Scripture Stories
Maneno ya Kujua


Maneno ya Kujua

A

madhabahu

Sehemu takatifu, eneo lililonyanyuliwa kwa mchanga au miamba ambapo sala au sadaka hutolewa kwa Mungu

Picha
madhabahu

madhabahu

malaika

mjumbe kutoka kwa Mungu

Vazi la kivita

Vazi ambalo wanajeshi huvaa kujilinda wao wenyewe katika vita.

Picha
Vazi la kivita

Vazi la kivita

jeshi

Kundi la wanajeshi wakijiandaa kupigana

mshale

Silaha yenye ncha iliyochongoka itumikayo kuwindia au vitani

Picha
mshale

mshale

B

ubatizo

Ibada ambapo mtu mwenye mamlaka kutoka kwa Mungu humzamisha mtu mwingine majini kabisa na kumnyanyua mtu huyo tena kutoka majini. Ubatizo unahitajika ili kuwa muumini wa Kanisa la Yesu Kristo.

Picha
ubatizo

ubatizo

mashua

Boti kubwa iliyotumika kubeba watu au vitu

Picha
mashua

mashua

amini

Kuhisi au kujua kwamba kitu fulani ni kweli

bariki

Kumpa mtu kitu ambacho kitamsaidia. Kubariki sakramenti ni kumuomba Mungu kukubali mkate na maji kama ishara ya Yesu Kristo.

kipofu

kutoweza kuona

utumwa

kutokuwa huru, na kutakiwa kufanya kazi siku nzima kwa manufaa ya mtu fulani

upinde

Fimbo ndefu yenye kamba iliyofungwa katika kila ncha yake ambayo hutumika kurusha mishale

Picha
upinde

upinde

bamba za shaba

Kumbukumbu ya amri za Mungu na matendo yake kwa mababu wa Lehi

Picha
bamba za shaba

bamba za shaba

jenga

kutengeneza au kuunda kitu

C

kapteni

Kiongozi wa jeshi

rungu

Zana iliyotumika kupigia wanyama au watu

Picha
rungu

rungu

amri

kitu ambacho Mungu huwaambia watu Wake kufanya ili waje kuwa na furaha

agano

ahadi takatifu kati ya Mungu na watu

sulubisha

Kumuua mtu kwa kumpigilia kwa misumari msalabani

D

kiziwi

kutoweza kusikia

angamiza

Kuharibu au kumaliza kitu kabisa, kama vile mji au maisha

mwanafunzi

mtu anayemfuata Yesu na kujaribu kuwa kama Yeye.

ndoto

hadithi ambayo huwa katika mawazo ya mtu wakati amelala

kulewa

Ukosefu wa kujidhibiti kutokana na kunywa pombe sana

E

toroka

Kwenda mbali na mtu

uzima wa milele

Kuishi milele na Mungu

uovu

Kitu ambacho ni kibaya

F

imani

kuamini katika Yesu Kristo

uaminifu

Kuendelea kutii amri

baa la njaa

Ukosefu wa chakula usababishwao na kukosekana kwa mvua na kushindwa kuota kwa mazao

kufunga

Kutokula wala kunywa wakati ukitafuta msaada wa kiroho

kujazwa na Roho Mtakatifu

Kuwa na Roho Mtakatifu kuweka ukweli kwenye mawazo na akili za mtu

kusamehe

Kusahau vitu vibaya ambavyo mtu amevifanya na kumpenda mtu

uhuru

Kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi

G

habari njema

Jumbe za matumaini na faraja kutoka kwa Mungu

bamba ya dhahabu

Kumbukumbu iliyoandikwa kwenye bati nyembamba za dhahabu. Moroni alizificha bamba hizi katika Mlima Kumora, na Joseph Smith baadaye alizifukua.

Picha
bamba ya dhahabu

bamba ya dhahabu

injili

mafundisho ya Yesu Kristo

Roho Mkuu

Jina la Mungu kutoka kwa Walamani

H

ponya

kufanya mtu aliye mgonjwa ama aliye umia kuwa mzima

mbinguni

mahali ambapo Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanaishi

unyenyekevu

Kuwa wa kufundishika na wa kutafuta kutenda mapenzi ya Mungu

I

sanamu

Kitu ambacho watu hukiabudu ambacho si Mungu

fimbo ya chuma

Alama katika ndoto ya Lehi ambayo huwakilisha neno la Mungu

J

jiunge

kuwa sehemu ya kikundi

mwamuzi

Kiongozi ambaye huamua nini sheria humaanisha au jinsi watu wanavyotakiwa kuzishika

Kiti cha hukumu

Wadhifa katika serikali ya Wanefi ambayo mwamuzi mkuu alikwa nao

K

Mfalme

Kiongozi juu ya kikundi cha watu

L

kiongozi

Mtu ambaye huongoza kikundi cha watu

Liahona

Chombo cha mviringo cha shaba Mungu alichowapa familia ya Lehi kuwaonyesha njia ya kuelekea nyikani. Kilifanya kazi pale tu familia ya Lehi ilipokuwa yenye haki.

Picha
Liahona

Liahona

uhuru

Uhuru wa kufanya uchaguzi

M

mshiriki

mtu ambaye yuko katika kanisa ama kikundi

muujiza

Tukio lisilo la kawaida au tukio linaloonyesha uwepo wa nguvu za Mungu

mmisionari

Mtu ambaye anafundisha injili ya Yesu Kristo

O

tii

kufanya kile ambacho kinatakiwa au kimeamriwa.

tawaza

Kutoa nguvu ya ukuhani na mamlaka

Picha
tawaza

tawaza

ibada

Utaratibu mtakatifu au kitendo ambacho kina maana ya kiroho, kama vile ubatizo au sakramenti

P

amani

Hisia tulivu au wakati ambapo hakuna vita

tesa

Kusema vitu vya uwongo juu ya mtu fulani na kujaribu kuwaumiza

bamba

Vipande vyembamba vya metali ambavyo watu walitumia kuandikia mafundisho ya Mungu na historia za watu

Picha
bamba

bamba

Kula njama

Kuweka mpango mwovu dhidi ya mtu fulani

nguvu

Nguvu ya wema au uovu, mara nyingi msaada maalum au nguvu kutoka kwa Mungu

sali

kuzungumza na Mungu, kumpa shukrani na kumuomba baraka

ukuhani

mamlaka ya kutenda katika jina la Mungu

gereza

Sehemu iliyotumika kuwaweka watu ambao wametenda makosa.

ahadi

Nadhiri au utayari wa kutenda kitu au kuwa mtu fulani

unabii

Kuelezea tukio kabla halijatokea

nabii

Mtu aliyeitwa na Mungu kuwaambia watu mapenzi ya Mungu

adhibu

Kusababisha au kuruhusu vitu vibaya kutokea kwa mtu fulani. Watu mara nyingi wanaadhibiwa wakati hawamtii Mungu.

R

Mwasi

Kutotii au kwenda kinyume na amri

tubu

Kuhisi huzuni kutokana na tendo au wazo na kuahidi kutolirudia

fufuka

Kumrudishia mtu au kitu uhai

haki

Kitu ambacho ni cha Mungu Watu wenye haki ni wale ambao wanafuata amri za Mungu.

joho

Nguo ndefu ya ifunikayo mwili mzima

S

sakramenti

Ibada ambapo wanaume ambao wana ukuhani hubariki na kupitisha mkate na maji kwa watu wengine. Sakramenti huwakumbusha watu kuhusu Yesu Kristo.

dhabihu

Kuacha kitu cha thamani kwa ajili ya Mungu

Ondoa ngozi ya juu ya kichwa

Kukata ngozi ya juu ya kichwa cha mtu fulani

mtumishi

Watu ambao hutumikia au kufanya kazi kwa mtu fulani kama vile mfalme

Ngao

Sehemu ya vazi la kivita ambayo hulinda sehemu ya juu ya mwili wa askari dhidi ya upanga na silaha zingine

dhambi

Kuvunja amri

watumwa

Watu ambao wanalazimishwa kufanya kazi kwa ajili ya watu wengine

kombeo

Silaha itumikayo katika kurusha mawe

Picha
kombeo

kombeo

askari

Mtu ambaye anapigana katika jeshi

mkuki

Fimbo ndefu, yenye ncha kali itumikayo kuchomea

Picha
mkuki

mkuki

iba

kuchukua kitu ambacho ni cha mtu mwingine

Piga kwa jiwe

Kurusha vipande vya miamba kwa mtu mpaka anapofariki

upanga

Kipande kirefu cha metali, chenye makali kitumikacho kukata au kuchana

Picha
upanga

upanga

sinagogi

Aina ya jengo ambapo watu hukusanyika kumwabudu Mungu

T

hekalu

nyumba ya Mungu.

Picha
hekalu

hekalu

ushuhuda

Hisia au ushahidi kwamba injili ni ya kweli

Bendera ya uhuru

Ujumbe ambao kapteni Moroni aliuandika kuwahamasisha watu wake kuulinda uhuru wao

Picha
Bendera ya uhuru

Bendera ya uhuru

mnara

Jengo refu au jukwaa refu ambapo watu wanaweza kusimama

Picha
mnara

mnara

tafsiri

Kubadilisha maneno kutoka lugha moja kwenda nyingine

Mti wa uzima

Mti katika ndoto ya Lehi ambao unawakilisha upendo wa Mungu

kweli

Kitu fulani ambacho kweli kilitokea au ambacho ni kizuri au sahihi

U

Fahamu

Kujua au kuelewa wazo fulani

Urimu na thumimu

Nyenzo maalum ambazo Mungu huwapa manabii kuwasaidia wao kutafsiri na kupokea ufunuo

V

thabiti

Kujua na kulinda kilicho cha kweli

ono

Aina ya ufunuo

W

vita

Mapigano kati ya maadui au majeshi yanayopingana

silaha

Kitu fulani knachotumika kudhuru au kuua watu wengine kama vile upanga au mkuki

uovu

Kitu ambacho si cha Kiungu Mtu mwovu humpenda Shetani na hatii amri za Mungu.

nyika

Sehemu wazi kubwa ya nchi ambayo haina miji au watu

abudu

Kupenda au kumfuata mtu au kitu

Chapisha