Sura ya 38
Mauaji ya Mwamuzi Mkuu
Watu waovu walikuwa waamuzi juu ya Wanefi. Waliwaadhibu watu wenye haki lakini si waovu.
Nefi alikuwa na huzuni kuona uovu mwingi miongoni mwa watu.
Siku moja alikuwa akisali katika mnara kwenye bustani yake. Bustani yake ilikuwa pembezoni mwa barabara iliyokuwa ikielekea katika soko la Zarahemla.
Watu waliopita barabarani walimsikia Nefi akisali. Kundi kubwa lilikusanyika, likishangaa kwa nini alikuwa mwenye huzuni.
Wakati Nefi alipoona watu, aliwaambia alikuwa na huzuni kwa sababu ya uovu wao. Aliwaambia watubu.
Aliwaonya kwamba kama hawangetubu, maadui wao wangechukua nyumba zao na miji yao na Bwana hangewasaidia kupigana na adui zao.
Nefi alisema Wanefi walikuwa waovu zaidi kuliko Walamani kwa sababu Wanefi walikuwa wamefundishwa amri lakini walikuwa hawazitii.
Alisema kama Wanefi hawangetubu, wangeharibiwa.
Baadhi ya waamuzi waovu walikuwepo pale. Walitaka watu wamwadhibu Nefi kwa kuongea dhidi yao na sheria yao.
Baadhi ya watu walikubaliana na waamuzi waovu. Wengine walimwamini Nefi; walijua alikuwa nabii na aliongea ukweli.
Nefi aliwaambia watu kwamba walikuwa wameasi dhidi ya Mungu na karibuni wangeadhibiwa kama hawangetubu.
Nefi aliwaambia watu kwenda kwa mwamuzi wao mkuu. Angekuwa amelala chini kwenye damu yake mwenyewe, akiwa ameuwawa na kaka yake aliyetaka nafasi yake.
Wanaume watano kutoka kwenye umati walikimbia kwenda kumuona mwamuzi mkuu. Hawakuamini kwamba Nefi alikuwa ni nabii wa Mungu.
Wakati walipomwona Seezoramu, mwamuzi mkuu, amelala kwenye damu yake, walianguka ardhini kwa woga. Sasa walijua kwamba Nefi alikuwa nabii.
Watumishi wa Seezoramu walikuwa tayari wamemuona Seezoramu na walikimbia kuwaambia watu. Walirudi na kuwakuta wanaume watano wakiwa wameanguka hapo.
Watu walifikiri wale watu watano ndio waliomuua Seezoramu.
Waliwatupa gerezani na kutuma waraka kote kwenye mji kwamba mwamuzi mkuu alikuwa amuwawa na kwamba wauwaji walikuwa gerezani.
Siku iliyofuata watu walikwenda sehemu ambapo mwamuzi mkuu angezikwa. Waamuzi waliokuwa na Nefi bustanini waliulizia wapi walipokuwepo wale wanaume watano.
Waamuzi waliomba kuwaona watuhumiwa wa mauaji.
Watuhumiwa walikuwa ni wale watano ambao walikimbia kutoka bustani ya Nefi kwenda kwa mwamuzi mkuu.
Wale watu watano walisema walimkuta mwamuzi mkuu amelala kwenye damu, kama Nefi alivyosema. Kisha waamuzi walimtuhumu Nefi kwa kumtuma mtu kumuua Seezoramu.
Kwa kujua kwamba Nefi alikuwa nabii, wale watano walibishana na waamuzi, lakini hawakuwasikiliza. Walimfunga Nefi kwa kamba
Waamuzi walimuahidi Nefi fedha na maisha yake kama angesema kwamba alipanga kumuua mwamuzi mkuu.
Nefi aliwaambia waamuzi watubu uovu wao. Kisha aliwaambia waende kwa Seantumu kaka wa Seezoramu.
Nefi aliwaambia wamuulize Seantumu kama yeye na Nefi walipanga kumuua Seezoramu. Nefi alisema Seantumu angejibu “hapana.”
Kisha waamuzi walitakiwa kumuuliza Seantumu kama alimuua kaka yake. Seantumu angesema “hapana, “ lakini waamuzi watakuta damu kwenye kanzu yake.
Nefi alisema Seantumu kisha angetetemeka na kunyauka na hatimaye atakiri kumuua kaka yake.
Waamuzi walikwenda kwenye nyumba ya Seantumu, na kila kitu kilitokea kama Nefi alivyosema kingetokea. Nefi na wale watano waliachiwa huru.
Wakati watu wakiachana na Nefi, baadhi walisema alikuwa ni nabii; na wengine walisema alikuwa ni mungu. Nefi alikwenda nyumbani, akiwa bado na huzuni kuhusu uovu wao.