Scripture Stories
Sura ya 49: Mormoni na Mafundisho Yake


Sura ya 49

Mormoni na Mafundisho Yake

Picha
makundi mawili ya watu

Miaka mingi baada ya Yesu Kristo kuwatembelea Wanefi, kundi dogo la watu liliacha Kanisa na kujiita Walamani.

Picha
Kundi likizungumza

Hatimaye karibu watu wote walikuwa waovu, wote Wanefi na Walamani.

Picha
Amaroni akificha kumbukumbu

Mtu mwenye haki, Amaroni, alikuwa na kumbukumbu takatifu. Roho Mtakatifu alimwambia azifiche kwamba ziwe salama.

Picha
Amaroni akiongea na Mormoni mdogo

Amaroni alimwambia Mormoni, mvulana wa miaka 10, wapi kumbukumbu zilikuwa zimefichwa. Amaroni alijua angeweza kumwamini Mormoni.

Picha
Amaroni na Mormoni

Wakati alipokuwa na miaka 24, Mormoni aliweza kuchukua bamba za Nefi na kuandika kuhusu watu wake.

Picha
Wanefi na Walamani wakipigana vita

Wakati Mormoni alipokuwa na miaka 11, vita ilianza kati ya Wanefi na walamani. Wanefi walishinda, na kulikuwa na amani tena.

Picha
Watu wakilewa

Lakini Wanefi walikuwa waovu sana kwamba Bwana aliwachukua wanafunzi watatu, jambo ambalo lilihitimisha miujiza na uponyaji. Roho Mtakatifu hakuwaongoza tena watu.

Picha
Mormoni

Wakati Mormoni alipokuwa na miaka 15 Yesu Kristo alimtembelea. Mormoni alijifunza zaidi kuhusu Mwokozi na wema Wake.

Picha
Mormoni akiwaangalia watu wawili

Mormoni alitaka kuwafundisha watu, lakini Yesu alimwambia asifanye hivyo kwa sababu watu walikuwa waovu sana. Mioyo yao ilikuwa dhidi ya Mungu.

Picha
Mormoni kama kiongozi wa jeshi

Punde vita nyingine ilianza Mormoni alikuwa mkubwa na mwenye nguvu, na Wanefi walimchagua yeye kuongoza jeshi lao.

Picha
Mormoni akizungumza na jeshi

Wanefi walipigana na Walamani kwa miaka mingi. Mormoni alijaribu kuwatia moyo watu wake kupigana kwa ajili ya familia na nyumba zao.

Picha
vita

Wanefi walikuwa waovu sana, kwamba Bwana asingewasaidia.

Picha
Mormoni akiongea na watu

Mormoni aliwaambia Wanefi wangelindwa kama tu wangetubu na kubatizwa. Lakini watu walikataa.

Picha
Mormoni akiliangalia jeshi

Walijivuna kuhusu nguvu zao wenyewe, wakisema wangewauwa walamani wote. Kwa sababu ya uovu wa Wanefi, Mormoni alikataa kuwaongoza.

Picha
Mormoni amesimama pamoja na jeshi

Walamani walianza kuwashinda Wanefi katika kila vita. Mormoni aliamua kuliongoza jeshi tena.

Picha
Mormoni amekaa

Alijua Wanefi waovu wasingeshinda vita. Hawakutubu wala kusali kwa ajili ya msaada waliouhitaji.

Picha
Mormoni akizifukua kumbukumbu

Mormoni alichukua kumbukumbu zote kutoka kwenye mlima ambapo Amaroni alikuwa amezificha na kuwaandikia watu ambao siku moja wangezisoma.

Picha
Mormoni akiwa na kumbukumbu takatifu

Alitaka kila mtu, ikijumuisha Myahudi, kujua kuhusu Yesu Kristo, kutubu na kubatizwa, na kuishi injili na kubarikiwa.

Picha
Mormoni akiandika kwenye bamba takatifu

Roho alimtia msukumo Mormoni kuweka bamba ndogo za Nefi, ambazo zilikuwa zimebeba unabii wa kuja kwa Kristo, na bamba za Mormoni.

Picha
Jeshi la Mormoni

Mormoni aliwaongoza Wanefi kwenye mji wa Kumora, ambapo walijiandaa kupigana na Walamani tena.

Picha
Mormoni amebeba bamba

Mormoni alikuwa akizeeka. Alijua hii ingekuwa vita ya mwisho. Hakutaka Walamani wazipate kumbukumbu takatifu na kuziharibu.

Picha
Mormoni akimpa Moroni bamba

Hivyo alimpa mwanawe Moroni, bamba za Mormoni, na kuficha bamba zilizobaki katika Mlima Kumora.

Picha
Wanefi wakifa

Walamani waliwavamia Wanefi na kuwauwa wote isipokuwa Wanefi 24. Mormoni alikuwa amejeruhiwa.

Picha
Mormoni akiwa amejeruhiwa

Mormoni alihuzunika kwamba Wanefi wengi walikuwa wamekufa, lakini alijua kuwa walikufa kwa sababu ya kumkataa Yesu.

Picha
Yesu Kristo

Mormoni alikuwa amejaribu kuwafundisha Wanefi ukweli. Alikuwa amewaambia jinsi gani ilikuwa muhimu kuwa na imani katika Yesu Kristo.

Picha
Mormoni akifundisha

Alikuwa amejaribu kuwafundisha kuwa na tumaini kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo na kuwa na hisani, ambayo ni upendo msafi wa Kristo.

Picha
Mormoni akiandika barua

Na mormoni alikuwa ameandika barua kwa mwanaye , Moroni, ambaye alikuwa amefundisha injili kwa Wanefi.

Picha
Moroni akisoma barua

Mormoni aliandika barua kuhusu uovu wa kuogofya wa Wanefi. Alimwambia Moroni kubakia mwaminifu katika Yesu Kristo.

Picha
Mormoni akiuwawa

Walamani walimuua Mormoni na Wanefi wote isipokuwa Moroni aliyemalizia kuandika kumbukumbu.

Chapisha