Scripture Stories
Sura ya 21: Waamlisi


Sura ya 21

Waamlisi

Picha
Amlisi na wafuasi wake

Amlisi alikuwa mtu mjanja, na mwovu ambaye alitaka kuwa mfalme wa Wanefi. Alikuwa na wafuasi wengi.

Picha
Watu wakimwangalia Amlisi

Wanefi wenye haki hawakumtaka Amlisi kuwa mfalme wao. Walijua alitaka kuliharibu Kanisa la Mungu.

Picha
Wanefi wakiongea

Wanefi walijikusanya katika makundi kuamua kama Amlisi angekuwa mfalme. Watu wengi walipiga kura kumpinga Amlisi, na hakuwa mfalme.

Picha
Amlisi na wafuasi wake

Amlisi na wafuasi wake walikasirika. Walijitenga kutoka kwa Wanefi na wakamfanya Amlisi kuwa mfalme wao, na kujiita Waamlisi. Amlisi aliwaamrisha kupigana na Wanefi.

Picha
Wanefi wakitengeneza mishale

Wanefi wenye haki walijiandaa kujilinda wao wenyewe kwa pinde na mishale, panga na silaha zingine.

Picha
Wanefi wanawashinda Waamlisi

Waamlisi walivamia, na Wanefi, ambao walikuwa wakiongozwa na Alma na kuimarishwa na Bwana, waliwaua wengi wa Waamlisi. Waamlisi waliobaki walikimbia.

Picha
Wapelelezi wa Alma wakiwatazama Wamlisi

Alma aliwatuma wapelelezi kuwatazama waamlisi. Wapelelezi waliwaona wakiungana na jeshi kubwa la Walamani na kuwavamia Wanefi walioishi Zarahemla.

Picha
Wanefi wakipigana na jeshi la Walamani–Waamlisi

Wanefi walisali, na Mungu aliwasaidia tena. Waliwaua wengi wa wanajeshi wa jeshi la Walamani–Waamlisi.

Picha
Alma akimuua Amlisi

Alma na Amlisi walipigana kwa panga. Alma alisali kwamba maisha yake yangelindwa, na Mungu alimpa nguvu za kumuua Amlisi.

Picha
vita

Wanefi waliwafukuzia Walamani na Waamlisi nyikani. Wengi wa waliojeruhiwa walikufa na waliliwa na wanyama wa mwituni.

Picha
Waamlisi wakijichora kwenye paji za nyuso

Kama walamani, Waamlisi walijichora kwa rangi nyekundu, kitu ambacho kilitimiza unabii. Waamlisi walikuwa wamejitenga wao wenyewe kutoka kwenye baraka za injili.

Chapisha