Scripture Stories
Sura ya 17: Alma na Watu Wake Wanatoroka


Sura ya 17

Alma na Watu Wake Wanatoroka

Picha
watu wakifanya kazi shambani

Siku moja wakati watu wa Alma walipokuwa wakifanya kazi katika mashamba yao, jeshi la Walamani lilivuka mpaka na kuingia nchini mwao.

Picha
Alma akizungumza na watu

Wanefi waliogopa na kukimbilia mjini kwa ajili ya usalama. Alma aliwaambia wamkumbuke Mungu na angewasaidia. Wanefi walianza kusali.

Picha
Alma akizungumza na Walamani

Bwana alilainisha mioyo ya Walamani, na hawakuwadhuru Wanefi. Walamani walikuwa wamepotea walipokuwa wakijaribu kuwatafuta watu wa Mfalme Limhi.

Picha
Alma akiwaonyesha Walamani njia ya kwenda nyumbani

Walamani walimwahidi Alma ya kwamba hawangewasumbua watu wake kama angewaonyesha njia ya kurudi nchini kwao. Alma aliwaonyesha njia.

Picha
Walamani wakiwalinda watu wa Alma

Lakini Walamani hawakutunza ahadi yao. Waliweka walinzi kuzunguka sehemu hiyo, na Alma na watu wake hawakuwa huru tena.

Picha
Amuloni akizungumza na mlinzi mlamani

Mfalme Mlamani alimfanya Amuloni kuwa kiongozi wa watu wa Alma. Amuloni alikuwa Mnefi na kuhani mwovu wa Mfalme Nuhu.

Picha
Amuloni akiwatazama watu wakifanya kazi

Amuloni aliwasababisha watu wa Alma kufanya kazi kwa bidii sana. Walisali kwa ajili ya msaada, lakini Amuloni alisema kwamba mtu yeyote ambaye angepatikana akisali angeuawa. Watu waliendelea kusali mioyoni mwao.

Picha
mvulana akiwa amebeba kikapu

Mungu alisikia sala zao na kuwaimarisha watu hivyo kazi yao ikaonekana kuwa rahisi. Watu walikuwa wenye furaha na wenye subira.

Picha
Mungu akizungumza na Alma

Mungu alifurahia kwamba watu walikuwa waaminifu. Alimwambia Alma kwamba angewasaidia kutoroka kutoka kwa Walamani.

Picha
Watu wa Alma wakitoroka

Wakati wa usiku watu walikusanya vyakula na mifugo. Asubuhi iliyofuata Mungu alizidisha usingizi wa Walamani wakati Alma na watu wake walipokuwa wakitoroka mjini.

Picha
Mfalme Mosia akimaribisha Alma

Baada ya kusafiri kwa siku 12, watu waliwasili Zarahemla, ambapo Mfalme Mosia na watu wake waliwakaribisha.

Chapisha