Scripture Stories
Sura ya 15: Alma Anafundisha na Kubatiza


Sura ya 15

Alma Anafundisha na Kubatiza

Picha
Alma akiandika

Alma alitoroka kutoka kwa watumishi wa Mfalme Nuhu na kujificha kwa siku nyingi. Wakati amejificha, aliandika kile nabii Abinadi alikifundisha.

Picha
Alma akiwafundisha wengine

Alma alitubu dhambi zake na kwenda kwa Wanefi kwa siri, akiwafundisha wao ujumbe wa Abinadi. Alma aliwaambia watu wawe na imani kwa Yesu Kristo na watubu.

Picha
Alma

Wakati wa mchana Alma alijificha katika msitu karibu na kijito kilichoitwa Maji ya Mormoni.

Picha
Alma akiwabatiza wengine

Wale walioamini mafundisho ya Alma walikwenda kwenye Maji ya Mormoni na walibatizwa. Alma alibatiza watu 204 kwenye Kanisa la Kristo.

Picha
Alma akitawaza makuhani

Alma aliwatawaza makuhani kuwafundisha watu. Aliwaambia makuhani kufundisha toba na imani katika Yesu Kristo. Aliwaambia pia lazima wasibishane lakini wawe wamoja.

Picha
Watu wakishirikiana

Watu wa Alma walipendana na kutumikiana. Walishiriki kila kitu walichokuwa nacho na walikuwa wenye shukrani kwamba walijifunza kuhusu Yesu Kristo, mwokozi wao.

Picha
Watumishi wa Nuhu wakimpeleleza Alma

Watumishi wa Mfalme Nuhu walimuona Alma akiwafundisha watu. Mfalme alisema Alma alikuwa akiigeuza mioyo ya Wanefi dhidi yake, hivyo alituma jeshi kuwauwa.

Picha
Alma na wengine wakitoroka

Mungu alimuonya Alma kwamba jeshi la Mfalme Nuhu lilikuwa linakuja. Watu walizikusanya familia zao, mifugo, na mali zingine na kutorokea nyikani.

Picha
Wanajeshi wa Mfalme Nuhu

Mungu aliwaimarisha watu wa Alma kwamba wangeweza kutoroka kutoka kwa jeshi la Mfalme. Jeshi liliwatafuta lakini halikuwapata.

Picha
Watu wakipanda

Baada ya kusafiri nyikani kwa siku nne, watu wa Alma walifika kwenye eneo zuri ambalo lilikuwa na maji safi yakitiririka. Hapo walipanda mazao na kujenga majengo.

Picha
Alma akiongea na wengine

Watu walitaka Alma awe mfalme wao, lakini Alma alisema Mungu hakutaka wao wawe na mfalme. Mungu alitaka wao wawe huru.

Chapisha