Sehemu za Kujua
- Amerika
-
nchi ya ahadi ambayo kwayo Mungu aliwaelekeza familia ya Lehi na Wayaredi
- Amoniha
-
mji wa watu waovu ambao hawakumsikiliza Alma Mdogo na Amuleki
- Babeli
-
mji ambapo watu waovu walijenga mnara ili waweze kukwea mbinguni
- Bethlehemu
-
mji karibu na Yerusalemu ambapo Yesu Kristo alizaliwa
- Neema1
-
mahali ambapo familia ya Lehi ilikita kambi baada ya kusafiri nyikani kwa miaka minane. kutoka hapa walisafiri hadi nchi ya ahadi.
- Neema2
-
mahali ambapo Yesu Kristo alienda alipowatembelea Wanefi
- Mlima Kumora
-
mahali ambapo Moroni alizika bamba za dhahabu na Joseph Smith baadaye akazifichua
- Yershoni
-
nchi ambayo Wanefi waliwapa watu wa Amoni
- Yerusalemu
-
mji ambapo Lehi alitoa unabii kwa waovu na mahali ambapo Yesu Kristo alifundisha na akasulubiwa
- Nefi
-
mji ambao Nefi na watu wake walijenga baada ya kuwaacha Lamani na Lamueli na wafuasi wao
- nchi ya ahadi
-
nchi yoyote ambapo Mungu anawaongoza wateule wake kwayo. Aliwaongoza familia ya Lehi na Wayaredi kwenye nchi ya ahadi.
- Sidomu
-
nchi ambapo Alma Mdogo alianzisha Kanisa. Ilikuja ikawa nyumba mpya kwa watu wenye haki walioondoka Amoniha.
- Maji ya Mormoni
-
mahali ambapo Alma aliwabatiza Wanefi waongofu waliokuwa wamemwacha Mfalme Nuhu
- Zarahemla
-
mji mkuu wa Wanefi ambao ulikuwa kituo cha serikali na Kanisa. Mfalme Mosia na Mfalme Benyamini waliishi hapa. Mji huo ulichomwa wakati wa kifo cha Yesu.