Sura ya 2
Lehi Anawaonya Watu
Wengi kati ya watu waliokuwa wakiishi Yerusalemu miaka 600 kabla ya kuzaliwa kwa Kristo walikuwa waovu. Mungu aliwatuma manabii wawaambie watubu, lakini hawakutaka kusikiliza.
Lehi alikuwa nabii. Alisali ili watu watubu. Alipokuwa akisali, nguzo ya moto ilitokea. Mungu alimwambia na kumwonyesha Lehi vitu vingi.
Lehi alirudi nyumbani na akapata ono. Alimwona Mungu akiwa amezungukwa na malaika wengi. Malaika walikuwa wakiimba na kumsifu Mungu.
Katika ono lake Lehi alipewa kitabu kilichozungumzia kitu ambacho kingetokea katika siku zijazo. Alisoma kwamba Yerusalemu ingeangamizwa kwa sababu watu walikuwa waovu.
Lehi aliwaambia watu kwamba Yerusalemu itaangamizwa. Pia alizungumza kuhusu ujio wa Yesu. Watu walikuwa na hasira na walijaribu kumuua Lehi, lakini Bwana alimkinga.