Scripture Stories
Watu wa Kujua


Watu wa Kujua

Haruni

Mwana wa Mfalme Mosia na mmisionari kwa Walamani

Abinadi

Nabii aliyetumwa kumfundisha Mfalme Nuhu, ambaye alisababisha Abinadi kuuwawa kwa kuchomwa moto

Adamu

Mtu wa kwanza duniani

Alma

Kuhani wa mfalme Nuhu ambaye aliamini mafundisho ya Abinadi na baadaye alikuwa kiongozi wa Kanisa

Alma Mdogo

Mwana wa Alma ambaye aliasi na kujaribu kuharibu Kanisa lakini alipata badiliko la moyo na alianza kufundisha injili. Alikuja kuwa kiongozi wa Kanisa na mwamuzi mkuu wa kwanza.

Amalikia

Mtu mwovu aliyetaka kuwa mfalme wa Wanefi lakini ambaye angechukua uhuru wa watu. Wakati aliposhindwa kuwa mfalme, aliondoka na kujiunga na Walamani.

Amlisi

Mtu mwovu aliyetaka kuwa mfalme wa Wanefi. Wakati alipokataliwa kuwa malme, yeye pamoja na wafuasi wake waliondoka, waliwashambulia Wanefi, na kisha walijiunga na Walamani.

Waamlisi

Wafuasi wa amlisi. Walijichora kwa alama nyekundu kwenye mapaji ya nyuso zao na walijiungana Walamani.

Amaroni

Mtu mwenye haki ambaye alimpa Mormoni kumbukumbu kwamba ziwe salama.

Amoni1

Kiongozi wa kikundi cha Wanefi kutoka Zarahemla waliokwenda kwenye nchi ya Nefi na kuwasaidia Wanefi waliokuwa huko kutoroka

Amoni2

Mmoja kati ya wana wa Mosia waliolinda mifugo ya mfalme Lamoni dhidi ya wezi. Alifundisha na kuwaongoa wengi wa Walamani wakati wa umisionari wake.

Watu wa Amoni

Walamani walioongoka kutokana na wana wa Mosia. Walizika silaha zao za kivita na kuweka agano kamwe kutopigana tena

Amuleki

Mmisionari mwenza wa Alma Mdogo. Walifungwa gerezani lakini walitumia nguvu za Mungu kufanya kuta za gereza kuanguka.

Amuloni

Kuhani mwovu wa Mfalme Nuhu ambaye alifanywa mtawala juu ya watu wa Alma. Aliwafanya wafanye kazi sana na alitishia kumuua yoyote aliyekamatwa akisali.

Anti-Nefi–Lehi

(ona Watu wa, Amoni)

Mfalme, Benyamini

Mfalme mwenye haki aliyesimama kwenye mnara kuwafundisha watu wake kuhusu Yesu Kristo

Kaka wa Yaredi

Nabii aliyemuomba Yesu kugusa mawe 16 ili kwamba yatoe mwanga katika mashua ambazo Wayaredi walitumia kusafiri kwenda nchi ya ahadi

Koriantoni

Mwana wa Alma Mdogo ambaye hakuwa mmisionari mwaminifu na mwenye haki

Koriantumuri

Mfalme mwovu ambaye alikuwa Myaredi wa mwisho kuishi

Enoshi

Mwana wa Yakobo ambaye alisali siku nzima na usiku. Alisali kwa ajili ya Wanefi na Walamani.

Etheri

Nabii ambaye aliwaonya Wayaredi watubu na aliandika kuhusu kuangamizwa kwao

Hawa

Mwanamke wa kwanza duniani

Watu huru

Wanefi waliotaka uhuru wa kuishi na kuabudu wapendavyo. Walitawaliwa na waamuzi, na si mfalme.

Gideoni

Mnefi mwenye haki ambaye alilinda Kanisa wakati Nehori alipoanza kufundisha uongo kwa watu. Nehori alimuua.

Hagothi

Mnefi mtengeneza meli ambaye alichukua wengi wa Wanefi kwenda katika nchi iliyokuwa kaskazini

Helamani

Mwana mkubwa wa Alma Mdogo. Alipewa bamba na kuambiwa kuandika historia ya watu wake. Pia alikuwa kiongozi wa vijana mashujaa 2,000.

Himni

Mwana wa Mfalme Mosia na mmisionari kwa Walamani

Ishmaeli

Mtu kutoka Yerusalemu ambaye alisafiri kwenda nchi ya ahadi pamoja na familia ya Lehi. Binti zake waliolewa na wana wa Lehi.

Yakobo

Mwana wa Lehi na Saria. Alikabiliana na Sheremu, ambaye alisema Kristo hayupo.

Wayaredi

Waliomfuata Yaredi na kaka yake ambao waliondoka Babeli na kusafiri kwenda nchi ya ahadi kwa mashua

Yusufu

Mwana mwenye haki wa Lehi na Saria ambaye alizaliwa nyikani

Joseph Smith, Mdogo.

Nabii wa siku za mwisho ambaye alitafsiri Kitabu cha Mormoni kutoka kwenye bamba za dhahabu

Watu wa mfalme

Wanefi ambao walitaka kutawaliwa na mfalme na si waamuzi. Wakati waliposhindwa kuwa na mfalme, walijiunga na Walamani na kuwashambulia Wanefi.

Korihori

Mtu mwovu aliyetaka ishara kuthibitisha kwamba Mungu anaishi. Mungu alimpa Korihori ishara kwa kuchukua sauti yake.

Labani

Mtu mwovu huko Yerusalemu ambaye hakutaka kuwapa wana wa Lehi bamba za shaba.

Lamani

Mwana mkubwa wa Lehi na Saria. Alimkuwa mwovu na mkaidi dhidi ya Mungu.

Lamani, Mfalme

Mfalme mwovu wa Walamani ambaye alimpa Zenivu na Wanefi waliomfuata miji miwili lakini kisha aliwavamia

Walamani

Uzao au wafuasi wa Lamani na Lemueli au watu ambao walikataa injili

Lamoni, Mfalme

Mfalme wa Walamani ambaye alifundishwa injili na aliiamini. Amoni2 alilinda mifugo ya mfalme dhidi ya wezi.

Lamoni, baba wa Mfalme

Mfalme wa Walamani ambaye alifundishwa injili na aliiamini. Alisema angetubu dhambi zake zote ili kumjua Mungu.

Lehi1

Nabii ambaye alionya kwamba Yesrusalemu ingeangamizwa. Alisikiliza wakati Mungu alipomwambia kuichukua familia yake kwenda nyikani.

Lehi2

mwana wa Helamani. Yeye pamoja na kaka yake, Nefi, walitupwa gerezani na kuzungukwa na moto.

Lemueli

Mwana mwovu wa Lehi na Saria

Limhi, Mfalme

Mwana mwema wa Nuhu Mfalme mwovu. Yeye na watu wake walikuwa watumwa wa Walamani lakini walitoroka

Mariamu

mama yake Yesu

Mormoni

Kiongozi wa jeshi la Wanefi na mmoja wa nabii wa mwisho wa Wanefi. Alikiweka pamoja Kitabu cha Mormoni.

Moroni

Mwana wa Mormoni na nabii wa mwisho wa Wanefi. Alifukia bamba za dhahabu na baadae alimtokea Joseph smith kama malaika.

Moroni, Kapteni

Kiongozi mwenye haki wa jeshi la Wanefi. Alitengeneza bendera ya uhuru na kuliambia jeshi lake kupigania uhuru wao.

Mosia, Mfalme

Mfalme wa mwisho wa wanefi. Alikuwa na wana wanne.

Nehori

Mtu mwovu aliyepinga kwa ujasiri Kanisa la Mungu. Alimuua Gideoni na yeye aliuwawa.

Nefi1

Mwana mwenye haki wa Lehi na Saria. Alipata bamba za shaba kutoka kwa Labani na kutengeneza meli ambayo ilibeba familia yake kwenda nchi ya ahadi.

Nefi2

mwana wa Helamani. Yeye na kaka yake, Lehi, walitupwa gerezani na walizungukwa na moto. Nefi alisababaisha baa la njaa ili kuwafundisha watu watubu.

Nefi3

Mtu mwenye haki aliyechaguliwa na Yesu Kristo kuwa mwanafunzi na kiongozi wa Kanisa

Wanefi

Wafuasi wa Nefi au watu walikubali injili

Nuhu, Mfalme

Mfalme mwovu wa Wanefi ambaye alipenda utajiri na aliwafundisha watu wake kuwa waovu. Watu wake mwenyewe walimuua kwa kumchoma moto.

Omneri

Mwana wa Mfalme Mosia na mmisionari kwa Walamani

Pahorani

Mwamuzi mkuu wa Wanefi ambaye alimsaidia Kapteni Moroni kuwashinda wanefi waovu

Samu

Mwana mwenye haki wa Lehi na Saria

Samueli Mlamani

Nabii ambaye alitoa unabii kwa wanefi kuhusu ishara za kuzaliwa na za kufa kwa Yesu Kristo

Saria

Lehi1 mke wa

Seantumu

Kaka wa Seezoramu na aliyemuua Seezoramu

Seezoramu

Mwamuzi mkuu ambaye aliuwawa na kaka yake

Sheremu

Mnefi mwovu aliyetaka ishara kwanza kabla ya kuamini katika Yesu Kristo

Shizi

Myaredi mwovu ambaye aliongoza jeshi dhidi ya Koriantumuri na alikuwa ni mmoja wa Wayaredi wa mwisho kuishi

Wana wa Mosia

Wana wa Mosia: Haruni, Amoni,2 Himni, na Omneri, ambao walikuwa wamisionari thabiti kwa Walamani

Vijana mashujaa elfu mbili

Jeshi la vijana wa Amoni liliongozwa na Helamani. Walipigana ili kwamba wazazi wao, waliokuwa wameingia kwenye la agano kutopigana, wasipigane.

Zeezromu

Mwanasheria ambaye alimuahidi Amuleki fedha ili kusema kwamba Mungu hayupo. Alma Mdogo alimfundisha injili, na alitubu

Zenivu

Kiongozi mwenye haki ambaye alichukua kundi la Wanefi kutoka Zarahemla kwenda nchi ya Nefi, ambapo waliwekwa utumwani na Lamani Mfalme mwovu

Zerahemna

Kingozi wa Walamani ambaye alipigana na Wanefi na alitaka Wanefi wawe watumwa wake. Alikatwa ngozi ya juu ya kichwa katika vita dhidi ya jeshi la Kapateni Moroni.

Zoramu

Mtumishi wa Labani ambaye alisafiri na familia ya Lehi kwenda nchi ya ahadi

Wazoramu

Watu waovu ambao mwanzo walikuwa watu wa kanisa la Mungu. Walisali ndani ya masinagogi wakisimama kwenye jukwaa lilioitwa Rameumtomu.

Chapisha