Scripture Stories
Mlango wa 3: Lehi Anaondoka Yerusalemu


Sura ya 3

Lehi Anaondoka Yerusalemu

Picha
Ndoto ya Lehi kuhusu safari

Bwana alipendezwa na Lehi na usiku mmoja alizungumza naye katika ndoto. Alimwambia Lehi kwamba achukuwe familia yake na aondoke Yerusalemu. Lehi alimtii Bwana.

Picha
familia nyikani

Familia ya Lehi walibeba chakula na mahema. Waliiacha nyumba yao na dhahabu na fedha na kusafiri nyikani.

Picha
Lehi, Saria, na wana wanne

Lehi na mkewe, Saria, walikuwa na wana wanne. Majina yao yalikuwa Lamani, Lemueli, Samu, na Nefi.

Picha
mahema na familia

Baada ya kusafiri kwa siku tatu, familia ya Lehi iliweka kambi bondeni karibu na mto.

Picha
Lehi na madhabahu

Lehi alijenga madhabahu ya mawe na kutoa sadaka kwa Mungu. Alimshukuru Mungu kwa kuiokoa familia yake kutoangamizwa.

Picha
Lehi, Lamani, na Lemueli

Lehi aliupa mto jina Lamani na akaliita bonde Lemueli. Lehi aliwataka wanawe wawe kama mto na bonde, daima ukitiririka kwa Mungu na imara kutii amri.

Picha
Lamani na Lemueli

Lamani na Lemueli walidhani baba yao alikuwa mpumbavu kwa kuondoka Yerusalemu na kuacha mali yao. Hawakuamini ya kwamba Yerusalemu itaangamizwa.

Picha
Nefi akisali

Nefi alitaka kuelewa vitu ambavyo Lehi alikuwa ameviona. Alisali ili ajue kama baba yake alikuwa amefanya jambo zuri kuondoka Yerusalemu.

Picha
Nefi akisali

Yesu Kristo alimtokea Nefi na kumweleza kwamba maneno ya Lehi yalikuwa ya kweli. Nefi aliamini na hakukaidi kama Lamani na Lemueli walivyofanya.

Picha
Nefi akizungumza na Samu

Nefi aliwaelezea kaka zake kile ambacho Yesu alikuwa amemwambia. Samu alimwamini Nefi, lakini Lamani na Lemueli hawakumwamini.

Picha
Nefi akizungumza na kaka zake

Bwana alimwahidi Nefi kwamba angebarikiwa kwa sababu ya imani yake. Angekuwa kiongozi wa kaka zake.

Chapisha