Sura ya 7
Kujenga Merikebu
Baada ya familia ya Lehi kupiga kambi kwa siku nyingi ufukoni mwa bahari, Bwana aliongea na Nefi. Alimwambia ajenge merikebu ya kuwabeba familia yake kwenda nchi ya ahadi.
Nefi hakujua jinsi ya kujenga merikebu, lakini Bwana alimwambia angemwonyesha. Alimwambia Nefi wapi pa kupata metali ili kutengeneza zana ambazo angehitaji
Lamani na Lemueli walimcheka Nefi kwa kutaka kujenga merikebu. Hawakuamini kwamba Bwana angemwonyesha Nefi jinsi ya kuijenga. Walikataa kumsaidia.
Nefi aliwaambia Lamani na Lemueli kutubu na wasiwe wakaidi. Aliwakumbusha wao kwamba walikuwa wamemuona malaika. Pia aliwaambia wao kwamba Mungu ana nguvu ya kufanya vitu vyote.
Lamani na Lemueli walimkasirikia Nefi na wakataka kumtupa baharini.
Wakati walipokuwa wakimkaribia Nefi, aliwaamuru wasimguse kwa sababu alikuwa amejazwa na nguvu za Mungu. Lamani na Lemueli waliogopa kwa siku nyingi.
Kisha Bwana akamwambia Nefi awaguse Lamani na Lemueli. Nefi alipofanya hivyo, Bwana aliwatikisa. Lamani na Lemueli walijua Nefi alikuwa na nguvu za Mungu.
Nefi aliwaambia Lamani na Lemueli wawatii wazazi wao na wamtii Mungu. Nefi alisema kama wangefanya hivi, wangebarikiwa.
Lamani na Lemueli walitubu na wakamsaidia Nefi kujenga merikebu.
Nefi alikwenda mlimani mara nyingi kusali kwa ajili ya msaada. Bwana alimfundisha jinsi ya kujenga merikebu.
Wakati Nefi na kaka zake walipokuwa wamekamilisha kujenga merikebu, walijua ilikuwa ni merikebu nzuri. Walimshukuru Mungu kwa kuwasaidia.