Scripture Stories
Sura ya 32: Kapteni Moroni na Bendera ya Uhuru


Sura ya 32

Kapteni Moroni na Bendera ya Uhuru

Picha
Amalikia akiongea

Mtu mwovu aliyeitwa Amalikia alitaka kuwa mfalme wa Wanefi. Wanefi wengi waliacha Kanisa kumfuata.

Picha
Amalikia

Kama Amalikia angekuwa mfalme, angejaribu kuharibu Kanisa la Mungu na kuchukua uhuru wa watu.

Picha
Moroni akimwangalia Amalikia

Wakati Kapteni Moroni, kiongozi wa majeshi ya Wanefi, aliposikia juu ya mpango wa Amalikia kuwa mfalme, alikasirika.

Picha
Moroni akiandika kwenye bendera

Moroni alichana koti kutengeneza bendera. Juu yake aliandika ujumbe kuwakumbusha watu kulinda dini, uhuru, na amani yao.

Picha
Moroni akisali

Moroni aliweka bendera kwenye mlingoti na kuiita bendera ya uhuru. Kisha alivaa vazi lake la kivita, akapiga magoti kusali.

Picha
Moroni akisali

Alimuomba Mungu kuwalinda wale walioamini katika Yesu Kristo na kusali kwa ajili ya uhuru katika nchi, wakiiita nchi ya uhuru.

Picha
Moroni akipeperusha bendera

Moroni alienda kati ya watu. Akipeperusha bendera, aliwaita kuja na kusaidia kuulinda uhuru.

Picha
Watu wakikusanyika kumzunguka Moroni

Watu walikuja kutoka kila sehemu zote za nchi. Waliahidi kutii amri za Mungu na kupigana kwa ajili ya uhuru.

Picha
Amalikia na wafuasi wake wakikimbia

Wakati Amalikia alipoona jinsi Wanefi walivyojiunga na Moroni, aliogopa. Yeye na wafuasi wake walikwenda kuungana na Walamani.

Picha
Moroni na jeshi lake

Moroni na jeshi lake walijaribu kuwazuia, lakini Amalikia na baadhi ya wafuasi wake walitoroka.

Picha
Bendera ikipepepa kwenye mnara

Moroni aliweka bendera ya uhuru katika kila mnara katika nchi ya Wanefi. Wanefi walikuwa na uhuru wao tena na amani.

Chapisha