Sura ya 26
Watu wa Amoni
Wana wa Mosia walifundisha injili kwa Walamani. Maelfu ya Walamani walitubu na kujiunga na Kanisa.
Walamani waliojiunga na Kanisa walijiita Wa Anti-Nefi-Lehi, au watu wa Amoni. Walikuwa wema, wenye juhudi katika kazi.
Walamani ambao hawakutubu waliwakasirikia watu wa Amoni na wakajiandaa kupigana nao.
Watu wa Amoni walijua kwamba Walamani waovu wangekuja kuwauwa lakini walichagua kutopigana nao. Walikuwa wametubu kuua.
Walizika silaha zao chini ardhini na kumuahidi Mungu kamwe hawangeua tena.
Wakati Walamani waovu walipokuja na kuanza kuwauwa, waliinama ardhini na kusali.
Kwa kuona kwamba watu wa Amoni hawangepigana na wao, wengi wa Walamani waovu waliacha kuwauwa.
Walamani walijisikia vibaya kwamba walikuwa wameua. Walitupa chini silaha zao na kujiunga na watu wa Amoni. Hawangepigana tena.
Walamani zaidi walikuja kuwauwa watu wa Amoni. Lakini bado hawakupigana nao, na wengi waliuwawa.
Kwa kutaka watu aliowapenda wasiuwawe, Amoni alisali kwa ajili ya msaada. Bwana alimwambia kuwachukua watu wake kutoka kwenye nchi.
Wanefi huko Zarahemla walimpa Amoni na watu wake nchi ya Jershoni na kuwalinda. Walikuwa marafiki.