Scripture Stories
Sura ya 19: Wana wa Mosia Wanakuwa Wamisionari


Sura ya 19

Wana wa Mosia Wanakuwa Wamisionari

Picha
wana wanne wa Mosia

Mosia alikuwa na wana wanne: Amoni, Haruni, Omneri, na Himni. Walikuwa pamoja na Alma Mdogo wakati malaika alipomtokea.

Picha
wana wa Mosia

Wana wa Mosia walikuwa wametubu dhambi zao na walihuzunika kwa ajili ya taabu waliyokuwa wamesababisha. Walijua injili ilikuwa ya kweli, na walitaka kuwafundisha wengine.

Picha
wana wa Mosia wakizungumza

Kila mmoja wa wana wa Mosia alikataa kuwa mfalme. Badala yake, walitaka kuhudumu kama wamisionari kwa Walamani na kushiriki nao baraka za injili.

Picha
Mfalme Mosia akisali

Mfalme Mosia alisali aweze kujua ikiwa alipaswa kuwaruhusu wana wake waende. Mungu alimwambia awaruhusu waende, na wangelindwa. Walamani wengi wangeamini ujumbe wao.

Picha
wana wanne wanasali

Wana wa Mosia walienda kuwafundisha Walamani. Walifunga na kusali ili wawe wamisionari wazuri.

Chapisha