Sura ya 32
Kapteni Moroni na Bendera ya Uhuru
Mtu mwovu aliyeitwa Amalikia alitaka kuwa mfalme wa Wanefi. Wanefi wengi waliacha Kanisa kumfuata.
Kama Amalikia angekuwa mfalme, angejaribu kuharibu Kanisa la Mungu na kuchukua uhuru wa watu.
Wakati Kapteni Moroni, kiongozi wa majeshi ya Wanefi, aliposikia juu ya mpango wa Amalikia kuwa mfalme, alikasirika.
Moroni alichana koti kutengeneza bendera. Juu yake aliandika ujumbe kuwakumbusha watu kulinda dini, uhuru, na amani yao.
Moroni aliweka bendera kwenye mlingoti na kuiita bendera ya uhuru. Kisha alivaa vazi lake la kivita, akapiga magoti kusali.
Alimuomba Mungu kuwalinda wale walioamini katika Yesu Kristo na kusali kwa ajili ya uhuru katika nchi, wakiiita nchi ya uhuru.
Moroni alienda kati ya watu. Akipeperusha bendera, aliwaita kuja na kusaidia kuulinda uhuru.
Watu walikuja kutoka kila sehemu zote za nchi. Waliahidi kutii amri za Mungu na kupigana kwa ajili ya uhuru.
Wakati Amalikia alipoona jinsi Wanefi walivyojiunga na Moroni, aliogopa. Yeye na wafuasi wake walikwenda kuungana na Walamani.
Moroni na jeshi lake walijaribu kuwazuia, lakini Amalikia na baadhi ya wafuasi wake walitoroka.
Moroni aliweka bendera ya uhuru katika kila mnara katika nchi ya Wanefi. Wanefi walikuwa na uhuru wao tena na amani.