Scripture Stories
Utangulizi


Utangulizi

Kwa Msomaji

Hadithi hizi za Kitabu cha Mormoni zimeandikwa mahsusi kwa ajili yako. Hadithi zimetolewa kutoka kwenye kitabu ambacho ni kitakatifu kwa sababu kilitoka kwa Baba wa Mbinguni. Unaposoma hadithi hizi, kumbuka kuwa zinawahusu watu wa kweli ambao waliishi Amerika hapo zamani za kale.

Baada ya kusoma hadithi katika kitabu hiki, pia utataka kuzisoma kutoka kwenye Kitabu cha Mormoni. Chini ya kila picha utaona wapi unaweza kupata hiyo hadithi katika Kitabu cha Mormoni. Muombe baba yako, mama, mwalimu, au rafiki wakusaidie.

Kama haujui nini maana ya neno, litafute katika sehemu ya “Maneno ya Kujua” mwishoni mwa kitabu hiki. Habari kuhusu watu na sehemu zilizotajwa katika Kitabu cha Mormoni pia vimejumuishwa mwishoni mwa kitabu.

Kwa Wazazi na Walimu

Kitabu hiki kitawasaidia kufundisha maandiko. Shiriki ushuhuda wako wa Kitabu cha Mormoni, na uwatie moyo wale unaowafundisha kutafuta shuhuda zao wenyewe. Uelewa wao utakua unapowasomea maandishi kamili ya hadithi wanazozienzi kutoka kwenye Kitabu cha Mormoni chenyewe.

Chapisha