Scripture Stories
Sura ya 26: Watu wa Amoni


Sura ya 26

Watu wa Amoni

Picha
Mosia akiwafundisha Walamani

Wana wa Mosia walifundisha injili kwa Walamani. Maelfu ya Walamani walitubu na kujiunga na Kanisa.

Picha
Waanti-Nefi Lehi

Walamani waliojiunga na Kanisa walijiita Wa Anti-Nefi-Lehi, au watu wa Amoni. Walikuwa wema, wenye juhudi katika kazi.

Picha
Walamani wakijiandaa kupigana

Walamani ambao hawakutubu waliwakasirikia watu wa Amoni na wakajiandaa kupigana nao.

Picha
Watu wa Amoni

Watu wa Amoni walijua kwamba Walamani waovu wangekuja kuwauwa lakini walichagua kutopigana nao. Walikuwa wametubu kuua.

Picha
Watu wakizika silaha

Walizika silaha zao chini ardhini na kumuahidi Mungu kamwe hawangeua tena.

Picha
Walamani wakija na watu wakisali

Wakati Walamani waovu walipokuja na kuanza kuwauwa, waliinama ardhini na kusali.

Picha
Walamani wakisimama kuwazunguka watu wa Amoni

Kwa kuona kwamba watu wa Amoni hawangepigana na wao, wengi wa Walamani waovu waliacha kuwauwa.

Picha
Walamani wakiweka chini silaha zao

Walamani walijisikia vibaya kwamba walikuwa wameua. Walitupa chini silaha zao na kujiunga na watu wa Amoni. Hawangepigana tena.

Picha
Walamani wakiwauwa watu wa Amoni

Walamani zaidi walikuja kuwauwa watu wa Amoni. Lakini bado hawakupigana nao, na wengi waliuwawa.

Picha
Amoni akisali

Kwa kutaka watu aliowapenda wasiuwawe, Amoni alisali kwa ajili ya msaada. Bwana alimwambia kuwachukua watu wake kutoka kwenye nchi.

Picha
Watu wa Amoni na Wanefi wa Zarahemla

Wanefi huko Zarahemla walimpa Amoni na watu wake nchi ya Jershoni na kuwalinda. Walikuwa marafiki.

Chapisha