Scripture Stories
Sura ya 18: Alma Mdogo Anatubu


Sura ya 18

Alma Mdogo Anatubu

Picha
Alma akiwatawaza wengine

Mfalme Mosia alimteua Alma kuwa kiongozi wa Kanisa kule Zarahemla. Alma kisha akawachagua watu wengine kumsaidia kuwafundisha Wanefi.

Picha
waaminifu wakiteswa

Alma na Mfalme Mosia walikuwa na wasi wasi kwa sababu wasioamini walikuwa wakisababisha mateso kwa waumini wa Kanisa kwa sababu ya imani yao.

Picha
Alma Mdogo

Alma alikuwa na mwana wa kiume aliyeitwa Alma. Alma Mdogo hakuamini mafundisho ya baba yake na akawa mtu muovu.

Picha
Alma Mdogo na wana wa Mfalme Mosia

Alma Mdogo na wana wanne wa Mfalme Mosia walipigana dhidi ya Kanisa. Waliwashawishi watu wengi kuacha Kanisa na kuwa waovu.

Picha
Alma akisali

Alma alisali kwamba mwanawe angejua ukweli na kutubu.

Picha
Alma Mdogo na wana wa Mfalme Mosia

Alma Mdogo na wana wa Mfalme Mosia waliendelea kujaribu kuliangamiza Kanisa.

Picha
malaika akiwatokea watu

Siku moja malaika aliwatokea. Malaika alizungumza kwa sauti kubwa ambayo ilitetemesha ardhi.

Picha
wavulana wakitiwa hofu na malaika

Wavulana hao watano walikuwa na hofu kiasi kwamba walianguka chini. Mara ya kwanza hawakuelewa kile malaika alichokuwa akisema.

Picha
malaika akizungumza na Alma Mdogo

Malaika alikuwa amekuja kujibu sala za waumini wa Kanisa. Malaika alimwuliza Alma Mdogo sababu ya kupigana dhidi ya Kanisa.

Picha
Alma Mdogo

Ardhi ilitetemeka malaika alipokuwa akimwambia Alma mdogo akome kuangamiza Kanisa.

Picha
wavulana wakianguka chini

Alma Mdogo na wana wa Mosia walianguka chini tena. Walikuwa wamemwona malaika, na walijua uwezo wa Mungu ulikuwa umetetemesha ardhi.

Picha
Alma Mdogo kwenye ardhi

Alma Mdogo alistaajabu kiasi cha kutoweza kuzungumza. Akawa mnyonge hata kwamba hakuweza kunyosha mikono yake.

Picha
Alma Mdogo akiwa amebebwa

Wana wa Mosia walimbeba Alma Mdogo kumpeleka kwa baba yake na kumwelezea kilichokuwa kimetokea kwao.

Picha
Alma akisali

Alma alikuwa na furaha. Alijua ya kwamba Mungu alikuwa amejibu sala zake.

Picha
Alma Mdogo kitandani

Alma aliwaita watu wengi pamoja ili washuhudie yale ambayo Bwana alikuwa amemtendea mwana wake na wana wa Mosia.

Picha
Alma akimbariki mwana wake

Alma, pamoja na viongozi wengine wa Kanisa, walifunga na kusali na kumwomba Mungu amsaidie Alma Mdogo apate nguvu tena.

Picha
Alma Mdogo akizungumza na Baba yake

Baada ya siku mbili kuchwa na kucha, Alma Mdogo aliweza kuongea na kusimama.

Picha
Alma Mdogo akizungumza na wengine

Aliwaambia watu kwamba alikuwa ametubu dhambi zake na Mungu alikuwa amemsamehe.

Picha
Alma Mdogo akifundisha

Alifundisha kwamba kila mtu ni lazima awe mwenye haki ili aweze kuingia katika ufalme wa Mungu. Pia alielezea kuhusu uchungu mkubwa alioteseka kwa ajili ya dhambi zake.

Picha
Alma Mdogo

Alma Mdogo alikuwa na furaha kwa sababu alikuwa ametubu na Mungu alikuwa amemsamehe. Alijua Mungu Alimpenda.

Picha
wanaume wakifundisha

Alma Mdogo na wana wa Mosia walianza kufundisha ukweli kote nchini, wakimwambia kila mtu yale waliyokuwa wameona na kusikia.

Picha
Alma Mdogo akiwafundisha watu

Walijaribu kurekebisha makosa waliyokuwa wamefanya. Waliwafafanulia watu maandiko na kuwafundisha kuhusu Yesu Kristo.

Picha
Alma Mdogo akiwabatiza wengine

Mungu aliwabariki Alma Mdogo na wana wa Mosia walipokuwa wakifundisha injili. Watu wengi waliwasikiliza na wakaamini.

Chapisha