Scripture Stories
Sura ya 39: Nefi Anapokea Nguvu Kuu


Sura ya 39

Nefi Anapokea Nguvu Kuu

Picha
Nefi akitafakari

Nefi alitembea kuelekea nyumbani kwake, akitafakari kuhusu kile Bwana alichomwonyesha na kuhusu uovu wa Wanefi. Alihuzunika kwa sababu ya uovu wao.

Picha
Nefi akisali

Bwana alizungumza na Nefi na kumsifia kwa kuwa mtiifu na kwa kufanya kazi kwa bidii kufundisha injili.

Picha
Nefi

Nefi alipewa nguvu za kufanya chochote. Bwana alijua angetumia nguvu hii kwa haki.

Picha
Nefi akitembea

Bwana alimwambia Nefi kuwaonya Wanefi kwamba kama hawangetubu, wangeangamizwa. Nefi alikwenda mara moja kuwaonya watu.

Picha
Wanefi wakimshambulia Nefi

Wanefi hawakumwamini Nefi. Walijaribu kumtupa gerezani, lakini nguvu za Mungu zilimlinda.

Picha
Nefi akiondoka

Nefi alitangaza neno la Mungu kwa Wanefi wote.

Picha
Watu wakipigana

Lakini watu walizidi kuwa waovu zaidi na kuanza kupigana wao kwa wao.

Picha
Nefi akisali

Nefi alisali kwa ajili ya njaa, akiamini kwamba ukosefu wa chakula ungewanyenyekeza Wanefi na kuwasaidia kutubu.

Picha
Watu kwenye ardhi kavu

Baa la njaa lilikuja. Hakukuwa na mvua, kwa hivyo ardhi ilikauka na mazao hayakukua. Watu waliacha kupigana.

Picha
familia ikisali

Wanefi walikuwa na njaa, na wengi wao walikufa. Wale waliobaki walianza kumkumbuka Bwana na kile ambacho Nefi aliwafundisha.

Picha
Watu wakiongea na waamuzi

Watu walitubu dhambi zao na kisha waliwaomba waamuzi wao kumuomba Nefi asitishe baa la njaa. Waamuzi wakienda kwa Nefi

Picha
Nefi akisali

Wakati Nefi alipowaona watu kwamba walikuwa wanyenyekevu na wametubu, alimuomba Bwana kumaliza baa la njaa.

Picha
Watu katika mvua

Bwana alijibu sala ya Nefi, na mvua ilianza kunyesha. Punde mazao yalianza kukua tena. Watu walimshukuru Mungu na kujua kwamba Nefi alikuwa ni nabii.

Picha
Nefi akifanya kazi

Wengi wa Wanefi walijiunga na Kanisa. Walikuwa matajiri, na miji yao ikakua. Kulikuwa na amani katika nchi.

Picha
Walamani wakiwavamia Wanefi

Kisha baadhi ya Wanefi ambao hapo awali walijiunga na Walamani waliwavamia Wanefi.

Picha
Wapiganaji

Wanefi walijaribu kuwashinda maadui wao, ambao walikuwa Wanyang’anyi wa Gadiantoni, lakini hawakuweza kwa sababu wao wenyewe walikuwa waovu tena.

Picha
Wanefi wakibeba vikapu

Wakati wanefi walipokuwa wema, Bwana aliwabariki. Walipokuwa na kiburi na kumsahau Bwana, aliwapa matatizo ili kuwasaidia kumkumbuka.

Chapisha