Scripture Stories
Sura ya 27: Korihori


Sura ya 27

Korihori

Picha
Korihori akitembea

Mtu mmoja aliyeitwa Korihori alikuja Zarahemla. Hakuwa na imani katika Yesu Kristo na alihubiri kwamba kile ambacho manabii walisema kuhusu Mwokozi kilikuwa si kweli.

Picha
Korihori akiwafundisha watu

Korihori aliwaambia watu walikuwa wapumbavu kuamini kwamba Yesu angekuja duniani na kuteseka kwa ajili ya dhambi zao.

Picha
wavulana wakitenda dhambi

Alisema watu hawawezi kuadhibiwa kwa ajili ya dhambi zao kwa sababu hakuna maisha baada ya kifo. Watu wengi walimwamini Korihori. Wakageuka kuwa waovu.

Picha
Korihori

Korihori alijaribu kuwahubiria watu wa Amoni, lakini hawakumsikiliza. Walimfunga na kumpeleka kwa Amoni, ambaye alimlazimisha kuondoka mjini.

Picha
Korihori akifukuzwa

Korihori alienda katika nchi ya Gideoni, lakini watu waliokuwa huko pia walikataa kumsikiliza. Mwamuzi mkuu alimpeleka kwa Alma.

Picha
Alma na Korihori

Alma alimuuliza Korihori kama aliamini katika Mungu. Korihori alisema la. Alma alishuhudia ya kwamba kuna Mungu na kwamba Kristo angekuja.

Picha
Korihori na Amoni

Korihori alimtaka Alma atende muujiza ili athibitishe kwamba kuna Mungu. Korihori alisema angesadikishwa kwamba kuna Mungu ikiwa angeona ishara ya uwezo wa Mungu.

Picha
Alma akiwa ameshika maandiko

Alma alimwambia Korihori kwamba alikuwa amekwisha kuziona ishara nyingi za uwezo wa Mungu kupitia maandiko na shuhuda za manabii wote.

Picha
Alma akizungumza na Korihori

Alma alisema kwamba dunia na vitu vyote vilivyo juu yake na mwendo wa sayari zilizo mbinguni pia ni ishara kwamba kuna Mungu.

Picha
Korihori na Alma

Korihori bado alikataa kuamini. Alma alikuwa na huzuni kwa sababu ya uovu wa Korihori na akamuonya kwamba nafsi yake ingeweza kuangamizwa.

Picha
Alma akiwa ameshika maandiko

Korihori bado alitaka ishara kuthibitisha kwamba kuna Mungu. Alma alisema ishara kutoka kwa Mungu ingekuwa kwamba Korihori hangeweza kusema.

Picha
Korihori

Baada ya Alma kusema haya, Korihori hakuweza kuzungumza.

Picha
Korihori anaandika kwenye mchanga

Korihori aliandika kwamba alijua hii ilikuwa ishara kutoka kwa Mungu na kwamba daima alikuwa anajua kuna Mungu. Alimuomba Alma asali na kuiondoa ile laana.

Picha
Alma akizungumza

Alma alijua ya kwama kama Korihori angeweza kusema tena angewadanganya watu tena. Alma alisema kwamba Bwana angeamua kama Korihori angezungumza tena.

Picha
Korihori akiomba chakula

Bwana hakumrudishia Korihori uwezo wake wa kusema. Korihori alikwenda nyumba hadi nyumba, akiomba chakula.

Picha
mwamuzi mkuu akiandika barua

Mwamuzi mkuu alituma barua kote nchini ikisema kilichompata Korihori. Aliwaambia wale ambao walikuwa wamemwamini Korihori watubu. Watu walitubu.

Picha
Korihori kwenye ardhi akiwa amefariki

Korihori alienda kuishi na Wazoramu. Siku moja alipokuwa akiombaomba, alikanyagwa hadi kufa.

Chapisha