Scripture Stories
Sura ya 11: Enoshi


Sura ya 11

Enoshi

Picha
Yakobo akimpa Enoshi bamba

Enoshi alikuwa mwana wa Yakobo. Alizihifadhi bamba na kuandika ndani yake baada ya baba yake kufariki.

Picha
Enoshi akiwinda

Siku moja Enoshi alikuwa akiwinda ndani ya msitu. Alifikiria kuhusu mafundisho ya baba yake na akataka msamaha wa dhambi zake.

Picha
Enoshi akisali

Enoshi alipiga magoti na kusali kwa Mungu. Alisali siku nzima na alikuwa angali anasali usiku ulipofika.

Picha
Enoshi akisali

Mungu alimwambia Enoshi kwamba kwa sababu ya imani yake katika Yesu Kristo, dhambi zake zilikuwa zimesamehewa.

Picha
Enoshi akisali

Kisha Enoshi alitaka Bwana awabariki Wanefi. Alisali kwa niaba yao, na Bwana akasema angewabariki ikiwa wangetii amri zake.

Picha
Walamani

Enoshi pia alitaka Bwana awabariki Walamani. Alisali kwa imani kubwa, na Bwana aliahidi kufanya kile ambacho Enoshi alimuomba.

Picha
Walamani wakipigana na Wanefi

Ingawaje Walamani walipigana na Wanefi na kujaribu kuharibu kumbukumbu zao, Enoshi alisali kwamba wangekuja kuwa watu wenye haki.

Picha
Enoshi akisali

Enoshi alisali kwamba kumbukumbu alizokuwa ameweka zingelindwa. Bwana aliahidi kwamba siku moja angewapa Walamani mafundisho ambayo yalikuwa katika kumbukumbu.

Picha
Enoshi akiwahubiria Wanefi

Enoshi aliwahubiria Wanefi. Aliwataka wamwamini Mungu na kutii amri.

Picha
Walamani wakifanya kazi

Wanefi walijaribu kuwafundisha Walamani injili, lakini hawakuwasikiliza. Walamani waliwachukia Wanefi.

Picha
Enoshi akiandika

Enoshi alitumia maisha yake kuwafundisha watu kuhusu Yesu na injili. Alimtumikia Mungu na kumpenda siku zake zote.

Chapisha