Scripture Stories
Mlango wa 12: Mfalme Benyamini


Sura ya 12

Mfalme Benyamini

Picha
Mfalme Benyamini anafundisha

Mfalme Benyamini alikuwa mfalme Mnefi mwenye haki. Kwa usaidizi wa wanaume wengine wenye haki, alisababisha kuwe na amani nchini.

Picha
Mfalme Benyamini na Mosia

Mfalme Benyamini alizeeka na akataka kuzungumza na watu wake. Alitaka kuwaambia kuwa mwanawe Mosia ndiye angekuwa mfalme anayefuata.

Picha
watu wakikusanyika karibu na hekalu

Watu walikuja kutoka kote nchini na kukusanyika karibu na hekalu. Waliweka mahema yao kwamba milango ilitazama hekalu.

Picha
Mfalme Benyamini anazungumza

Mfalme Benyamini alizungumza kutoka juu ya mnara ili Wanefi waweze kumsikia.

Picha
Wanefi

Aliwaambia watu wake kwamba alikuwa amejitahidi kwa kadiri ya uwezo wake kuwatumikia. Alisema njia ya kumtumikia Mungu ni kwa kutumikiana.

Picha
Mfalme Benyamini

Mfalme Benyamini aliwaambia watu watii amri za Mungu. Wale wanaotii amri kwa uaminifu watakuwa na furaha na siku moja wataishi na Mungu.

Picha
mtoto Yesu na Maria

Mfalme Benyamini alisema Yesu Kristo angezaliwa duniani karibuni. Jina la mama yake lingekuwa Mariamu.

Picha
Yesu akitenda miujiza

Yesu angetenda miujiza. Angewaponya wagonjwa na kuwarudishia uhai wafu. Angewafanya vipofu kuona na viziwi kusikia.

Picha
Yesu akisali

Yesu angeteseka na kufa kwa ajili ya dhambi za watu wote. Wale wanaotubu na kuwa na imani katika Yesu watasamehewa dhambi zao.

Picha
Yesu anasulubiwa

Mfalme Benyamini aliwaambia Wanefi kwamba watu waovu wangempiga Yesu mijeledi. Kisha wangemsulubisha.

Picha
Yesu afufuka

Baada ya siku tatu Yesu angefufuka.

Picha
Wanefi wakitubu

Baada ya Mfalme Benyamini kuzungumza, Wanefi walianguka ardhini. Walihuzunika kwa ajili ya dhambi zao na walitaka kutubu.

Picha
watu wakisali

Watu walikuwa na imani katika Yesu Kristo, na walisali kwa ajili ya msamaha.

Picha
Wanefi wakitabasamu

Roho Mtakatifu alijaza mioyo yao. Walifahamu ya kwamba Mungu alikuwa amewasamehe na kwamba aliwapenda. Walihisi amani na furaha.

Picha
Mfalme Benyamini akizungumza na watu

Mfalme Benyamini aliwaambia watu wake wamwamini Mungu. Aliwataka wafahamu kwamba Mungu alikuwa ameumba vitu vyote na kwamba yeye ni mwenye hekima na mwenye nguvu.

Picha
familia ikisali

Mfalme Benyamini aliwaambia watu wanyenyekee na kusali kila siku. Aliwataka watu wake daima wamkumbuke Mungu na wawe waaminifu.

Picha
Mfalme Benyamini anazungumza

Aliwaambia wazazi wasikubali watoto wao wapigane au wazozane.

Picha
wazazi wakiwafundisha watoto

Aliwaambia wawafundishe watoto wao kuwa watiifu na wapendane na kutumikiana mmoja kwa mwingine.

Picha
Wanefi wakimsikiliza Mfalme Benyamini

Aliwaonya watu wawe waangalifu na fikira zao, maneno yao, na vitendo vyao. Walihitajika kuwa waaminifu na kutii amri kwa muda uliobaki katika maisha yao.

Picha
Mfalme Benyamini akizungumza na watu

Mfalme Benyamini aliwauliza watu ikiwa waliamini mahubiri yake. Wote walisema ndio. Roho Mtakatifu alikuwa amewabadili, na hawakutaka kutenda dhambi tena.

Picha
Wanefi wakitabasamu

Wote walifanya maagano, au waliahidi, kutii amri za Mungu. Mfalme Benyamini alifurahishwa.

Picha
Mfalme Benyamini akimbariki Mosia

Mfalme Benyamini alimpa mwana wake Mosia haki ya kuwa mfalme mpya. Miaka mitatu baadaye Mfalme Benyamini alifariki.

Picha
Mosia akifanya kazi

Mosia alikuwa mfalme mwema. Alifanya kazi kwa bidii na kuwatumikia watu wake, jinsi alivyofanya baba yake.

Chapisha