Sura ya 8
Kuvuka Bahari
Upepo mkali uliisukuma merikebu kuelekea nchi ya ahadi.
Lamani, Lemueli, na baadhi ya wengine walianza kuwa waovu. Wakati Nefi alipowaambia kuacha uovu, walimkasirikia na wakamfunga kwa kamba.
Kwa sababu ya uovu wao, Liahona iliacha kufanya kazi. Hawakujua ni upande upi wangeiongoza merikebu. Dhoruba kali ilisukuma merikebu kurudi nyuma kwa siku tatu.
Lehi aliwaambia Lamani na Lemueli wamfungue Nefi, lakini hawakumsikiliza. Lehi na Saria walihuzunika sana mpaka kwamba wakaugua.
Mke na watoto wa Nefi walilia. Waliwaomba Lamani na Lemueli wamfungue Nefi, lakini walikataa.
Katika siku ya nne dhoruba ilikuwa kali zaidi. Merikebu ilikuwa karibu kuzama.
Lamani na Lemueli walijua kwamba Mungu ameruhusu dhoruba. Waliogopa kwamba wangezama.
Hatimaye Lamani na Lemueli walitubu na kumfungua Nefi. Japokuwa viwiko vyake na vifundo vilikuwa vimevimba na vyenye maumivu kutokana na kamba, Nefi hakunung’unika.
Kisha Nefi akaichukua Liahona, na ikafanya kazi tena. Nefi akasali, na upepo ukakoma. Bahari ikawa shwari.
Nefi akaiongoza merikebu, na ikaelekea tena uelekeo wa nchi ya ahadi.