Sura ya 3
Lehi Anaondoka Yerusalemu
Bwana alipendezwa na Lehi na usiku mmoja alizungumza naye katika ndoto. Alimwambia Lehi kwamba achukuwe familia yake na aondoke Yerusalemu. Lehi alimtii Bwana.
Familia ya Lehi walibeba chakula na mahema. Waliiacha nyumba yao na dhahabu na fedha na kusafiri nyikani.
Lehi na mkewe, Saria, walikuwa na wana wanne. Majina yao yalikuwa Lamani, Lemueli, Samu, na Nefi.
Baada ya kusafiri kwa siku tatu, familia ya Lehi iliweka kambi bondeni karibu na mto.
Lehi alijenga madhabahu ya mawe na kutoa sadaka kwa Mungu. Alimshukuru Mungu kwa kuiokoa familia yake kutoangamizwa.
Lehi aliupa mto jina Lamani na akaliita bonde Lemueli. Lehi aliwataka wanawe wawe kama mto na bonde, daima ukitiririka kwa Mungu na imara kutii amri.
Lamani na Lemueli walidhani baba yao alikuwa mpumbavu kwa kuondoka Yerusalemu na kuacha mali yao. Hawakuamini ya kwamba Yerusalemu itaangamizwa.
Nefi alitaka kuelewa vitu ambavyo Lehi alikuwa ameviona. Alisali ili ajue kama baba yake alikuwa amefanya jambo zuri kuondoka Yerusalemu.
Yesu Kristo alimtokea Nefi na kumweleza kwamba maneno ya Lehi yalikuwa ya kweli. Nefi aliamini na hakukaidi kama Lamani na Lemueli walivyofanya.
Nefi aliwaelezea kaka zake kile ambacho Yesu alikuwa amemwambia. Samu alimwamini Nefi, lakini Lamani na Lemueli hawakumwamini.
Bwana alimwahidi Nefi kwamba angebarikiwa kwa sababu ya imani yake. Angekuwa kiongozi wa kaka zake.