Scripture Stories
Sura ya 47: Yesu Kristo Anawabariki Wanafunzi Wake


Sura ya 47

Yesu Kristo Anawabariki Wanafunzi Wake

Picha
Yesu na wanafunzi

Siku moja wakati wanafunzi walikuwa kwa pamoja wamefunga na kusali, Yesu Kristo aliwajia.

Picha
Kristo akizungumza na wanafunzi

Wanafunzi walimwuliza jina watakaloliita Kanisa. Yesu alisema kwamba liitwe kwa jina Lake kwa maana ni Kanisa Lake.

Picha
Yesu akizungumza na wanafunzi

Yesu Kristo aliwaelezea wanafunzi Wake kwamba Baba wa Mbinguni alikuwa amemtuma duniani kutoa uhai Wake kwa ajili ya watu wote.

Picha
Kristo akizungumza na wanafunzi

Alisema kila mtu ambaye anatubu, anabatizwa katika jina Lake, na kutii amri Zake hatapatikana na hatia mbele za Baba wa Mbinguni.

Picha
Kristo akizungumza na wanafunzi

Mwokozi aliwaambia wanafunzi wafanye vitu walivyokuwa wameona akifanya. Alikuwa amewapa mfano.

Picha
Kristo akizungumza kuhusu maandiko

Pia aliwaambia waandike yale waliyokuwa wameyaona na kusikia ili wengine wajue kuyahusu.

Picha
Kristo na mwanafunzi

Yesu aliwauliza wanafunzi Wake kitu walichohitaji kutoka Kwake. Tisa kati yao walitaka kuwa naye baada ya maisha yao duniani kukamilika.

Picha
Yesu na wanafunzi

Yesu aliwaahidi ya kwamba watakapofikisha umri wa miaka 72, wangejiunga naye mbinguni.

Picha
Yesu na wanafunzi watatu

Wale wanafunzi wengine watatu hawakuthubutu kuuliza kile walichokitaka, lakini Yesu alijua. Walitaka kubaki duniani na kufundisha injili hadi Yesu atakaporudi tena.

Picha
Mwokozi na wanafunzi

Mwokozi aliwaahidi kwamba hawangepata maumivu ya kimwili au huzuni na hawangefariki. Wangewafudisha watu injili hadi atakaporudi.

Picha
Yesu akiondoka

Yesu alimgusa kila mwanafunzi isipokuwa wale watatu ambao wangebaki duniani. Kisha akaondoka.

Picha
wanafunzi watatu wanachukuliwa mbinguni

Wale wanafunzi watatu walichukuliwa mbinguni, ambapo waliona na kusikia vitu vingi vya ajabu. Walikuwa na uwezo bora wa kuelewa vitu vya Mungu.

Picha
wanafunzi watatu

Miili yao iligeuzwa ili wasife.

Picha
wanafunzi wakiwabatiza wengine

Wanafunzi watatu walirudi duniani na kuanza kuhubiri na kubatiza.

Picha
Wanafunzi watatu ndani ya shimo lenye kina

Wanefi waovu waliwatupa wanafunzi watatu gerezani na katika mashimo yenye kina, lakini uwezo wa Mungu uliwawezesha kutoroka.

Picha
wanafunzi wakisukumwa ndani ya tanuu

Wakati walipotupwa katika tanuu na mashimo pamoja na wanyama wa mwitu, walilindwa pia na uwezo wa Mungu.

Picha
wanafunzi wakiwahubiria watu

Wale wanafunzi watatu waliendelea kuhubiri injili ya Yesu Kristo miongoni mwa Wanefi. Bado wanaendelea kuhubiri injili Yake.

Chapisha