Scripture Stories
Sura ya 40: Samueli Mlamani Anazungumza Kuhusu Yesu Kristo


Sura ya 40

Samueli Mlamani Anazungumza Kuhusu Yesu Kristo

Picha
Walamani wakitembea

Walamani walitii amri za Mungu. Walikuwa wenye haki zaidi kuliko Wanefi.

Picha
Samueli akiwahubiria Wanefi

Samueli, nabii wa Kilamani, alikwenda Zarahemla kuhubiri kwa Wanefi waovu. Aliwaambia watubu.

Picha
Samueli akikimbia kutoka kwa walinzi wa Kinefi

Wanefi walimfukuza Samueli nje ya mji, na akaanza kurudi katika nchi yake.

Picha
Samueli akisali

Lakini Bwana alimwambia Samueli arudi Zarahemla na kuwaambia watu vitu ambavyo Bwana aliviweka katika moyo wake.

Picha
Samueli anahubiri akiwa ukutani

Wanefi hawakumruhusu Samueli kurudi kwenye mji, hivyo alipanda juu ya ukuta wa mji na kuhubiri kutokea pale.

Picha
Watu wakimsikiliza Samueli

Alitoa unabii kwamba Wanefi wangeangamizwa ndani ya miaka 400 isipokuwa watu watubu na kuwa na imani katika Yesu Kristo.

Picha
Samueli akizungumza

Samweli aliwaambia Wanefi kwamba Yesu Kristo angezaliwa ndani ya miaka mia tano na kwamba angewaokoa wale wote waliomwamini.

Picha
nyota mjini Bethlehemu

Samueli aliwaambia kuhusu ishara ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Nyota mpya ingetokea, na usiku kabla ya Yesu kuzaliwa kusingekuwa na giza.

Picha
Watu wamekaa katika giza

Kisha Samueli aliwaambia ishara ya kifo cha Yesu. Kungekuwa na siku tatu za giza totoro—jua, mwezi na nyota havingetoa nuru.

Picha
Radi ikipiga majengo

Pia kungekuwa na ngurumo na radi na matetemeko ya nchi. Milima ingeanguka, na miji mingi ingeharibiwa.

Picha
Wanefi wakiongea na Nefi

Baadhi ya Wanefi walimwamini Samueli na wakatubu dhambi zao. Walikwenda kumtafuta Nefi, Mnefi mwenye haki ambaye angewabatiza.

Picha
Watu wakimrushia mishale Samueli

Wanefi waliobaki hawakumwamini Samueli. Walimrushia mawe na mishale. Lakini Bwana alimlinda, na hakuna kati ya jiwe au mshale ulimpiga.

Picha
Wanefi wakirusha mishale

Watu walipoona kwamba hawezi kupigwa, wengi wao walimwamini na wakaenda kwa Nefi kubatizwa.

Picha
Nefi akimbatiza mtu

Nefi pia aliwafundisha watu kuhusu Yesu. Alitaka wao wamwamini Yesu, watubu na kubatizwa.

Picha
Watu wakipanda ngazi

Wengi wa Wanefi, hata hivyo, hawakumwamini Samueli. Walijaribu kumkamata.

Picha
Samueli akiruka kutoka ukutani

Samueli aliruka chini kutoka ukutani na kukimbia katika nchi yake.

Picha
Samueli akiwafundisha Walamani

Samueli alinza kuwafundisha Walamani. Hakusikika tena kati ya Wanefi.

Chapisha