Watu wa Kujua
- Haruni
-
Mwana wa Mfalme Mosia na mmisionari kwa Walamani
- Abinadi
-
Nabii aliyetumwa kumfundisha Mfalme Nuhu, ambaye alisababisha Abinadi kuuwawa kwa kuchomwa moto
- Adamu
-
Mtu wa kwanza duniani
- Alma
-
Kuhani wa mfalme Nuhu ambaye aliamini mafundisho ya Abinadi na baadaye alikuwa kiongozi wa Kanisa
- Alma Mdogo
-
Mwana wa Alma ambaye aliasi na kujaribu kuharibu Kanisa lakini alipata badiliko la moyo na alianza kufundisha injili. Alikuja kuwa kiongozi wa Kanisa na mwamuzi mkuu wa kwanza.
- Amalikia
-
Mtu mwovu aliyetaka kuwa mfalme wa Wanefi lakini ambaye angechukua uhuru wa watu. Wakati aliposhindwa kuwa mfalme, aliondoka na kujiunga na Walamani.
- Amlisi
-
Mtu mwovu aliyetaka kuwa mfalme wa Wanefi. Wakati alipokataliwa kuwa malme, yeye pamoja na wafuasi wake waliondoka, waliwashambulia Wanefi, na kisha walijiunga na Walamani.
- Waamlisi
-
Wafuasi wa amlisi. Walijichora kwa alama nyekundu kwenye mapaji ya nyuso zao na walijiungana Walamani.
- Amaroni
-
Mtu mwenye haki ambaye alimpa Mormoni kumbukumbu kwamba ziwe salama.
- Amoni1
-
Kiongozi wa kikundi cha Wanefi kutoka Zarahemla waliokwenda kwenye nchi ya Nefi na kuwasaidia Wanefi waliokuwa huko kutoroka
- Amoni2
-
Mmoja kati ya wana wa Mosia waliolinda mifugo ya mfalme Lamoni dhidi ya wezi. Alifundisha na kuwaongoa wengi wa Walamani wakati wa umisionari wake.
- Watu wa Amoni
-
Walamani walioongoka kutokana na wana wa Mosia. Walizika silaha zao za kivita na kuweka agano kamwe kutopigana tena
- Amuleki
-
Mmisionari mwenza wa Alma Mdogo. Walifungwa gerezani lakini walitumia nguvu za Mungu kufanya kuta za gereza kuanguka.
- Amuloni
-
Kuhani mwovu wa Mfalme Nuhu ambaye alifanywa mtawala juu ya watu wa Alma. Aliwafanya wafanye kazi sana na alitishia kumuua yoyote aliyekamatwa akisali.
- Anti-Nefi–Lehi
-
(ona Watu wa, Amoni)
- Mfalme, Benyamini
-
Mfalme mwenye haki aliyesimama kwenye mnara kuwafundisha watu wake kuhusu Yesu Kristo
- Kaka wa Yaredi
-
Nabii aliyemuomba Yesu kugusa mawe 16 ili kwamba yatoe mwanga katika mashua ambazo Wayaredi walitumia kusafiri kwenda nchi ya ahadi
- Koriantoni
-
Mwana wa Alma Mdogo ambaye hakuwa mmisionari mwaminifu na mwenye haki
- Koriantumuri
-
Mfalme mwovu ambaye alikuwa Myaredi wa mwisho kuishi
- Enoshi
-
Mwana wa Yakobo ambaye alisali siku nzima na usiku. Alisali kwa ajili ya Wanefi na Walamani.
- Etheri
-
Nabii ambaye aliwaonya Wayaredi watubu na aliandika kuhusu kuangamizwa kwao
- Hawa
-
Mwanamke wa kwanza duniani
- Watu huru
-
Wanefi waliotaka uhuru wa kuishi na kuabudu wapendavyo. Walitawaliwa na waamuzi, na si mfalme.
- Gideoni
-
Mnefi mwenye haki ambaye alilinda Kanisa wakati Nehori alipoanza kufundisha uongo kwa watu. Nehori alimuua.
- Hagothi
-
Mnefi mtengeneza meli ambaye alichukua wengi wa Wanefi kwenda katika nchi iliyokuwa kaskazini
- Helamani
-
Mwana mkubwa wa Alma Mdogo. Alipewa bamba na kuambiwa kuandika historia ya watu wake. Pia alikuwa kiongozi wa vijana mashujaa 2,000.
- Himni
-
Mwana wa Mfalme Mosia na mmisionari kwa Walamani
- Ishmaeli
-
Mtu kutoka Yerusalemu ambaye alisafiri kwenda nchi ya ahadi pamoja na familia ya Lehi. Binti zake waliolewa na wana wa Lehi.
- Yakobo
-
Mwana wa Lehi na Saria. Alikabiliana na Sheremu, ambaye alisema Kristo hayupo.
- Wayaredi
-
Waliomfuata Yaredi na kaka yake ambao waliondoka Babeli na kusafiri kwenda nchi ya ahadi kwa mashua
- Yusufu
-
Mwana mwenye haki wa Lehi na Saria ambaye alizaliwa nyikani
- Joseph Smith, Mdogo.
-
Nabii wa siku za mwisho ambaye alitafsiri Kitabu cha Mormoni kutoka kwenye bamba za dhahabu
- Watu wa mfalme
-
Wanefi ambao walitaka kutawaliwa na mfalme na si waamuzi. Wakati waliposhindwa kuwa na mfalme, walijiunga na Walamani na kuwashambulia Wanefi.
- Korihori
-
Mtu mwovu aliyetaka ishara kuthibitisha kwamba Mungu anaishi. Mungu alimpa Korihori ishara kwa kuchukua sauti yake.
- Labani
-
Mtu mwovu huko Yerusalemu ambaye hakutaka kuwapa wana wa Lehi bamba za shaba.
- Lamani
-
Mwana mkubwa wa Lehi na Saria. Alimkuwa mwovu na mkaidi dhidi ya Mungu.
- Lamani, Mfalme
-
Mfalme mwovu wa Walamani ambaye alimpa Zenivu na Wanefi waliomfuata miji miwili lakini kisha aliwavamia
- Walamani
-
Uzao au wafuasi wa Lamani na Lemueli au watu ambao walikataa injili
- Lamoni, Mfalme
-
Mfalme wa Walamani ambaye alifundishwa injili na aliiamini. Amoni2 alilinda mifugo ya mfalme dhidi ya wezi.
- Lamoni, baba wa Mfalme
-
Mfalme wa Walamani ambaye alifundishwa injili na aliiamini. Alisema angetubu dhambi zake zote ili kumjua Mungu.
- Lehi1
-
Nabii ambaye alionya kwamba Yesrusalemu ingeangamizwa. Alisikiliza wakati Mungu alipomwambia kuichukua familia yake kwenda nyikani.
- Lehi2
-
mwana wa Helamani. Yeye pamoja na kaka yake, Nefi, walitupwa gerezani na kuzungukwa na moto.
- Lemueli
-
Mwana mwovu wa Lehi na Saria
- Limhi, Mfalme
-
Mwana mwema wa Nuhu Mfalme mwovu. Yeye na watu wake walikuwa watumwa wa Walamani lakini walitoroka
- Mariamu
-
mama yake Yesu
- Mormoni
-
Kiongozi wa jeshi la Wanefi na mmoja wa nabii wa mwisho wa Wanefi. Alikiweka pamoja Kitabu cha Mormoni.
- Moroni
-
Mwana wa Mormoni na nabii wa mwisho wa Wanefi. Alifukia bamba za dhahabu na baadae alimtokea Joseph smith kama malaika.
- Moroni, Kapteni
-
Kiongozi mwenye haki wa jeshi la Wanefi. Alitengeneza bendera ya uhuru na kuliambia jeshi lake kupigania uhuru wao.
- Mosia, Mfalme
-
Mfalme wa mwisho wa wanefi. Alikuwa na wana wanne.
- Nehori
-
Mtu mwovu aliyepinga kwa ujasiri Kanisa la Mungu. Alimuua Gideoni na yeye aliuwawa.
- Nefi1
-
Mwana mwenye haki wa Lehi na Saria. Alipata bamba za shaba kutoka kwa Labani na kutengeneza meli ambayo ilibeba familia yake kwenda nchi ya ahadi.
- Nefi2
-
mwana wa Helamani. Yeye na kaka yake, Lehi, walitupwa gerezani na walizungukwa na moto. Nefi alisababaisha baa la njaa ili kuwafundisha watu watubu.
- Nefi3
-
Mtu mwenye haki aliyechaguliwa na Yesu Kristo kuwa mwanafunzi na kiongozi wa Kanisa
- Wanefi
-
Wafuasi wa Nefi au watu walikubali injili
- Nuhu, Mfalme
-
Mfalme mwovu wa Wanefi ambaye alipenda utajiri na aliwafundisha watu wake kuwa waovu. Watu wake mwenyewe walimuua kwa kumchoma moto.
- Omneri
-
Mwana wa Mfalme Mosia na mmisionari kwa Walamani
- Pahorani
-
Mwamuzi mkuu wa Wanefi ambaye alimsaidia Kapteni Moroni kuwashinda wanefi waovu
- Samu
-
Mwana mwenye haki wa Lehi na Saria
- Samueli Mlamani
-
Nabii ambaye alitoa unabii kwa wanefi kuhusu ishara za kuzaliwa na za kufa kwa Yesu Kristo
- Saria
-
Lehi1 mke wa
- Seantumu
-
Kaka wa Seezoramu na aliyemuua Seezoramu
- Seezoramu
-
Mwamuzi mkuu ambaye aliuwawa na kaka yake
- Sheremu
-
Mnefi mwovu aliyetaka ishara kwanza kabla ya kuamini katika Yesu Kristo
- Shizi
-
Myaredi mwovu ambaye aliongoza jeshi dhidi ya Koriantumuri na alikuwa ni mmoja wa Wayaredi wa mwisho kuishi
- Wana wa Mosia
-
Wana wa Mosia: Haruni, Amoni,2 Himni, na Omneri, ambao walikuwa wamisionari thabiti kwa Walamani
- Vijana mashujaa elfu mbili
-
Jeshi la vijana wa Amoni liliongozwa na Helamani. Walipigana ili kwamba wazazi wao, waliokuwa wameingia kwenye la agano kutopigana, wasipigane.
- Zeezromu
-
Mwanasheria ambaye alimuahidi Amuleki fedha ili kusema kwamba Mungu hayupo. Alma Mdogo alimfundisha injili, na alitubu
- Zenivu
-
Kiongozi mwenye haki ambaye alichukua kundi la Wanefi kutoka Zarahemla kwenda nchi ya Nefi, ambapo waliwekwa utumwani na Lamani Mfalme mwovu
- Zerahemna
-
Kingozi wa Walamani ambaye alipigana na Wanefi na alitaka Wanefi wawe watumwa wake. Alikatwa ngozi ya juu ya kichwa katika vita dhidi ya jeshi la Kapateni Moroni.
- Zoramu
-
Mtumishi wa Labani ambaye alisafiri na familia ya Lehi kwenda nchi ya ahadi
- Wazoramu
-
Watu waovu ambao mwanzo walikuwa watu wa kanisa la Mungu. Walisali ndani ya masinagogi wakisimama kwenye jukwaa lilioitwa Rameumtomu.