Sura ya 49
Mormoni na Mafundisho Yake
Miaka mingi baada ya Yesu Kristo kuwatembelea Wanefi, kundi dogo la watu liliacha Kanisa na kujiita Walamani.
Hatimaye karibu watu wote walikuwa waovu, wote Wanefi na Walamani.
Mtu mwenye haki, Amaroni, alikuwa na kumbukumbu takatifu. Roho Mtakatifu alimwambia azifiche kwamba ziwe salama.
Amaroni alimwambia Mormoni, mvulana wa miaka 10, wapi kumbukumbu zilikuwa zimefichwa. Amaroni alijua angeweza kumwamini Mormoni.
Wakati alipokuwa na miaka 24, Mormoni aliweza kuchukua bamba za Nefi na kuandika kuhusu watu wake.
Wakati Mormoni alipokuwa na miaka 11, vita ilianza kati ya Wanefi na walamani. Wanefi walishinda, na kulikuwa na amani tena.
Lakini Wanefi walikuwa waovu sana kwamba Bwana aliwachukua wanafunzi watatu, jambo ambalo lilihitimisha miujiza na uponyaji. Roho Mtakatifu hakuwaongoza tena watu.
Wakati Mormoni alipokuwa na miaka 15 Yesu Kristo alimtembelea. Mormoni alijifunza zaidi kuhusu Mwokozi na wema Wake.
Mormoni alitaka kuwafundisha watu, lakini Yesu alimwambia asifanye hivyo kwa sababu watu walikuwa waovu sana. Mioyo yao ilikuwa dhidi ya Mungu.
Punde vita nyingine ilianza Mormoni alikuwa mkubwa na mwenye nguvu, na Wanefi walimchagua yeye kuongoza jeshi lao.
Wanefi walipigana na Walamani kwa miaka mingi. Mormoni alijaribu kuwatia moyo watu wake kupigana kwa ajili ya familia na nyumba zao.
Wanefi walikuwa waovu sana, kwamba Bwana asingewasaidia.
Mormoni aliwaambia Wanefi wangelindwa kama tu wangetubu na kubatizwa. Lakini watu walikataa.
Walijivuna kuhusu nguvu zao wenyewe, wakisema wangewauwa walamani wote. Kwa sababu ya uovu wa Wanefi, Mormoni alikataa kuwaongoza.
Walamani walianza kuwashinda Wanefi katika kila vita. Mormoni aliamua kuliongoza jeshi tena.
Alijua Wanefi waovu wasingeshinda vita. Hawakutubu wala kusali kwa ajili ya msaada waliouhitaji.
Mormoni alichukua kumbukumbu zote kutoka kwenye mlima ambapo Amaroni alikuwa amezificha na kuwaandikia watu ambao siku moja wangezisoma.
Alitaka kila mtu, ikijumuisha Myahudi, kujua kuhusu Yesu Kristo, kutubu na kubatizwa, na kuishi injili na kubarikiwa.
Roho alimtia msukumo Mormoni kuweka bamba ndogo za Nefi, ambazo zilikuwa zimebeba unabii wa kuja kwa Kristo, na bamba za Mormoni.
Mormoni aliwaongoza Wanefi kwenye mji wa Kumora, ambapo walijiandaa kupigana na Walamani tena.
Mormoni alikuwa akizeeka. Alijua hii ingekuwa vita ya mwisho. Hakutaka Walamani wazipate kumbukumbu takatifu na kuziharibu.
Hivyo alimpa mwanawe Moroni, bamba za Mormoni, na kuficha bamba zilizobaki katika Mlima Kumora.
Walamani waliwavamia Wanefi na kuwauwa wote isipokuwa Wanefi 24. Mormoni alikuwa amejeruhiwa.
Mormoni alihuzunika kwamba Wanefi wengi walikuwa wamekufa, lakini alijua kuwa walikufa kwa sababu ya kumkataa Yesu.
Mormoni alikuwa amejaribu kuwafundisha Wanefi ukweli. Alikuwa amewaambia jinsi gani ilikuwa muhimu kuwa na imani katika Yesu Kristo.
Alikuwa amejaribu kuwafundisha kuwa na tumaini kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo na kuwa na hisani, ambayo ni upendo msafi wa Kristo.
Na mormoni alikuwa ameandika barua kwa mwanaye , Moroni, ambaye alikuwa amefundisha injili kwa Wanefi.
Mormoni aliandika barua kuhusu uovu wa kuogofya wa Wanefi. Alimwambia Moroni kubakia mwaminifu katika Yesu Kristo.
Walamani walimuua Mormoni na Wanefi wote isipokuwa Moroni aliyemalizia kuandika kumbukumbu.