Scripture Stories
Sura ya 1: Jinsi Tulivyopata Kitabu cha Mormoni


Sura ya 1

Jinsi Tulivyopata Kitabu cha Mormoni

Picha
Joseph akitazama kanisa

Wakati Joseph alipokuwa na umri wa miaka 14, makanisa mengi yalidai kuwa ya kweli, na hakujua ni lipi angejiunga nalo.

Picha
Joseph akisoma Biblia

Siku moja Joseph alisoma Yakobo 1:5 katika Biblia: “Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu.” Joseph alitaka kujua ni kanisa gani lilikuwa la kweli, kwa hiyo aliamua kumuuliza Mungu.

Picha
Joseph katika msitu

Asubuhi moja ya majira ya kuchipua, Joseph alikwenda msituni karibu na nyumbani kwake kusali.

Picha
Joseph akisali

Wakati Joseph alipopiga magoti na kuanza kusali, Shetani alijaribu kumzuia. Joseph alisali kwa nguvu zaidi, akimwomba Baba wa Mbinguni msaada.

Picha
Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo walimjia Joseph Smith katika nguzo ya mwanga. Baba wa Mbinguni alimwonyesha Yesu na akasema: “Huyu ni Mwanangu Mpendwa. Msikilize Yeye!”

Picha
Yesu

Joseph aliuliza ni kanisa gani angejiunga nalo. Yesu alimwambia asijiunge na kanisa lolote kwani yote yalikuwa si sahihi.

Picha
watu wakimcheka Joseph

Wakati Joseph alipowaambia baadhi ya watu kile alichokuwa ameona na kusikia, walimcheka. Viongozi wengi wa makanisa yaliyokuwa katika eneo lake walimtesa.

Picha
Joseph akisali

Miaka mitatu ilipita. Usiku mmoja Joseph alikuwa akisali kwa ajili ya msamaha wa dhambi zake na kwa ajili ya kujua kile alichohitajika kukifanya.

Picha
Moroni akimtokea Joseph

Malaika kwa jina Moroni alimtokea na kumwambia Joseph kuhusu kitabu ambacho kilikuwa kimeandikwa kwenye bamba za dhahabu. Joseph alitakiwa kuzitafsiri bamba hizi kwa Kiingereza.

Picha
Joseph kitandani

Wakati Moroni alipoondoka, Joseph aliwaza kuhusu kile ambacho Moroni alikuwa amemwambia yeye. Moroni alirudi tena mara mbili zaidi usiku huo.

Picha
Joseph akiinua jiwe

Siku iliyofuata Joseph alikwenda kileleni mwa Mlima Kumorah, aliokuwa ameuona katika ono. Hapo alikuta jiwe kubwa. Aliinua jiwe lile kwa kutumia fimbo.

Picha
Joseph akitazama bamba za dhahabu

Chini ya jiwe lile kulikuwa na sanduku lililoundwa kwa mawe. Joseph alipokuwa akitazama ndani ya sanduku, aliziona bamba za dhahabu.

Picha
Moroni akimtokea Joseph

Moroni alimtokea na kumwambia Joseph asichukue zile bamba ila arudi tena siku kama hiyo kila mwaka kwa miaka minne. Kila wakati Joseph alipokwenda, Moroni alimfunza.

Picha
Moroni akimtokea Joseph

Baada ya miaka minne Joseph hatimaye aliruhusiwa kuchukua bamba zile. Alitumia Urimu na Thumimu kutafsiri baadhi ya bamba hizo.

Picha
Joseph pamoja na mwandishi

Waandishi walimsaidia Joseph kwa kuandika maneno wakati alipokuwa akiyatafsiri kutoka kwenye bamba za dhahabu.

Picha
Joseph na mpiga chapa

Joseph aliyapeleka maneno yaliyokuwa yametafsiriwa kwa mpiga chapa na kuyatengeneza kuwa kitabu.

Historia ya Kanisa 1:71

Picha
Kitabu cha Mormoni

Kitabu hicho kinaitwa Kitabu cha Mormoni. Kinasimulia kuhusu watu walioishi Marekani miaka mingi iliyopita. Pia kinasimulia kuhusu Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

Chapisha