Sura ya 4
Bamba za Shaba
Lehi alimwambia Nefi kwamba Bwana aliwataka yeye na kaka zake kurudi Yerusalemu. Walitakiwa kupata bamba za shaba kutoka kwa mtu aitwaye Labani
Bamba za shaba zilikuwa ni kumbukumbu muhimu . Zilizungumzia kuhusu mababu wa Lehi na zilikuwa na maneno ya Mungu yaliyofunuliwa kupitia manabii.
Lamani na Lemueli hawakutaka kurudi kuchukua Bamba za shaba. Walisema ingekuwa ni vigumu sana kufanya hivyo. Hawakuwa na imani katika Bwana.
Nefi alitaka kumtii Bwana Alijua Bwana angemsaidia yeye na kaka zake kupata bamba za shaba kutoka kwa Labani.
Lamani, Lemueli, Samu na Nefi walisafiri kurudi Yerusalemu kufuata bamba za shaba
Lamani alikwenda kwa Labani
Labani alikasirika na hangempa Lamani bamba za shaba. Labani alitaka kumuua Lamani, lakini Lamani alitoroka
Lamani aliwaambia kaka zake kilichotokea. Alikuwa akiogopa na alitaka kukata tamaa na kurudi kwa baba yao nyikani.
Nefi alisema wasingeweza kurudi bila bamba za shaba. Aliwaambia kaka zake wawe na imani zaidi katika Bwana na wangeweza kupata bamba za shaba.
Nefi na kaka zake walikwenda kwenye mji wao wa zamani huko Yerusalemu na kukusanya dhahabu yao na fedha ili kubadilishana kupata bamba.
Walimwonyesha Labani utajiri wao na kumuomba kubadilishana kwa bamba. Wakati Labani alipoiona dhahabu yao na fedha, aliitaka kwa ajili yake mwenyewe na akawafukuza nje.
Labani Aliwaambia watu wake kuwaua wana wa Lehi Nefi na kaka zake walikimbia na kujificha pangoni. Labani aliichukua dhahabu yao na fedha.
Lamani na Lemueli walimkasirikia Nefi. Waliwapiga Nefi na Samu kwa fimbo.
Malaika akawatokea na kuwaambia Lamani na Lemueli kuacha kuwapiga. Aliwaambia Bwana angewasaidia wao kupata bamba. Pia alisema kwamba Nefi angekuwa kiongozi juu ya kaka zake.
Nefi aliwaambia kaka zake kuwa na imani katika Bwana na kutomwogopa Labani na watu wake. Nefi aliwatia moyo kaka zake kurudi tena Yerusalemu
Usiku ule kaka zake Nefi walijificha nje ya ukuta wa mji wakati Nefi akijipenyeza ndani kwa kunyatia. Alitembea kuelekea nyumba ya Labani.
Wakati Nefi alipofika karibu na nyumba ya Labani, alimuona mtu amelala chini akiwa amelewa. Alikuwa ni Labani
Nefi aliuona upanga wa Labani na kuuchukua. Roho mtakatifu alimwambia Nefi amuue Labani, lakini Nefi hakutaka kumuua.
Roho Mtakatifu alimwambia Nefi tena kumuua Labani ili kwamba Nefi aweze kupata bamba za dhahabu. Familia ya Lehi walihitaji bamba ili kwamba waweze kujifunza injili.
Nefi alimtii Roho Mtakatifu na alimuua Labani. Kisha Nefi akavaa mavazi na vazi la kivita la Labani.
Nefi alikwenda ndani ya nyumba ya Labani na alikutana na Zoramu, mtumishi wa Labani. Nefi alionekana na kuongea kama Labani
Alimwambia Zoramu alete bamba za shaba. Zoramu alidhani Nefi ni Labani, hivyo akampa mabamba. Nefi alimwambia Zoramu amfuate.
Lamani, Lemueli, na Samu walimuona Nefi akija na waliogopa; walidhani alikuwa ni Labani. Walianza kukimbia lakini walisimama wakati Nefi alipowaita.
Kisha Zoramu akatambua kwamba Nefi hakuwa Labani, na alijaribu kukimbia. Nefi alimkamata Zoramu na kumuahidi kutomdhuru kama angeenda nao nyikani.
Zoramu alikubali. Nefi pamoja na kaka zake walimchukua Zoramu na bamba za shaba na kurudi kwa Lehi na Saria.
Walimpa Lehi bamba za shaba Yeye na Saria walikuwa na furaha wana wao walikuwa salama. Wote walifurahi na kumshukuru Mungu
Lehi akisoma bamba za dhahabu. Zilizungumzia kuhusu Adamu na Hawa na Uumbaji wa dunia. Zilikuwa na maneno ya manabii wengi.
Lehi na Nefi walifurahi kwa sababu walikuwa wametii amri ya Bwana na walikuwa wameweza kupata bamba za dhahabu.
Lehi na familia yake walibeba bamba za dhahabu pamoja nao safarini ili kwamba waweze kuwafundisha watoto wao amri zilizoandikwa kwenye bamba.