Sura ya 9
Makao mapya katika Nchi ya ahadi
Merikebu iliyowabeba Lehi na familia yake ilivuka bahari na kufika kwenye nchi ya ahadi. Watu wanaweka hema.
Waliandaa udongo na kupanda mbegu walizokuja nazo.
Wakati wakitembea kuzunguka nchi mpya, walikuta wanyama wa aina nyingi. Pia walikuta dhahabu, fedha, na shaba.
Mungu alimwambia Nefi kutengeneza bamba za madini na kuandika juu yake. Nefi aliandika kuhusu familia yake na safari zao. Aliandika maneno ya Mungu.
Lehi alizeeka. Kabla hajafa aliongea na wanawe na kuwambia kuwa watii amri za Mungu. Pia aliwabariki wajukuu zake.
Baada ya Lehi kufariki Lamani na Lemueli walipata hasira juu ya Nefi na wakataka kumuua. Hawakutaka Nefi, kaka yao mdogo, kuwa kiongozi wao.
Bwana alimwambia Nefi kuwaongoza watu walio wema kwenda nyikani. Walisafiri kwa siku nyingi na hatimaye walisimama kwenye nchi walioyoiita Nefi.
Watu waliomfuata Nefi walimtii Mungu. Walifanya kazi kwa bidii na walibarikiwa. Nefi aliwafundisha watu wake kujenga kwa kutumia mbao na chuma. Walijenga hekalu zuri.
Wafuasi wa Lamani na Lamueli waliitwa Walamani.
Walamani hawakumtii Mungu na waliondolewa kutoka kwenye uwepo Wake. Roho wa Bwana asingeweza kuwa pamoja nao mpaka watubu.
Walamani walijawa na fitina na mara kwa mara walipigana na Wanefi.