Sura ya 21
Waamlisi
Amlisi alikuwa mtu mjanja, na mwovu ambaye alitaka kuwa mfalme wa Wanefi. Alikuwa na wafuasi wengi.
Wanefi wenye haki hawakumtaka Amlisi kuwa mfalme wao. Walijua alitaka kuliharibu Kanisa la Mungu.
Wanefi walijikusanya katika makundi kuamua kama Amlisi angekuwa mfalme. Watu wengi walipiga kura kumpinga Amlisi, na hakuwa mfalme.
Amlisi na wafuasi wake walikasirika. Walijitenga kutoka kwa Wanefi na wakamfanya Amlisi kuwa mfalme wao, na kujiita Waamlisi. Amlisi aliwaamrisha kupigana na Wanefi.
Wanefi wenye haki walijiandaa kujilinda wao wenyewe kwa pinde na mishale, panga na silaha zingine.
Waamlisi walivamia, na Wanefi, ambao walikuwa wakiongozwa na Alma na kuimarishwa na Bwana, waliwaua wengi wa Waamlisi. Waamlisi waliobaki walikimbia.
Alma aliwatuma wapelelezi kuwatazama waamlisi. Wapelelezi waliwaona wakiungana na jeshi kubwa la Walamani na kuwavamia Wanefi walioishi Zarahemla.
Wanefi walisali, na Mungu aliwasaidia tena. Waliwaua wengi wa wanajeshi wa jeshi la Walamani–Waamlisi.
Alma na Amlisi walipigana kwa panga. Alma alisali kwamba maisha yake yangelindwa, na Mungu alimpa nguvu za kumuua Amlisi.
Wanefi waliwafukuzia Walamani na Waamlisi nyikani. Wengi wa waliojeruhiwa walikufa na waliliwa na wanyama wa mwituni.
Kama walamani, Waamlisi walijichora kwa rangi nyekundu, kitu ambacho kilitimiza unabii. Waamlisi walikuwa wamejitenga wao wenyewe kutoka kwenye baraka za injili.