Scripture Stories
Mlango wa 6: Ndoto ya Lehi


Sura ya 6

Ndoto ya Lehi

Picha
Lehi na familia

Lehi aliiambia familia yake kuhusu ono muhimu alilokuwa ameona katika ndoto. Ndoto ya Lehi ilimpa furaha kwa ajili ya Nefi na Samu lakini ikampa huzuni kwa ajili ya Lamani na Lemueli.

Picha
Lehi na malaika

Katika ndoto yake Lehi alimuona mwanaume akiwa amevalia joho jeupe ambaye alimwambia Lehi amfuate. Lehi alimfuata mwanaume huyo katika nyika yenye giza na yenye kuhuzunisha.

Picha
Lehi akisali

Baada ya kusafiri gizani kwa masaa mengi, Lehi alisali kwa ajili ya msaada.

Picha
mti wa uzima

Kisha akaona mti wenye tunda jeupe. Tunda hili tamu liliwafanya waliolila kuwa wenye furaha.

Picha
Lehi akila tunda

Lehi alikula tunda, na lilimjaza na shangwe. Alitaka familia yake ionje tunda kwa sababu alijua lingewafanya wawe na furaha pia.

Picha
Saria, Samu, na Nefi wanatembea kuelekea mahali alipo Lehi

Lehi aliona mto ukitiririka kando ya mti. Mwishoni mwa mto aliwaona Saria, Samu, na Nefi.

Picha
Familia ikitembea kuelekea kwenye mti

Lehi aliwaita mkewe na wanawe waje na waonje lile tunda. Saria, Samu, na Nefi walienda na kuonja tunda, lakini Lamani na Lemueli walikataa.

Picha
fimbo inayoongoza hadi kwenye mti

Lehi pia aliona fimbo ya chuma na njia nyembamba na iliyosonga ikielekea kwenye mti.

Picha
watu wakishikilia fimbo

Aliwaona watu wengi wakitembea kwenye njia au kuelekea kwenye njia. Kwa sababu ya ukungu wa giza, wengine walitangatanga kutoka kwenye njia na wakapotea.

Picha
Watu wakishikilia fimbo

Wengine walishikilia kwa nguvu fimbo ya chuma na kuongozwa kwa usalama kupita kwenye giza hadi kuufikia mti. Walionja tunda.

Picha
watu wakila tunda

Watu waliokuwa ndani ya jengo pana kwenye ng’ambo nyingine ya mto waliwafanyia mzaha wale waliokuwa wakila tunda. Wengine ambao walikuwa wamekula tunda waliaibika na kuondoka kutoka kwenye mti.

Picha
jengo kubwa na pana

Lehi aliwaona watu wengi katika ndoto yake. Baadhi walishikilia kwa nguvu fimbo ya chuma na kuongozwa kupita kwenye giza hadi kuufikia mti. Walionja tunda. Wengine walienda kwenye lile jengo kubwa au walizama ndani ya mto au wakapotea. Lamani na Lemueli walikataa kula tunda. Lehi alikuwa na wasiwasi juu yao na alijaribu kuwasaidia kutii amri za Mungu.

Chapisha