Scripture Stories
Sura ya 30: Alma Anawashauri Wanawe


Sura ya 30

Alma Anawashauri Wanawe

Picha
Alma akizungumza na wana

Alma hakuwa na furaha kwa sababu ya jinsi ambavyo Wanefi walikuwa wamekuwa waovu. Alizungumza na kila mmoja wa wanawe kuhusu kuishi kwa njia ya haki.

Picha
malaika na Alma pamoja na wana wa Mosia

Alma alimwambia Helamani, mwanawe mkubwa , amwamini Mungu. Alimwambia kuhusu malaika ambaye Mungu alikuwa amemtuma kumwambia Alma aache kuangamiza Kanisa.

Picha
Alma akiteseka kitandani

Kwa siku tatu Alma alikuwa ameteseka kwa sababu ya majuto yake. Kisha akakumbuka mafundisho ya baba yake kuhusu Yesu, na akajua dhambi zake zingeweza kusamehewa.

Picha
Alma

Alma alisali kwa ajili ya msamaha, na shangwe ilichukua nafasi ya uchungu katika nafsi yake. Alisamehewa kwa sababu alikuwa na imani katika Yesu Kristo na alikuwa ametubu.

Picha
Alma akifundisha

Kuanzia wakati huo Alma alikuwa amewafundisha wengine injili ili waweze kuhisi shangwe sawa na ile aliyokuwa amehisi. Mungu alikuwa amembariki Alma kwa sababu ya imani yake kwa Mungu.

Picha
Alma akimpa Helamani maandiko

Alma alimpa Helamani maandiko matakatifu na kumwambia aendelee kuandika historia ya watu wao.

Picha
Alma akizungumza na Helamani

Alma alimwambia kwamba kama angetii amri, Mungu angembariki na kumsaidia kulinda maandiko hayo.

Picha
Alma na Helamani

Alma pia alimwambia Helamani asali kila asubuhi na usiku na kuzungumza na Mungu kuhusu kila kitu alichokuwa akifanya ili Mungu aweze kumsaidia kwa kumuongoza.

Picha
Shibloni

Alma alikuwa na furaha kwa ajili ya mwanawe Shibloni, ambaye alikuwa mmisionari jasiri kwa Wazoramu. Shibloni alikuwa amebaki mwaminifu hata wakati ambapo alikuwa amepigwa kwa mawe.

Picha
Alma na Shibloni

Alma alimkumbusha Shibloni kwamba njia pekee ya kuokolewa ni kupitia kwa Yesu Kristo. Alma kisha akawatia moyo wanawe waendelee kufundisha injili.

Picha
Koriantoni

Koriantoni mwana wa Alma hakuwa ametii amri. Hakuwa mmisionari mwaminifu wakati alipokuwa akiwafundisha Wazoramu.

Picha
Alma

Kwa sababu ya kile ambacho Koriantoni alikuwa amefanya, Wazoramu hawangeamini mahubiri ya Alma.

Picha
Alma na Koriantoni

Alma alimwambia Koriantoni kwamba watu hawawezi kuficha dhambi zao kwa Mungu na kwamba Koriantoni alihitaji kutubu.

Picha
Alma

Alma aliwafundisha wanawe kwamba kila mtu atafufuliwa lakini ni wenye haki tu ndiyo watakaoishi na Mungu.

Picha
Alma na Koriantoni

Maisha haya ni wakati wa watu kutubu na kumtumikia Mungu, Alma alisema.

Picha
Alma akimpa Koriantoni maandiko

Akimkumbusha Koriantoni kwamba alikuwa ameitwa kuwa mmisionari, Alma alimwambia arudi kwa Wazoramu na kuwafundisha watu watubu.

Picha
Alma na wanawe wakifundisha

Alma na wanawe waliendelea kufundisha injili. Walifundisha kwa uwezo wa ukuhani.

Chapisha