Sura ya 40
Samueli Mlamani Anazungumza Kuhusu Yesu Kristo
Walamani walitii amri za Mungu. Walikuwa wenye haki zaidi kuliko Wanefi.
Samueli, nabii wa Kilamani, alikwenda Zarahemla kuhubiri kwa Wanefi waovu. Aliwaambia watubu.
Wanefi walimfukuza Samueli nje ya mji, na akaanza kurudi katika nchi yake.
Lakini Bwana alimwambia Samueli arudi Zarahemla na kuwaambia watu vitu ambavyo Bwana aliviweka katika moyo wake.
Wanefi hawakumruhusu Samueli kurudi kwenye mji, hivyo alipanda juu ya ukuta wa mji na kuhubiri kutokea pale.
Alitoa unabii kwamba Wanefi wangeangamizwa ndani ya miaka 400 isipokuwa watu watubu na kuwa na imani katika Yesu Kristo.
Samweli aliwaambia Wanefi kwamba Yesu Kristo angezaliwa ndani ya miaka mia tano na kwamba angewaokoa wale wote waliomwamini.
Samueli aliwaambia kuhusu ishara ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Nyota mpya ingetokea, na usiku kabla ya Yesu kuzaliwa kusingekuwa na giza.
Kisha Samueli aliwaambia ishara ya kifo cha Yesu. Kungekuwa na siku tatu za giza totoro—jua, mwezi na nyota havingetoa nuru.
Pia kungekuwa na ngurumo na radi na matetemeko ya nchi. Milima ingeanguka, na miji mingi ingeharibiwa.
Baadhi ya Wanefi walimwamini Samueli na wakatubu dhambi zao. Walikwenda kumtafuta Nefi, Mnefi mwenye haki ambaye angewabatiza.
Wanefi waliobaki hawakumwamini Samueli. Walimrushia mawe na mishale. Lakini Bwana alimlinda, na hakuna kati ya jiwe au mshale ulimpiga.
Watu walipoona kwamba hawezi kupigwa, wengi wao walimwamini na wakaenda kwa Nefi kubatizwa.
Nefi pia aliwafundisha watu kuhusu Yesu. Alitaka wao wamwamini Yesu, watubu na kubatizwa.
Wengi wa Wanefi, hata hivyo, hawakumwamini Samueli. Walijaribu kumkamata.
Samueli aliruka chini kutoka ukutani na kukimbia katika nchi yake.
Samueli alinza kuwafundisha Walamani. Hakusikika tena kati ya Wanefi.