Sura ya 11
Enoshi
Enoshi alikuwa mwana wa Yakobo. Alizihifadhi bamba na kuandika ndani yake baada ya baba yake kufariki.
Siku moja Enoshi alikuwa akiwinda ndani ya msitu. Alifikiria kuhusu mafundisho ya baba yake na akataka msamaha wa dhambi zake.
Enoshi alipiga magoti na kusali kwa Mungu. Alisali siku nzima na alikuwa angali anasali usiku ulipofika.
Mungu alimwambia Enoshi kwamba kwa sababu ya imani yake katika Yesu Kristo, dhambi zake zilikuwa zimesamehewa.
Kisha Enoshi alitaka Bwana awabariki Wanefi. Alisali kwa niaba yao, na Bwana akasema angewabariki ikiwa wangetii amri zake.
Enoshi pia alitaka Bwana awabariki Walamani. Alisali kwa imani kubwa, na Bwana aliahidi kufanya kile ambacho Enoshi alimuomba.
Ingawaje Walamani walipigana na Wanefi na kujaribu kuharibu kumbukumbu zao, Enoshi alisali kwamba wangekuja kuwa watu wenye haki.
Enoshi alisali kwamba kumbukumbu alizokuwa ameweka zingelindwa. Bwana aliahidi kwamba siku moja angewapa Walamani mafundisho ambayo yalikuwa katika kumbukumbu.
Enoshi aliwahubiria Wanefi. Aliwataka wamwamini Mungu na kutii amri.
Wanefi walijaribu kuwafundisha Walamani injili, lakini hawakuwasikiliza. Walamani waliwachukia Wanefi.
Enoshi alitumia maisha yake kuwafundisha watu kuhusu Yesu na injili. Alimtumikia Mungu na kumpenda siku zake zote.