Scripture Stories
Sura ya 43: Yesu Kristo Anawatokea watu wa Nefi


Sura ya 43

Yesu Kristo Anawatokea watu wa Nefi

Picha
Wanefi wanakusanyika

Wanefi wengi walikusanyika karibu na hekalu kule Neema. Walistaajabishwa na mabadiliko makuu nchini.

Picha
watu wakizungumza

Watu walikuwa wakizungumza kuhusu Yesu Kristo na ishara ya kifo chake.

Picha
Watu wakisikia sauti tulivu

Wakiwa wanazungumza, walisikia sauti tulivu kutoka mbinguni. Ilisababisha mioyo yao kuwaka.

Picha
Mwanaume akiwa amemshikilia mwanamke

Mara ya kwanza hawakuitambua sauti hiyo, lakini wakati ilipozungumza mara ya tatu, waliielewa.

Picha
watu wakisikiliza

Sauti ilikuwa ya Baba wa Mbinguni. Ilimtambulisha Yesu Kristo na kuwaambia watu wamsikilize.

Picha
Yesu akiwa miongoni mwa watu

Yesu Kristo alishuka chini kutoka mbinguni na kusimama miongoni mwa watu. Walikuwa na uwoga wa kuzungumza kwa maana hawakuelewa kilichokuwa kikitendeka. Walidhania Yesu alikuwa malaika.

Picha
Yesu akizungumza na watu

Aliwaambia kwamba alikuwa Yesu Kristo, ambaye manabii walisema atakuja.

Picha
Yesu akiwa na watu

Yesu aliwaambia watu waje na waguse alama ubavuni mwake na katika mikono na miguu, ambapo alipigiliwa misumari msalabani.

Picha
Yesu akiwa ameketi na watoto

Yesu aliwataka watu wajue kwamba alikuwa Mungu wao na kwamba alikuwa amekufa kwa ajili ya dhambi zao.

Picha
Kristo na Wanefi

Mmoja baada ya mwingine watu waligusa alama ubavuni, mikononi, na miguuni mwa Yesu. Watu walifahamu kwamba alikuwa Mwokozi.

Picha
watu wakimwabudu Yesu

Kisha watu walimsifu Yesu na kuinama miguuni mwake na kumwabudu.

Picha
Yesu akiwapa wanaume ukuhani

Yesu alimwita Nefi na watu wengine 11 waende kwake. Aliwapa nguvu za ukuhani na kuwafundisha njia sahihi ya kubatiza.

Picha
Yesu akiwafundisha watu

Aliwaambia Wanefi wamwamini, watubu na watii amri. Kama hawangefanya hivyo, hawangeweza kuingia katika ufalme wake.

Picha
Yesu akiwafundisha watu

Aliwafundisha Wanefi jinsi ya kuomba kwa Baba wa Mbinguni. Pia aliwafundisha kuhusu kufunga na akasema wangesamehewa kama wangesameheana.

Picha
Yesu akiwafundisha watu

Baada ya kuwafundisha watu vitu vingi, Yesu aliwaambia waende nyumbani na kufikiria na kusali kuhusu kile alichokuwa amesema.

Picha
Wanefi wanalia

Wanefi walianza kulia. Hawakutaka Yesu aondoke.

Picha
Yesu akiwafundisha watu

Yesu aliwapenda Wanefi. Aliwaambia wawalete kwake watu waliokuwa wagonjwa au waliokuwa wameumia ili aweze kuwaponya.

Picha
Yesu akimponya mtoto

Yesu aliwaponya hawa watu. Kila mtu aliinama na kumwabudu.

Chapisha