yao.
Ingawa wana wa Helamani hawakuwa wamewahi kupigana vita, hawakuogopa. Mama zao waliwafundisha kuwa na imani katika Mungu na kujua kwamba angewasaidia.
Helamani na jeshi lake walipigana vita kadhaa dhidi ya Walamani. Vijana hawa walitii yote Helamani aliyoamrisha.
Walipigana kwa ushujaa na walisaidia kumfukuza adui. Baada ya vita Helamani alikuta kwamba wana wake wote walikuwa wamejeruhiwa lakini hakuna aliyekuwa ameuwawa.
Ilikuwa ni muujiza. Helamani alifurahi sana. Alijua kwamba vijana hawa walikuwa wamelindwa kwa sababu ya imani yao kubwa katika Mungu.