Scripture Stories
Sura ya 9: Makao mapya katika Nchi ya Ahadi


Sura ya 9

Makao mapya katika Nchi ya ahadi

Picha
Nchi ya ahadi

Merikebu iliyowabeba Lehi na familia yake ilivuka bahari na kufika kwenye nchi ya ahadi. Watu wanaweka hema.

Picha
kupanda mbegu

Waliandaa udongo na kupanda mbegu walizokuja nazo.

Picha
Wanyama wengi

Wakati wakitembea kuzunguka nchi mpya, walikuta wanyama wa aina nyingi. Pia walikuta dhahabu, fedha, na shaba.

Picha
Nefi akiandika

Mungu alimwambia Nefi kutengeneza bamba za madini na kuandika juu yake. Nefi aliandika kuhusu familia yake na safari zao. Aliandika maneno ya Mungu.

Picha
Lehi akiongea na familia yake

Lehi alizeeka. Kabla hajafa aliongea na wanawe na kuwambia kuwa watii amri za Mungu. Pia aliwabariki wajukuu zake.

Picha
Lamani na Lemueli wakimkasirikia Nefi

Baada ya Lehi kufariki Lamani na Lemueli walipata hasira juu ya Nefi na wakataka kumuua. Hawakutaka Nefi, kaka yao mdogo, kuwa kiongozi wao.

Picha
Nefi pamoja na walio wema wanaondoka

Bwana alimwambia Nefi kuwaongoza watu walio wema kwenda nyikani. Walisafiri kwa siku nyingi na hatimaye walisimama kwenye nchi walioyoiita Nefi.

Picha
watu wakiongea

Watu waliomfuata Nefi walimtii Mungu. Walifanya kazi kwa bidii na walibarikiwa. Nefi aliwafundisha watu wake kujenga kwa kutumia mbao na chuma. Walijenga hekalu zuri.

Picha
Walamani

Wafuasi wa Lamani na Lamueli waliitwa Walamani.

Picha
Walamani

Walamani hawakumtii Mungu na waliondolewa kutoka kwenye uwepo Wake. Roho wa Bwana asingeweza kuwa pamoja nao mpaka watubu.

Picha
Walamani wakipigana na Wanefi

Walamani walijawa na fitina na mara kwa mara walipigana na Wanefi.

Chapisha