Sura ya 10
Yakobo na Sheremu
Kabla ya Nefi kufariki alimpa ndugu yake mdogo Yakobo bamba alizokuwa ameziandika. Yakobo alikuwa mwenye haki.
Nefi alimwambia Yakobo aandike vitu ambavyo vingewasaidia watu kuamini katika Yesu Kristo.
Nefi alimpa Yakobo uwezo wa kuwa kuhani katika Kanisa na kuwafundisha Wanefi neno la Mungu.
Baada ya Nefi kufariki wengi kati ya Wanefi walikuwa waovu. Yakobo aliwafundisha watu na kuwaambia watubu uovu waliokuwa wakiutenda.
Mwanaume mwovu aliyeitwa Sheremu alizunguka miongoni mwa Wanefi, akiwafundisha wasiamini katika Yesu Kristo.
Sheremu aliwaambia watu kwamba hakungekuwepo na Kristo. Watu wengi walimwamini Sheremu.
Yakobo aliwafundisha watu kuamini katika Kristo. Sheremu alitaka kubishana na Yakobo na kumshawishi kwamba hakungekuwepo na Kristo.
Imani ya Yakobo katika Yesu Kristo haingeweza kutikisika. Alikuwa amewaona malaika na alikuwa ameisikia sauti ya Bwana. Alijua kwamba Yesu angekuja.
Roho Mtakatifu alikuwa na Yakobo alipokuwa akishiriki ushuhuda wake wa Yesu Kristo kwa Sheremu.
Sheremu alitaka kuona ishara. Alitaka Yakobo athibitishe kwamba kuna Mungu. Alitaka kuona muujiza.
Yakobo alikataa kumuomba Mungu aonyeshe ishara. Alisema Sheremu tayari alijua kwamba kile Yakobo acholikuwa amefundisha kilikuwa kweli.
Yakobo alisema ikiwa Mungu angempiga Sheremu, hiyo ingekuwa ishara ya uwezo wa Mungu.
Sheremu mara moja akaanguka chini. Hakuweza kusimama kwa kipindi cha siku nyingi.
Sheremu alikuwa mdhaifu na alijua alikuwa anakaribia kifo. Aliwaita watu pamoja.
Aliwaambia kwamba alikuwa amedanganya. Aliwaambia waamini katika Yesu Kristo.
Baada ya Sheremu kumaliza kuongea na watu, alifariki. Watu walihisi nguvu za Mungu, na waliinama kwenye ardhi.
Watu walianza kutubu na kusoma maandiko. Waliishi kwa amani na upendo. Yakobo alikuwa na furaha na alijua ya kwamba Mungu alikuwa amejibu sala zake.