Scripture Stories
Sura ya 10: Yakobo na Sheremu


Sura ya 10

Yakobo na Sheremu

Picha
Nefi akimpa Yakobo bamba

Kabla ya Nefi kufariki alimpa ndugu yake mdogo Yakobo bamba alizokuwa ameziandika. Yakobo alikuwa mwenye haki.

Picha
Yakobo akiandika kwenye bamba

Nefi alimwambia Yakobo aandike vitu ambavyo vingewasaidia watu kuamini katika Yesu Kristo.

Picha
Nefi akimbariki Yakobo

Nefi alimpa Yakobo uwezo wa kuwa kuhani katika Kanisa na kuwafundisha Wanefi neno la Mungu.

Picha
Yakobo akiwafundisha watu

Baada ya Nefi kufariki wengi kati ya Wanefi walikuwa waovu. Yakobo aliwafundisha watu na kuwaambia watubu uovu waliokuwa wakiutenda.

Picha
Sheremu anafundisha

Mwanaume mwovu aliyeitwa Sheremu alizunguka miongoni mwa Wanefi, akiwafundisha wasiamini katika Yesu Kristo.

Picha
Sheremu

Sheremu aliwaambia watu kwamba hakungekuwepo na Kristo. Watu wengi walimwamini Sheremu.

Picha
Sheremu akibishana na Yakobo

Yakobo aliwafundisha watu kuamini katika Kristo. Sheremu alitaka kubishana na Yakobo na kumshawishi kwamba hakungekuwepo na Kristo.

Picha
Yakobo na Sheremu

Imani ya Yakobo katika Yesu Kristo haingeweza kutikisika. Alikuwa amewaona malaika na alikuwa ameisikia sauti ya Bwana. Alijua kwamba Yesu angekuja.

Picha
Yakobo akimshuhudia Sheremu

Roho Mtakatifu alikuwa na Yakobo alipokuwa akishiriki ushuhuda wake wa Yesu Kristo kwa Sheremu.

Picha
Sheremu akitaka ishara

Sheremu alitaka kuona ishara. Alitaka Yakobo athibitishe kwamba kuna Mungu. Alitaka kuona muujiza.

Picha
Yakobo

Yakobo alikataa kumuomba Mungu aonyeshe ishara. Alisema Sheremu tayari alijua kwamba kile Yakobo acholikuwa amefundisha kilikuwa kweli.

Picha
Yakobo na Sheremu

Yakobo alisema ikiwa Mungu angempiga Sheremu, hiyo ingekuwa ishara ya uwezo wa Mungu.

Picha
Sheremu akianguka chini

Sheremu mara moja akaanguka chini. Hakuweza kusimama kwa kipindi cha siku nyingi.

Picha
Sheremu

Sheremu alikuwa mdhaifu na alijua alikuwa anakaribia kifo. Aliwaita watu pamoja.

Picha
Sheremu akizungumza na watu

Aliwaambia kwamba alikuwa amedanganya. Aliwaambia waamini katika Yesu Kristo.

Picha
Sheremu

Baada ya Sheremu kumaliza kuongea na watu, alifariki. Watu walihisi nguvu za Mungu, na waliinama kwenye ardhi.

Picha
Yakobo na wengine

Watu walianza kutubu na kusoma maandiko. Waliishi kwa amani na upendo. Yakobo alikuwa na furaha na alijua ya kwamba Mungu alikuwa amejibu sala zake.

Chapisha