Sura ya 54
Ahadi ya Kitabu cha Mormoni
Kabla ya Moroni kuzika bamba zile kwa mara ya mwisho, aliandika ahadi kwa Walamani na kwa mtu yeyote ambaye angesoma kumbukumbu hiyo.
Aliwaambia watu wasome kumbukumbu hiyo, watafakari sana juu yake, na kisha wamuulize Baba wa Mbinguni kama ni ya kweli.
Moroni aliahidi ya kwamba kama watu wangeuliza kwa moyo wa kweli, na imani katika Kristo, Roho Mtakatifu angewasaidia kujua kwamba kumbukumbu hii ni ya kweli.
Moroni aliandika kwamba kama watu watatubu, wamfuate Yesu Kristo, na kumpenda Baba wa Mbinguni, wanaweza kuwa wakamilifu.
Wakati Moroni alipomaliza kuandika kwenye bamba za dhahabu, alizificha ndani a sanduku la mawe katika Mlima Kumora na kulifunika sanduku lile kwa jiwe kubwa. Kazi yake katika maisha ya kufa ilikuwa imekamilika.