Scripture Stories
Sura ya 53: Moroni na Mafundisho Yake


Sura ya 53

Moroni na Mafundisho Yake

Picha
Moroni akiandika kwenye bamba

Baada ya Mormoni kufariki, Moroni alibaki peke yake. Alimalizia kumbukumbu ambazo baba yake alikuwa amempa yeye.

Picha
Moroni akimwona Joseph Smith

Moroni alijua bamba za dhahabu siku moja zingetolewa kutoka kwenye ardhi.

Picha
wenza wakiwa na Kitabu cha Mormoni

Maneno yaliyoko kwenye bamba za dhahabu yanashuhudia kuhusu Yesu Kristo. Yanatoa ushuhuda na kufundisha watu jinsi ya kuishi kwa haki.

Picha
Walamani wakiwateka Wanefi

Walamani waovu walimuua kila Mnefi ambaye alikataa kumkana Yesu Kristo.

Picha
Moroni akijificha kutoka kwa Walamani

Moroni kamwe asingemkana Yesu Kristo. Alihama hama, akijificha kutoka kwa Walamani.

Picha
Moroni akiandika kwenye bamba za dhahabu

Moroni aliandika mengi zaidi kwenye bamba za dhahabu, hasa kwa Walamani wa siku za Mwisho.

Picha
wavulana wakibariki sakramenti

Aliandika vitu vingi muhimu, ikijumuisha maneno ya sala za sakramenti.

Picha
mwanaume akibatizwa

Moroni aliandika kwamba wanaoweza kubatizwa ni wale tu walio radhi kutubu dhambia zao na kumtumikia Yesu Kristo.

Picha
Yesu Kristo

Moroni alitaka kila mtu amwamini Yesu Kristo na waweze kumfahamu. Alisema kila kilicho kizuri kinatoka kwa Kristo.

Picha
Moroni akiandika kwenye bamba

Moroni aliandika kwamba kama watu watampenda Mungu na kumfuata, wanaweza kuwa wakamilifu.

Picha
Moroni

Moroni alijua kwamba baada ya kufariki angefufuliwa na angeishi na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Chapisha