Sura ya 44
Yesu Kristo Anawabariki Watoto
Picha
Kristo na watoto
Yesu Kristo aliwaambia Wanefi wawalete watoto wao kwake. Watoto waliketi chini karibu na Yesu.
Picha
Yesu akisali pamoja na watoto
Mwokozi aliwaambia watu wapige magoti. Kisha akapiga magoti na kumwomba Baba wa Mbinguni.
Picha
watu wakitabasamu
Sala ya Mwokozi ilikuwa ya ajabu kiasi kwamba haikuweza kuandikwa. Iliwajaza Wanefi na shangwe.
Picha
Yesu akizungumza na watu
Baada ya sala yake Yesu alisema kwamba Wanefi wangebarikiwa kwa sababu ya imani yao.
Picha
Yesu
Alihisi upendo na furaha nyingi hadi akalia.
Picha
Yesu anawabariki watoto
Kisha akawachukua watoto na kuwabariki kila mmoja. Aliomba kwa Baba wa Mbinguni kwa ajili yao na akalia tena.
Picha
Yesu pamoja na watoto
Yesu aliwaambia Wanefi wawatazame watoto wao.
Picha
malaika wakiwa wamewazingira watoto
Watu wakiwa wanatazama, malaika walishuka kutoka mbinguni na kuwazingira watoto. Watoto na malaika walikuwa wamezingirwa na moto.