Sura ya 51
Wayaredi Wanasafiri Kwenda Nchi ya Ahadi
Wakati Wayaredi walipopiga hema ufukoni, kaka wa Yaredi alisahau kusali. Bwana alimjia katika wingu na kumwambia atubu.
Kaka wa Yaredi alitubu na alisali. Bwana alimsamehe kaka wa Yaredi lakini alisema lazima asitende dhambi tena.
Bwana alimwambia kaka wa Yaredi kutengeneza mashua ya kuwapeleka watu wake kwenda nchi ya ahadi.
Bwana alimwambia kaka wa Yaredi jinsi ya kutengeneza mashua.
Mashua zilikuwa hazipitishi hewa hivyo maji yasingeweza kuingia ndani.
Kaka wa Yaredi alijiuliza ni kwa vipi watu wangeweza kupumua ndani ya mashua. Alimuuliza Bwana ni nini alipaswa kufanya.
Bwana alimwambia kutengeneza shimo juu na chini ya kila mashua. Tundu lingeweza kufunuliwa na kuacha hewa kuingia na kufungwa kuziba maji yasiingie.
Kaka wa Yaredi alimwambia Bwana kwamba mashua zilikuwa na giza ndani. Bwana alimwambia kutafakari jinsi ya kuwa na mwanga ndani ya mashua.
Mwanga kwa ajili ya mashua usingeweza kutoka katika moto au madirisha kwa sababu yangevunjika.
Kaka wa Yaredi alikwenda mlimani na kuchonga mawe madogo 16 toka kwenye mwamba. Mawe yalionekana kama kioo safi. Alichonga mawe mawili kwa ajili ya kila mashua nane.
Kaka wa Yaredi alibeba mawe mpaka kwenye kilele cha mlima. Huko alisali kwa Bwana
Kaka wa Yaredi alimuomba Bwana kugusa mawe kwamba yatoe mwanga ndani ya mashua.
Bwana aligusa kila jiwe kwa kidole Chake.
Kwa sababu kaka wa Yaredi alikuwa na imani kubwa, aliona kidole cha Bwana. Kilionekana kama kidole cha mwanadamu.
Kisha Bwana akijionyesha kwa kaka wa Yaredi.
Yesu alisema watu wanaomwamini watapata uzima wa milele.
Yesu alimfundisha na kumwonyesha kaka wa Yaredi vitu vingi. Yesu alimwambia kuviandika vile alivyoviona na kusikia.
Kaka wa Yaredi alibeba yale mawe kutoka mlimani. Aliweka jiwe moja katika kila mwisho wa mashua. Yalitoa mwanga ndani ya mashua.
Wayaredi waliingia katika mashua pamoja na wanyama na chakula. Bwana alisababisha upepo mkali kusukuma mashua kuelekea nchi ya ahadi.
Bwana aliwalinda katika bahari yenye dhoruba. Walimshukuru Bwana na kuimba sifa Kwake.
Baada ya siku 344 kwenye maji, mashua zilifika ufukoni mwa nchi ya ahadi.
Wakati Wayaredi walipotoka nje ya mashua, walipiga magoti na kulia machozi ya furaha.
Wayaredi walijenga miji na kupanda mazao katika nchi ya ahadi. Waliwafundisha watoto wao kumsikiliza Bwana na kutii maneno Yake.