Scripture Stories
Sura ya 51: Wayaredi Wanasafiri Kwenda Nchi ya Ahadi


Sura ya 51

Wayaredi Wanasafiri Kwenda Nchi ya Ahadi

Picha
Kaka wa Yaredi na wingu

Wakati Wayaredi walipopiga hema ufukoni, kaka wa Yaredi alisahau kusali. Bwana alimjia katika wingu na kumwambia atubu.

Picha
Kaka wa Yaredi akisali

Kaka wa Yaredi alitubu na alisali. Bwana alimsamehe kaka wa Yaredi lakini alisema lazima asitende dhambi tena.

Picha
Kaka wa Yaredi akisali

Bwana alimwambia kaka wa Yaredi kutengeneza mashua ya kuwapeleka watu wake kwenda nchi ya ahadi.

Picha
Kaka wa Yaredi akiongea na Bwana

Bwana alimwambia kaka wa Yaredi jinsi ya kutengeneza mashua.

Picha
Wayaredi wakitengeneza mashua

Mashua zilikuwa hazipitishi hewa hivyo maji yasingeweza kuingia ndani.

Picha
Kaka wa Yaredi akiongea na Bwana

Kaka wa Yaredi alijiuliza ni kwa vipi watu wangeweza kupumua ndani ya mashua. Alimuuliza Bwana ni nini alipaswa kufanya.

Picha
Kaka wa Yaredi akiziba tundu

Bwana alimwambia kutengeneza shimo juu na chini ya kila mashua. Tundu lingeweza kufunuliwa na kuacha hewa kuingia na kufungwa kuziba maji yasiingie.

Picha
Kaka wa Yaredi akizungumza na Bwana

Kaka wa Yaredi alimwambia Bwana kwamba mashua zilikuwa na giza ndani. Bwana alimwambia kutafakari jinsi ya kuwa na mwanga ndani ya mashua.

Picha
Kaka wa Yaredi akimsikiliza Bwana

Mwanga kwa ajili ya mashua usingeweza kutoka katika moto au madirisha kwa sababu yangevunjika.

Picha
Kaka wa Yaredi akichonga mawe yenye kupenyeza mwanga

Kaka wa Yaredi alikwenda mlimani na kuchonga mawe madogo 16 toka kwenye mwamba. Mawe yalionekana kama kioo safi. Alichonga mawe mawili kwa ajili ya kila mashua nane.

Picha
Kaka wa Yaredi akipanda mlimani

Kaka wa Yaredi alibeba mawe mpaka kwenye kilele cha mlima. Huko alisali kwa Bwana

Picha
Kaka wa Yaredi akisali

Kaka wa Yaredi alimuomba Bwana kugusa mawe kwamba yatoe mwanga ndani ya mashua.

Picha
Kristo akigusa kila jiwe

Bwana aligusa kila jiwe kwa kidole Chake.

Picha
Kaka wa Yaredi

Kwa sababu kaka wa Yaredi alikuwa na imani kubwa, aliona kidole cha Bwana. Kilionekana kama kidole cha mwanadamu.

Picha
Kristo pamoja na kaka wa Yaredi

Kisha Bwana akijionyesha kwa kaka wa Yaredi.

Picha
Yesu Kristo

Yesu alisema watu wanaomwamini watapata uzima wa milele.

Picha
Yesu akimfundisha kaka wa Yaredi

Yesu alimfundisha na kumwonyesha kaka wa Yaredi vitu vingi. Yesu alimwambia kuviandika vile alivyoviona na kusikia.

Picha
Kaka wa Yaredi akishuka kutoka mlimani

Kaka wa Yaredi alibeba yale mawe kutoka mlimani. Aliweka jiwe moja katika kila mwisho wa mashua. Yalitoa mwanga ndani ya mashua.

Picha
Mashua majini

Wayaredi waliingia katika mashua pamoja na wanyama na chakula. Bwana alisababisha upepo mkali kusukuma mashua kuelekea nchi ya ahadi.

Picha
Kaka wa Yaredi

Bwana aliwalinda katika bahari yenye dhoruba. Walimshukuru Bwana na kuimba sifa Kwake.

Picha
Mashua zikiwasili katika nchi ya ahadi

Baada ya siku 344 kwenye maji, mashua zilifika ufukoni mwa nchi ya ahadi.

Picha
Wayaredi wakisali

Wakati Wayaredi walipotoka nje ya mashua, walipiga magoti na kulia machozi ya furaha.

Picha
Mwanamke akibeba ngano

Wayaredi walijenga miji na kupanda mazao katika nchi ya ahadi. Waliwafundisha watoto wao kumsikiliza Bwana na kutii maneno Yake.

Chapisha