Scripture Stories
Sura ya 41: Ishara za kuzaliwa kwa Kristo


Sura ya 41

Ishara za kuzaliwa kwa Kristo

Picha
Nefi akimpa kumbukumbu mwanawe

Nefi, mwana wa Helamani, alimpa kumbukumbu takatifu na maandiko mwanawe mkubwa, Nefi

Picha
Watu wakizungumza

Wanefi waliona ishara kuu na maajabu ambayo manabii walikuwa wamesema yangetokea kabla ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo.

Picha
Watu wakitabasamu

Lakini baadhi ya Wanefi walisema wakati wa Yesu kuzaliwa tayari ulikuwa umepita. Waliwadhihaki wale walioendelea kuuamini unabii wa Samweli Mlamani.

Picha
Watu wakimsikiliza mtu mzee

Watu walioamini katika Yesu Kristo na manabii walihuzunika na kudhani kwamba kitu fulani kingeuzuia unabii usitimie.

Picha
Familia ikitazama juu

Watu waliutazamia kwa uaminifu usiku ambao hauna giza, ambao ulikuwa ni ishara kwamba Yesu Kristo angezaliwa.

Picha
Watu wakipanga njama

Wale ambao hawakuamini katika Yesu Kristo walichagua siku ya kuwauwa walioamini kama ishara isingeonekana.

Picha
Nefi

Nefi alihuzunika kwa sababu ya uovu wa wale ambao hawakuamini katika Mwokozi.

Picha
Nefi akisali

Nefi alisali siku nzima kwa ajili ya watu ambao wangeuwawa.

Picha
Nefi

Bwana alimfariji Nefi na kumwambia kwamba usiku huo usingekuwa na giza. Yesu angezaliwa siku iliyofuata huko Bethlehemu.

Picha
Familia ikitazama machweo

Usiku huo jua lilitua, lakini hakukuwa na giza. Ishara ya kuzaliwa kwa Kristo ilionekana. Watu walishangazwa.

Picha
Watu waovu wakiwa ardhini

Wale waliokuwa wamepanga kuwauwa waaminio walianguka ardhini na kuonekana kama wafu.

Picha
watu wawili

Waliogopa kwa sababu walikuwa waovu. Sasa walijua kwamba Mwokozi angezaliwa na kwamba manabii walikuwa sahihi.

Picha
Wapiganaji vitani

Kulikuwa na mwanga usiku mzima. Jua lilipotoka asubuhi iliyofuata, watu walijua kwamba Yesu Kristo angezaliwa siku hiyo. Unabii ulikuwa umetimia.

Picha
Watu wakiona nyota mpya

Nyota mpya ilitokea kwenye anga, kama vile manabii walivyosema ingetokea.

Picha
Mwanamke na mwanaume wakitazama juu

Shetani bado aliwafanya watu kutoamini ishara ambayo waliiona, lakini wengi waliamini.

Picha
Nefi akimbatiza mtu

Nefi na viongozi wengine wa Kanisa waliwabatiza wote ambao waliamini na kutubu.

Picha
watu katika mji

Kulikuwa na habari njema katika nchi kwa sababu maneno ya manabii yalikuwa yametimizwa. Yesu Kristo alikuwa amezaliwa.

Chapisha