Scripture Stories
Sura ya 13: Zenivu


Sura ya 13

Zenivu

Picha
Wanefi wakitembea

Zenivu na kundi la Wanefi waliondoka manyumbani kwao kule Zarahemla na kusafiri kuelekea nchi ya Nefi, ambapo Wanefi wengine walikuwa wameishi kwa wakati fulani.

Picha
Wanefi wakizungumza na Mfalme Lamani

Waliwakuta Walamani wakiishi huko. Zenivu na watu wake wanne walienda mjini kuzungumza na mfalme. Walimuuliza Mfalme Lamani kama wangeweza kuishi katika nchi yake.

Picha
Mfalme Lamani

Mfalme Lamani alisema wangeweza kuchukua miwili kati ya miji yake. Mfalme alitaka waishi katika nchi yake ili wawe watumwa wake.

Picha
Wanefi wakipanda

Watu wa Zenivu walijenga nyumba na kuimarisha kuta zilizozingira miji yao. Walipanda aina nyingi ya nafaka na matunda. Pia walikuwa na mifugo wengi.

Picha
Walamani wakiwavamia Wanefi

Mfalme Lamani aliwaambia watu wake kwamba Wanefi walikuwa wameanza kuwa na nguvu sana. Baadaye kidogo Walamani wengi walienda kuwavamia Wanefi na kuiba mifugo na mimea yao.

Picha
Wanefi wakikimbia

Wanefi walikimbilia mji wa Nefi. Huko Zenivu aliwahami watu kwa pinde na mishale, panga, rungu, na kombeo. Walienda kupigana na Walamani.

Picha
Wanefi wakisali

Kabla ya wao kupigana, Wanefi walisali, wakiomba msaada kutoka kwa Mungu. Mungu aliwabariki Wanefi na nguvu za ziada, na waliwashinda Walamani.

Picha
mlinzi pamoja na kondoo

Baada ya vita, Zenivu aliwaweka walinzi pembeni mwa miji ya Wanefi. Alitaka kuwalinda watu wake pamoja na mifugo yao kutokana na Walamani.

Picha
wanawake wakifuma

Wanefi waliishi kwa amani kwa miaka mingi. Wanaume walifanya kazi katika mashamba, na wanawake walisokota nyuzi na kutengeneza nguo.

Picha
vita

Mfalme Lamani alifariki na mwanawe akawa mfalme. Mfalme mpya alituma jeshi lake kupigana na Wanefi.

Picha
Wanefi wakiwatazama Walamani

Wanefi tena walipokea nguvu kutoka kwa Bwana. Waliwaua Walamani wengi, na waliobaki walitoroka.

Chapisha