Scripture Stories
Sura ya 35: Kapteni Moroni na Pahorani


Sura ya 35

Kapteni Moroni na Pahorani

Picha
Moroni akisoma karatasi

Kapteni Moroni alifurahi kusikia kwamba Helamani na jeshi lake waliweza kutwaa tena sehemu kubwa ya ardhi ya Wanefi kutoka kwa Walamani.

Picha
Wapiganaji wamesimama ukutani

Lakini Helamani na jeshi lake walihitaji msaada. Hawakuwa na wanajeshi wa kutosha kulinda miji mingi.

Picha
Kapteni Moroni akiandika

Kapteni Moroni aliandika barua kwa Pahorani mwamuzi mkuu na gavana. Alimuomba Pahorani atume wanajeshi zaidi kulisaidia jeshi la Helamani.

Picha
Walamani wakiuvamia mji

Walamani waliuvamia mji wa Wanefi ambao Helamani alikuwa ameuchukua. Waliwauwa wengi wa Wanefi na kuwafukuza waliobaki kutoka kwenye mji.

Picha
Moroni akiandika

Akiwa ameukasirikia uongozi wa serikali kwa sababu hawakutuma msaada, Moroni aliandika barua nyingine kwa Pahorani.

Picha
wanajeshi

Kapteni Moroni aliandika kwamba watu wengi walikuwa wameuwawa kwa sababu Pahorani hakutuma wanajeshi zaidi.

Picha
Moroni akiandika

Kwa vile Pahorani hakutuma haraka watu zaidi na chakula, Moroni angechukua jeshi lake mpaka Zarahemla na kuchukua kile jeshi lake lilichokihitaji.

Picha
Moroni akipokea barua

Punde Moroni alipokea barua kutoka kwa Pahorani. Alikuwa na huzuni kwamba Moroni na jeshi lake walikuwa wakiteseka.

Picha
Pahorani akiandika barua

Pahorani alimwambia Moroni kwamba kundi la Wanefi waovu walioitwa watu wa mfalme hawakumtaka yeye kuwa mwamuzi mkuu. Walikuwa wamemlazimisha yeye na wale waliomuunga mkono kutoka nje ya Zarahemla.

Picha
Jeshi likijikusanya nje ya mji

Pahorani aliongeza kwamba alikuwa akikusanya jeshi kujaribu kuuchukua tena mji wa Zarahemla.

Picha
Mfalme na watu wake

Watu wa mfalme walikuwa wamemchagua mfalme kuwa kiongozi wao na walikuwa wameungana na Walamani.

Picha
Pahorani akiandika barua

Pahorani hakuwa na hasira juu ya kile Moroni alichokuwa amekiandika. Alitaka Wanefi kuwa huru pia.

Picha
Moroni akisoma barua

Alimuomba Moroni kuleta watu wachache kumsaidia na akasema kama Moroni angekusanya watu zaidi njiani, jeshi lililoungana lingeweza kuuchukua tena mji wa Zarahemla.

Picha
Moroni akishika barua

Kapteni Moroni alikuwa na furaha kwamba Pahorani bado alikuwa mwaminifu kwa nchi yake na bado alitaka uhuru kwa ajili ya watu.

Picha
Moroni na wanajeshi

Akiwa na watu wachache, Moroni alikwenda kukutana na Pahorani. Alibeba bendera ndogo ya uhuru, na maelfu ya wanaume waliungana nao njiani.

Picha
Vita katika ukuta wa mji

Jeshi la muungano la Moroni na Pahorani lilisonga kuelekea Zarahemla. Walimuua mfalme wa Wanefi waovu na kuwateka watu wake.

Picha
Moroni na wanajeshi

Kisha Moroni alituma chakula na wanajeshi 12,000 kusaidia majeshi ya Wanefi. Majeshi haya yaliwafukuza Walamani, na kulikuwa na amani tena katika nchi.

Chapisha