Sura ya 18
Alma Mdogo Anatubu
Mfalme Mosia alimteua Alma kuwa kiongozi wa Kanisa kule Zarahemla. Alma kisha akawachagua watu wengine kumsaidia kuwafundisha Wanefi.
Alma na Mfalme Mosia walikuwa na wasi wasi kwa sababu wasioamini walikuwa wakisababisha mateso kwa waumini wa Kanisa kwa sababu ya imani yao.
Alma alikuwa na mwana wa kiume aliyeitwa Alma. Alma Mdogo hakuamini mafundisho ya baba yake na akawa mtu muovu.
Alma Mdogo na wana wanne wa Mfalme Mosia walipigana dhidi ya Kanisa. Waliwashawishi watu wengi kuacha Kanisa na kuwa waovu.
Alma alisali kwamba mwanawe angejua ukweli na kutubu.
Alma Mdogo na wana wa Mfalme Mosia waliendelea kujaribu kuliangamiza Kanisa.
Siku moja malaika aliwatokea. Malaika alizungumza kwa sauti kubwa ambayo ilitetemesha ardhi.
Wavulana hao watano walikuwa na hofu kiasi kwamba walianguka chini. Mara ya kwanza hawakuelewa kile malaika alichokuwa akisema.
Malaika alikuwa amekuja kujibu sala za waumini wa Kanisa. Malaika alimwuliza Alma Mdogo sababu ya kupigana dhidi ya Kanisa.
Ardhi ilitetemeka malaika alipokuwa akimwambia Alma mdogo akome kuangamiza Kanisa.
Alma Mdogo na wana wa Mosia walianguka chini tena. Walikuwa wamemwona malaika, na walijua uwezo wa Mungu ulikuwa umetetemesha ardhi.
Alma Mdogo alistaajabu kiasi cha kutoweza kuzungumza. Akawa mnyonge hata kwamba hakuweza kunyosha mikono yake.
Wana wa Mosia walimbeba Alma Mdogo kumpeleka kwa baba yake na kumwelezea kilichokuwa kimetokea kwao.
Alma alikuwa na furaha. Alijua ya kwamba Mungu alikuwa amejibu sala zake.
Alma aliwaita watu wengi pamoja ili washuhudie yale ambayo Bwana alikuwa amemtendea mwana wake na wana wa Mosia.
Alma, pamoja na viongozi wengine wa Kanisa, walifunga na kusali na kumwomba Mungu amsaidie Alma Mdogo apate nguvu tena.
Baada ya siku mbili kuchwa na kucha, Alma Mdogo aliweza kuongea na kusimama.
Aliwaambia watu kwamba alikuwa ametubu dhambi zake na Mungu alikuwa amemsamehe.
Alifundisha kwamba kila mtu ni lazima awe mwenye haki ili aweze kuingia katika ufalme wa Mungu. Pia alielezea kuhusu uchungu mkubwa alioteseka kwa ajili ya dhambi zake.
Alma Mdogo alikuwa na furaha kwa sababu alikuwa ametubu na Mungu alikuwa amemsamehe. Alijua Mungu Alimpenda.
Alma Mdogo na wana wa Mosia walianza kufundisha ukweli kote nchini, wakimwambia kila mtu yale waliyokuwa wameona na kusikia.
Walijaribu kurekebisha makosa waliyokuwa wamefanya. Waliwafafanulia watu maandiko na kuwafundisha kuhusu Yesu Kristo.
Mungu aliwabariki Alma Mdogo na wana wa Mosia walipokuwa wakifundisha injili. Watu wengi waliwasikiliza na wakaamini.