Sura ya 53
Moroni na Mafundisho Yake
Baada ya Mormoni kufariki, Moroni alibaki peke yake. Alimalizia kumbukumbu ambazo baba yake alikuwa amempa yeye.
Moroni alijua bamba za dhahabu siku moja zingetolewa kutoka kwenye ardhi.
Maneno yaliyoko kwenye bamba za dhahabu yanashuhudia kuhusu Yesu Kristo. Yanatoa ushuhuda na kufundisha watu jinsi ya kuishi kwa haki.
Walamani waovu walimuua kila Mnefi ambaye alikataa kumkana Yesu Kristo.
Moroni kamwe asingemkana Yesu Kristo. Alihama hama, akijificha kutoka kwa Walamani.
Moroni aliandika mengi zaidi kwenye bamba za dhahabu, hasa kwa Walamani wa siku za Mwisho.
Aliandika vitu vingi muhimu, ikijumuisha maneno ya sala za sakramenti.
Moroni aliandika kwamba wanaoweza kubatizwa ni wale tu walio radhi kutubu dhambia zao na kumtumikia Yesu Kristo.
Moroni alitaka kila mtu amwamini Yesu Kristo na waweze kumfahamu. Alisema kila kilicho kizuri kinatoka kwa Kristo.
Moroni aliandika kwamba kama watu watampenda Mungu na kumfuata, wanaweza kuwa wakamilifu.
Moroni alijua kwamba baada ya kufariki angefufuliwa na angeishi na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.