Sura ya 15
Alma Anafundisha na Kubatiza
Alma alitoroka kutoka kwa watumishi wa Mfalme Nuhu na kujificha kwa siku nyingi. Wakati amejificha, aliandika kile nabii Abinadi alikifundisha.
Alma alitubu dhambi zake na kwenda kwa Wanefi kwa siri, akiwafundisha wao ujumbe wa Abinadi. Alma aliwaambia watu wawe na imani kwa Yesu Kristo na watubu.
Wakati wa mchana Alma alijificha katika msitu karibu na kijito kilichoitwa Maji ya Mormoni.
Wale walioamini mafundisho ya Alma walikwenda kwenye Maji ya Mormoni na walibatizwa. Alma alibatiza watu 204 kwenye Kanisa la Kristo.
Alma aliwatawaza makuhani kuwafundisha watu. Aliwaambia makuhani kufundisha toba na imani katika Yesu Kristo. Aliwaambia pia lazima wasibishane lakini wawe wamoja.
Watu wa Alma walipendana na kutumikiana. Walishiriki kila kitu walichokuwa nacho na walikuwa wenye shukrani kwamba walijifunza kuhusu Yesu Kristo, mwokozi wao.
Watumishi wa Mfalme Nuhu walimuona Alma akiwafundisha watu. Mfalme alisema Alma alikuwa akiigeuza mioyo ya Wanefi dhidi yake, hivyo alituma jeshi kuwauwa.
Mungu alimuonya Alma kwamba jeshi la Mfalme Nuhu lilikuwa linakuja. Watu walizikusanya familia zao, mifugo, na mali zingine na kutorokea nyikani.
Mungu aliwaimarisha watu wa Alma kwamba wangeweza kutoroka kutoka kwa jeshi la Mfalme. Jeshi liliwatafuta lakini halikuwapata.
Baada ya kusafiri nyikani kwa siku nne, watu wa Alma walifika kwenye eneo zuri ambalo lilikuwa na maji safi yakitiririka. Hapo walipanda mazao na kujenga majengo.
Watu walitaka Alma awe mfalme wao, lakini Alma alisema Mungu hakutaka wao wawe na mfalme. Mungu alitaka wao wawe huru.