Sura ya 42
Ishara za Kusulubiwa kwa Kristo
Miaka thelathini na tatu ilikuwa imepita tangu watu walipokuwa wameziona ishara za kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Sasa walisubiri kuona ishara ya kifo chake: siku tatu za giza.
Baadhi hawakuamini kwamba ishara hii ingeonekana. Walibishana na wale walioamini.
Siku moja dhoruba kali ilikuja. Kulikuwa na upepo mkali.
Radi iliwaka, na ngurumo ilitetemesha dunia nzima.
Mji wa Zarahemla uliwaka moto. Mji wa Moroni ulizama baharini. Mji wa Moroniha ulifunikwa na ardhi.
Tetemeko la ardhi litetemesha dunia nzima. Barabara kuu ziliharibiwa, na majengo yakaanguka. Miji mingi iliharibiwa, na watu wengi waliuwawa.
Dhoruba na tetemeko la ardhi vilidumu kwa takriban masaa matatu.
Wakati dhoruba na tetemeko la ardhi vilipokoma, giza lilitanda nchini. Hapakuwa na mwangaza mahali popote. Watu hata waliweza kuhisi giza hilo.
Giza lilidumu kwa muda wa siku tatu. Mishumaa haikuwaka, na watu hawakuweza kuliona jua, mwezi, au nyota.
Watu walilia kwa sababu ya giza, uharibifu, na mauti. Walisikitika kwa kuwa hawakuwa wametubu dhambi zao.
Kisha watu wakasikia sauti ya Yesu Kristo.
Yesu aliwaambia kuhusu uharibifu mkuu katika nchi. Alisema kwamba watu waovu zaidi walikuwa wameangamizwa.
Alisema kwamba wale ambao walikuwa wamenusurika walihitaji kutubu. Kama wangefanya hivyo na kuja kwake, angewabariki.
Watu walistaajabu baada ya kuisikia sauti hadi wakaacha kulia. Kulikuwa na kimya kwa masaa mengi.
Kisha Yesu akazungumza tena, akisema mara nyingi alikuwa amejaribu kuwasaidia watu. Kama wangetubu hivi sasa, bado wangeweza kurudi kwake.
Baada ya siku tatu giza liliondoka. Watu walisherehekea na kumshukuru Bwana kwa Shangwe.