Sura ya 41
Ishara za kuzaliwa kwa Kristo
Nefi, mwana wa Helamani, alimpa kumbukumbu takatifu na maandiko mwanawe mkubwa, Nefi
Wanefi waliona ishara kuu na maajabu ambayo manabii walikuwa wamesema yangetokea kabla ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Lakini baadhi ya Wanefi walisema wakati wa Yesu kuzaliwa tayari ulikuwa umepita. Waliwadhihaki wale walioendelea kuuamini unabii wa Samweli Mlamani.
Watu walioamini katika Yesu Kristo na manabii walihuzunika na kudhani kwamba kitu fulani kingeuzuia unabii usitimie.
Watu waliutazamia kwa uaminifu usiku ambao hauna giza, ambao ulikuwa ni ishara kwamba Yesu Kristo angezaliwa.
Wale ambao hawakuamini katika Yesu Kristo walichagua siku ya kuwauwa walioamini kama ishara isingeonekana.
Nefi alihuzunika kwa sababu ya uovu wa wale ambao hawakuamini katika Mwokozi.
Nefi alisali siku nzima kwa ajili ya watu ambao wangeuwawa.
Bwana alimfariji Nefi na kumwambia kwamba usiku huo usingekuwa na giza. Yesu angezaliwa siku iliyofuata huko Bethlehemu.
Usiku huo jua lilitua, lakini hakukuwa na giza. Ishara ya kuzaliwa kwa Kristo ilionekana. Watu walishangazwa.
Wale waliokuwa wamepanga kuwauwa waaminio walianguka ardhini na kuonekana kama wafu.
Waliogopa kwa sababu walikuwa waovu. Sasa walijua kwamba Mwokozi angezaliwa na kwamba manabii walikuwa sahihi.
Kulikuwa na mwanga usiku mzima. Jua lilipotoka asubuhi iliyofuata, watu walijua kwamba Yesu Kristo angezaliwa siku hiyo. Unabii ulikuwa umetimia.
Nyota mpya ilitokea kwenye anga, kama vile manabii walivyosema ingetokea.
Shetani bado aliwafanya watu kutoamini ishara ambayo waliiona, lakini wengi waliamini.
Nefi na viongozi wengine wa Kanisa waliwabatiza wote ambao waliamini na kutubu.
Kulikuwa na habari njema katika nchi kwa sababu maneno ya manabii yalikuwa yametimizwa. Yesu Kristo alikuwa amezaliwa.