Scripture Stories
Sura ya 33: Watu wa Mfalme dhidi ya Watu Huru


Sura ya 33

Watu wa Mfalme dhidi ya Watu Huru

Picha
Pahorani akizungumza na wengine

Baadhi ya Wanefi walimtaka mwamuzi mkuu, Pahorani, kubadili baadhi ya sheria.

Picha
watu wamekasirika

Wakati Pahorani alipokataa, watu walimkasirikia na wakataka kumuondoa Pahorani kama mwamuzi mkuu. Walitaka kuwa na mfalme, na si waamuzi.

Picha
Watu wawili wakiongea

Wakijiita watu wa mfalme, walitumaini kwamba mmoja wao angekuwa mfalme na kuwa na nguvu juu ya watu.

Picha
Kikundi cha wanaume wakisali

Watu waliokuwa wakimtaka Pahorani kama mwamuzi mkuu waliitwa watu huru. Walitaka kuwa huru kuishi na kuabudu kama wapendavyo.

Picha
Wanaume kwenye mstari wa kupiga kura

Watu walipiga kura kati ya watu huru na watu wa mfalme. Wengi wao walipigia kura upande wa watu huru.

Picha
Jeshi la Walamani

Wakati huohuo, Amalikia alikuwa akikusanya jeshi kubwa la Walamani kuwashambulia Wanefi.

Picha
Watu wa mfalme

Wakati watu wa mfalme waliposikia kwamba Walamani wanakuja, walifurahia na wakakataa kuilinda nchi yao.

Picha
Moroni akiwaangalia watu wa mfalme

Kapteni Moroni aliwakasirikia watu wa mfalme kwa kutopigana. Alikuwa amefanya kazi sana kuwaweka Wanefi kuwa huru.

Picha
Moroni akiongea na gavana

Alimuomba gavana mamlaka ya kuwafanya watu wa mfalme wapigane na Walamani au wauwawe.

Picha
Gavana akiongea na Moroni

Wakati Gavana, Pahorani, alipompa Moroni mamlaka haya, Moroni aliliongoza jeshi lake dhidi ya watu wa mfalme.

Picha
Wanefi na Walamani wakipigana

Wengi wa Watu wa mfalme waliuwawa; baadhi wakafungwa gerezani. Waliobaki walikubali kusaidia kuilinda nchi yao dhidi ya Walamani.

Chapisha