Sura ya 46
Yesu Kristo Anawafundisha na Kusali pamoja na Wanefi
Wanefi ambao walimuona Yesu Kristo waliwaambia rafiki zao angekuja tena siku iliyofuata. Watu wengi walifanya kazi sana kufika pale ambapo Yesu angekuwepo.
Asubuhi iliyofuata Nefi na wanafunzi wengine walilifundisha kundi ambalo lilikuwa limekusanyika. Wanafunzi kisha walisali kwamba wangeweza kupokea Roho Mtakatifu.
Nefi alikwenda majini na akabatizwa. Kisha aliwabatiza wanafunzi wengine.
Baada ya kuwa wamebatizwa, wanafunzi walipokea Roho Mtakatifu. Moto ulionekana kuwazunguka, na malaika walishuka kutoka mbinguni na kuwahudumia.
Wakati malaika wakiwa na wanafunzi, Yesu alikuja na kusimama miongoni mwao.
Kristo aliwaambia Wanefi wote kupiga magoti ardhini. Aliwaambia wanafunzi wake wasali.
Wakati wakisali, Yesu alikwenda mbali kidogo na watu na kupiga magoti na kusali kwa Baba wa Mbinguni.
Yesu alimshukuru Baba wa Mbinguni kwa kuwapa wanafunzi Roho Mtakatifu. Kisha aliomba kwa ajili ya Roho Mtakatifu kupewa kwa yoyote ambaye aliamini maneno ya wanafunzi.
Yesu aliwabariki wanafunzi wake walipokuwa wakisali. Alitabasamu kwao, na walikuwa wenye kung’aa kama uso na nguo zake.
Yesu alisali tena kwa ajili ya wanafunzi. Alifurahishwa na imani yao kuu.
Kristo aliwaambia watu kuacha kusali lakini waendelee kusali katika mioyo yao. Kisha aliwapa sakramenti.
Hakuna yoyote aliyekuwa ameleta mkate au divai, lakini Mwokozi alivileta kimiujiza.
Yesu Kristo aliwaambia Wanefi kwamba injili yake ingeletwa tena duniani katika siku za mwisho.
Aliwaambia wajifunze maandiko, na alimwambia Nefi aandike katika kumbukumbu utimizwaji wa sehemu za unabii zilizobaki za Samueli Mlamani.
Kisha Yesu alifundisha watu kutoka kwenye maandiko. Aliwaambia kufundishana vitu ambavyo aliwafundisha.
Yesu alirudi mbinguni, na wanafunzi wake waliwafundisha watu. Wale walioamini walibatizwa na kupokea Roho Mtakatifu.
Wanefi walianza kutii amri zote.