Sura ya 13
Zenivu
Zenivu na kundi la Wanefi waliondoka manyumbani kwao kule Zarahemla na kusafiri kuelekea nchi ya Nefi, ambapo Wanefi wengine walikuwa wameishi kwa wakati fulani.
Waliwakuta Walamani wakiishi huko. Zenivu na watu wake wanne walienda mjini kuzungumza na mfalme. Walimuuliza Mfalme Lamani kama wangeweza kuishi katika nchi yake.
Mfalme Lamani alisema wangeweza kuchukua miwili kati ya miji yake. Mfalme alitaka waishi katika nchi yake ili wawe watumwa wake.
Watu wa Zenivu walijenga nyumba na kuimarisha kuta zilizozingira miji yao. Walipanda aina nyingi ya nafaka na matunda. Pia walikuwa na mifugo wengi.
Mfalme Lamani aliwaambia watu wake kwamba Wanefi walikuwa wameanza kuwa na nguvu sana. Baadaye kidogo Walamani wengi walienda kuwavamia Wanefi na kuiba mifugo na mimea yao.
Wanefi walikimbilia mji wa Nefi. Huko Zenivu aliwahami watu kwa pinde na mishale, panga, rungu, na kombeo. Walienda kupigana na Walamani.
Kabla ya wao kupigana, Wanefi walisali, wakiomba msaada kutoka kwa Mungu. Mungu aliwabariki Wanefi na nguvu za ziada, na waliwashinda Walamani.
Baada ya vita, Zenivu aliwaweka walinzi pembeni mwa miji ya Wanefi. Alitaka kuwalinda watu wake pamoja na mifugo yao kutokana na Walamani.
Wanefi waliishi kwa amani kwa miaka mingi. Wanaume walifanya kazi katika mashamba, na wanawake walisokota nyuzi na kutengeneza nguo.
Mfalme Lamani alifariki na mwanawe akawa mfalme. Mfalme mpya alituma jeshi lake kupigana na Wanefi.
Wanefi tena walipokea nguvu kutoka kwa Bwana. Waliwaua Walamani wengi, na waliobaki walitoroka.