Scripture Stories
Sura ya 42: Ishara za Kusubiwa kwa Kristo


Sura ya 42

Ishara za Kusulubiwa kwa Kristo

Picha
mwanaume akiwa amemshika msichana mkono

Miaka thelathini na tatu ilikuwa imepita tangu watu walipokuwa wameziona ishara za kuzaliwa kwa Yesu Kristo.

Picha
watu wakiangalia juu angani

Sasa walisubiri kuona ishara ya kifo chake: siku tatu za giza.

Picha
watu wakibishana

Baadhi hawakuamini kwamba ishara hii ingeonekana. Walibishana na wale walioamini.

Picha
wanaume ndani ya dhoruba

Siku moja dhoruba kali ilikuja. Kulikuwa na upepo mkali.

Picha
mwanaume ameketi

Radi iliwaka, na ngurumo ilitetemesha dunia nzima.

Picha
wanaume wakikimbia

Mji wa Zarahemla uliwaka moto. Mji wa Moroni ulizama baharini. Mji wa Moroniha ulifunikwa na ardhi.

Picha
mwanaume na watoto

Tetemeko la ardhi litetemesha dunia nzima. Barabara kuu ziliharibiwa, na majengo yakaanguka. Miji mingi iliharibiwa, na watu wengi waliuwawa.

Picha
dhoruba kote nchini

Dhoruba na tetemeko la ardhi vilidumu kwa takriban masaa matatu.

Picha
watu wakitembea gizani

Wakati dhoruba na tetemeko la ardhi vilipokoma, giza lilitanda nchini. Hapakuwa na mwangaza mahali popote. Watu hata waliweza kuhisi giza hilo.

Picha
familia gizani

Giza lilidumu kwa muda wa siku tatu. Mishumaa haikuwaka, na watu hawakuweza kuliona jua, mwezi, au nyota.

Picha
watu wakilia gizani

Watu walilia kwa sababu ya giza, uharibifu, na mauti. Walisikitika kwa kuwa hawakuwa wametubu dhambi zao.

Picha
watu katika giza

Kisha watu wakasikia sauti ya Yesu Kristo.

Picha
nchi iliyoharibiwa ikiwa katika giza

Yesu aliwaambia kuhusu uharibifu mkuu katika nchi. Alisema kwamba watu waovu zaidi walikuwa wameangamizwa.

Picha
watu wakisali gizani

Alisema kwamba wale ambao walikuwa wamenusurika walihitaji kutubu. Kama wangefanya hivyo na kuja kwake, angewabariki.

Picha
watu katika giza

Watu walistaajabu baada ya kuisikia sauti hadi wakaacha kulia. Kulikuwa na kimya kwa masaa mengi.

Picha
familia gizani

Kisha Yesu akazungumza tena, akisema mara nyingi alikuwa amejaribu kuwasaidia watu. Kama wangetubu hivi sasa, bado wangeweza kurudi kwake.

Picha
watu wakiangalia juu

Baada ya siku tatu giza liliondoka. Watu walisherehekea na kumshukuru Bwana kwa Shangwe.

Chapisha