Scripture Stories
Sura ya 34: Helamani na vijana Mashujaa 2000


Sura ya 34

Helamani na Vijana Mashujaa 2000

Picha
Walinzi katika ukuta

Watu wa Amoni walikuwa wamemuahidi Mungu kwamba hawangepigana tena. Waliishi karibu na Wanefi, na Wanefi waliwalinda.

Picha
Watu wakiongea na Helamani

Wakati maadui wa watu wa Amoni walipowashambulia Wanefi, watu wa Amoni walitaka kuvunja ahadi yao na kuwasaidia Wanefi.

Picha
Helamani akizungumza na kundi

Helamani na viongozi wengine wa Wanefi hawakutaka watu wa Amoni kuvunja ahadi yao kwa Mungu.

Picha
Wana wa watu wa Amoni

Vijana wadogo wa watu wa Amoni walikuwa hawajaweka ahadi. Walitaka kulisaidia jeshi la Wanefi kupigania uhuru.

Picha
Mashujaa 2000

Elfu mbili kati ya hao vijana walichagua kuilinda nchi yao. Walimuomba Helamani kuwa kiongozi wao.

Picha
Mashujaa watatu

Vijana hawa walikuwa thabiti, mashujaa na wenye nguvu. Pia walikuwa wakweli na wa kuaminika, na walitii amri za Mungu.

Picha
Helamani akiwa na mashujaa

Helamani aliongoza vijana mashujaa 2000 kwenye vita. Aliwaita wanawe, na wao walimwita baba yao.

Picha
Helamani akiwaongoza mashujaa

Ingawa wana wa Helamani hawakuwa wamewahi kupigana vita, hawakuogopa. Mama zao waliwafundisha kuwa na imani katika Mungu na kujua kwamba angewasaidia.

Picha
Mashujaa wakipigana vita

Helamani na jeshi lake walipigana vita kadhaa dhidi ya Walamani. Vijana hawa walitii yote Helamani aliyoamrisha.

Picha
Mashujaa baada ya vita

Walipigana kwa ushujaa na walisaidia kumfukuza adui. Baada ya vita Helamani alikuta kwamba wana wake wote walikuwa wamejeruhiwa lakini hakuna aliyekuwa ameuwawa.

Picha
Helamani akiwa na mashujaa

Ilikuwa ni muujiza. Helamani alifurahi sana. Alijua kwamba vijana hawa walikuwa wamelindwa kwa sababu ya imani yao kubwa katika Mungu.

Chapisha