Scripture Stories
Sura ya 14: Abinadi na Mfalme Nuhu


Sura ya 14

Abinadi na Mfalme Nuhu

Picha
Zenifu

Zenifu alikuwa mfalme mwenye haki wa kundi la Wanefi. Alipozeeka, mtoto wake Nuhu alikuwa mfalme.

Picha
Nuhu

Nuhu hakuwa mfalme mzuri kama baba yake. Alikuwa mwovu na hangetii amri za Mungu.

Picha
Watu wakimpa mfalme Nuhu mali yao.

Aliwalazimisha watu wake kumpa sehemu ya kipato chao, mifugo, dhahabu na fedha.

Picha
Nuhu akiwa katika meza ya chakula

Mfalme Nuhu alifanya hivi kwa kuwa alikuwa mvivu. Aliwafanya Wanefi kumpa kila kitu alichohitaji ili kuishi.

Picha
makuhani wema na makuhani waovu

Aliwaweka makuhani waovu badala ya wale wema ambao baba yake aliwaweka. Makuhani hawa waovu waliwafundisha watu kutenda dhambi.

Picha
Kiti cha enzi na walinzi

Mfalme Nuhu alikuwa na majengo mengi mazuri, ikijumuisha kasri kubwa lenye kiti cha enzi. Majengo yalikuwa yamepambwa kwa dhahabu, fedha na mbao za thamani sana.

Picha
Nuhu

Nuhu aliupenda utajiri aliochukua kutoka kwa watu wake. Yeye pamoja na makuhani wake walitumia muda wao kunywa mvinyo na kuwa waovu.

Picha
Abinadi akifundisha toba

Mungu alimtuma nabii aliyeitwa Abinadi kwa watu wa Nuhu. Abinadi aliwaonya kwamba kama hawangetubu, wangekuwa watumwa wa walamani.

Picha
Nuhu akiwa mezani

Wakati mfalme Nuhu aliposikia kile Abinadi alichosema, alikasirika. Aliwatuma watu kumpleka Abinadi kwenye kasri ili kwamba amuue.

Picha
Abinadi akiongea na mfalme

Abinadi alipelekwa kwa mfalme. Mfalme Nuhu na makuhani wake walimuuliza maswali mengi. Walijaribu kumtega katika kusema kitu kisicho sahihi.

Picha
Abinadi akiongea na mfalme

Abinadi hakuogopa kujibu maswali yao. alijua kwamba Mungu angemsaidia. Makuhani walishangazwa na majibu ya Abinadi.

Picha
Mfalme Nuhu amejawa na hasira

Mfalme Nuhu alikasirika na kuamuru makuhani wake kumuua Abinadi. Abinadi aliwaambia kama wangemgusa, Mungu angewaua.

Picha
Roho Mtakatifu anamlinda Abinadi

Roho Mtakatifu alimlinda Abinadi ili kwamba angemaliza kusema Bwana alichomtaka kusema. Uso wa Abinadi uling’aa. Makuhani waliogopa kumgusa.

Picha
Abinadi akinena

Akinena kwa nguvu kutoka kwa Mungu, Abinadi aliwaambia watu kuhusu uovu wao. Aliwasomea amri za Mungu.

Picha
Mariamu, Yusufu, na mtoto Yesu.

Aliwaambia Yesu Kristo angezaliwa duniani. Yesu angefanya iwezekane kwa watu kutubu, kufufuka, na kuishi na Mungu.

Picha
Yesu Kristo

Abinadi aliwaambia watu watubu na kuamini katika Yesu Kristo au sivyo wasingeokolewa.

Picha
Abinadi akichukuliwa kama mfungwa

Mfalme Nuhu na wengine wote isipokuwa mmoja wa makuhani wake walikataa kumwamini Abinadi. Nuhu aliwaambia makuhani kumuua Abinadi. Walimfunga na kumtupa gerezani.

Picha
Alma akiongea na mfalme Nuhu

Kuhani mmoja aliyemwamini Abinadi aliitwa Alma. Alimuomba mfalme Nuhu kumruhusu Abinadi aende.

Picha
Alma akijificha

Mfalme alimkasirikia Alma na akamfukuza. Kisha akatuma watumishi wake kumuua. Alma alikimbia na kujificha, na watumishi wa mfalme hawakumpata.

Picha
Abinadi Mbele ya Nuhu

Baada ya kukaa kwa siku tatu gerezani, Abinadi aliletwa tena mbele ya Mfalme Nuhu. Mfalme alimwambia Abinadi kukanusha alichokisema dhidi yake na watu wake.

Picha
Mfalme Nuhu amejawa na hasira

Mfalme Nuhu alimwambia Abinadi kwamba kama hatakanusha yote aliyoyasema, atauwawa.

Picha
Abinadi akinena

Abinadi alijua alikuwa amezungumza ukweli. Alikuwa tayari kufa kuliko kukanusha kile Mungu alichomtuma kusema.

Picha
Abinadi akichomwa moto

Mfalme Nuhu aliamrisha makuhani wake kumuua Abinadi. Walimfunga, wakamchapa kwa mjeledi, na kumchoma moto mpaka kufa. Kabla hajafa, Abinadi alisema Mfalme Nuhu pia angekufa kwa kuchomwa moto.

Picha
Walamani wakipigana na watu wa Nuhu

Baadhi ya Wanefi walimpinga Mfalme Nuhu na kujaribu kumuua. Jeshi la Walamani pia lilikuja kupigana na mfalme na watu wake.

Picha
Mfalme na wafuasi wake wakikimbia

Mfalme na wale waliomfuata walikimbia kutoka kwa Walamani, lakini Walamani waliwashika na kuanza kuwaua. Mfalme aliwaambia wanaume waache famila zao na waendelee kukimbia.

Picha
Walamani wakiwateka watu

Wengi wa wanaume hawakufanya hivyo. Walitekwa na Walamani.

Picha
Wanaume wakimkasirikia Nuhu

Wengi wa wanaume ambao walikimbia pamoja na Mfalme Nuhu walihuzunika. Walitaka kurudi na kuwasaidia wake zao na watoto na watu wao.

Picha
Nuhu pamoja na wanaume wengine

Mfalme Nuhu hakutaka wanaume warudi kwa familia zao. Aliwaamrisha kubaki pamoja naye.

Picha
Wanaume wakimchoma Mfalme Nuhu

Wanaume walimkasirikia Mfalme Nuhu. Walimchoma mpaka kufa, kama Abinadi alivyotoa unabii. Kisha wakarudi kwa familia zao.

Chapisha