Sura ya 24
Amoni anakutana na Baba wa Mfalme Lamoni
Mfalme Lamoni alitaka kumpeleka Amoni kukutana na baba yake. Bwana alimuonya Amoni asiende kwa sababu baba wa Lamoni angejaribu kumuua.
Bwana alimwambia Amoni badala yake kwenda katika nchi ya Midoni, ambapo Haruni kaka yake alikuwa gerezani. Mfalme Lamoni alikwenda na Amoni.
Wakati wakisafiri walikutana na baba yake Mfalme Lamoni, ambaye alikuwa mfalme katika nchi nzima. Alimuuliza Lamoni wapi alikuwa akienda na Mnefi mdanganyifu.
Mfalme Lamoni alimwambia baba yake kuhusu Amoni na kaka yake aliyekuwa gerezani. Kwa hasira, baba yake Lamoni aliamuru Lamoni amuue Amoni na kurudi Midoni.
Lamoni alikataa kumuua amoni na alisema yeye na amoni walikuwa wakienda kumtoa Haruni gerezani. Baba yake Lamoni alikasirika zaidi na akatoa upanga ili kumuua Lamoni.
Amoni alisonga mbele na kumlinda Lamoni. Baba wa Lamoni kisha alijaribu kumuua Amoni, lakini alijilinda na akajeruhi mkono wa baba wa Lamoni.
Wakati baba wa Lamoni alipoona kwamba Amoni angemuua, alimuahidi Amoni nusu ya ufalme wake kama angemwacha hai.
Amoni alisema alitaka Haruni na wenzake waachiliwe huru kutoka gerezani na alitaka Lamoni abakie na ufalme wake.
Baba wa Lamoni alitambua kwamba Amoni hakutaka kumuumiza. Alishangazwa na jinsi gani Amoni alivyompenda mtoto wake. Alimwalika Amoni amfundishe injili.
Amoni na Mfalme Lamoni walikwenda Midoni. Lamoni aliongea na mfalme wa huko, na Haruni na wenzake waliachiliwa kutoka gerezani.
Amoni alikuwa na huzuni kuwaona jinsi kwa duni walivyotendewa. Walikuwa wameteseka kwa mengi lakini walikuwa wavumilivu.