Sura ya 30
Alma Anawashauri Wanawe
Alma hakuwa na furaha kwa sababu ya jinsi ambavyo Wanefi walikuwa wamekuwa waovu. Alizungumza na kila mmoja wa wanawe kuhusu kuishi kwa njia ya haki.
Alma alimwambia Helamani, mwanawe mkubwa , amwamini Mungu. Alimwambia kuhusu malaika ambaye Mungu alikuwa amemtuma kumwambia Alma aache kuangamiza Kanisa.
Kwa siku tatu Alma alikuwa ameteseka kwa sababu ya majuto yake. Kisha akakumbuka mafundisho ya baba yake kuhusu Yesu, na akajua dhambi zake zingeweza kusamehewa.
Alma alisali kwa ajili ya msamaha, na shangwe ilichukua nafasi ya uchungu katika nafsi yake. Alisamehewa kwa sababu alikuwa na imani katika Yesu Kristo na alikuwa ametubu.
Kuanzia wakati huo Alma alikuwa amewafundisha wengine injili ili waweze kuhisi shangwe sawa na ile aliyokuwa amehisi. Mungu alikuwa amembariki Alma kwa sababu ya imani yake kwa Mungu.
Alma alimpa Helamani maandiko matakatifu na kumwambia aendelee kuandika historia ya watu wao.
Alma alimwambia kwamba kama angetii amri, Mungu angembariki na kumsaidia kulinda maandiko hayo.
Alma pia alimwambia Helamani asali kila asubuhi na usiku na kuzungumza na Mungu kuhusu kila kitu alichokuwa akifanya ili Mungu aweze kumsaidia kwa kumuongoza.
Alma alikuwa na furaha kwa ajili ya mwanawe Shibloni, ambaye alikuwa mmisionari jasiri kwa Wazoramu. Shibloni alikuwa amebaki mwaminifu hata wakati ambapo alikuwa amepigwa kwa mawe.
Alma alimkumbusha Shibloni kwamba njia pekee ya kuokolewa ni kupitia kwa Yesu Kristo. Alma kisha akawatia moyo wanawe waendelee kufundisha injili.
Koriantoni mwana wa Alma hakuwa ametii amri. Hakuwa mmisionari mwaminifu wakati alipokuwa akiwafundisha Wazoramu.
Kwa sababu ya kile ambacho Koriantoni alikuwa amefanya, Wazoramu hawangeamini mahubiri ya Alma.
Alma alimwambia Koriantoni kwamba watu hawawezi kuficha dhambi zao kwa Mungu na kwamba Koriantoni alihitaji kutubu.
Alma aliwafundisha wanawe kwamba kila mtu atafufuliwa lakini ni wenye haki tu ndiyo watakaoishi na Mungu.
Maisha haya ni wakati wa watu kutubu na kumtumikia Mungu, Alma alisema.
Akimkumbusha Koriantoni kwamba alikuwa ameitwa kuwa mmisionari, Alma alimwambia arudi kwa Wazoramu na kuwafundisha watu watubu.
Alma na wanawe waliendelea kufundisha injili. Walifundisha kwa uwezo wa ukuhani.