Scripture Stories
Sura ya 38: Mauaji ya Mwamuzi Mkuu


Sura ya 38

Mauaji ya Mwamuzi Mkuu

Picha
Wanefi waovu wakiongea

Watu waovu walikuwa waamuzi juu ya Wanefi. Waliwaadhibu watu wenye haki lakini si waovu.

Picha
Nefi

Nefi alikuwa na huzuni kuona uovu mwingi miongoni mwa watu.

Picha
barabara kuelekea Zarahemla

Siku moja alikuwa akisali katika mnara kwenye bustani yake. Bustani yake ilikuwa pembezoni mwa barabara iliyokuwa ikielekea katika soko la Zarahemla.

Picha
Nefi akisali

Watu waliopita barabarani walimsikia Nefi akisali. Kundi kubwa lilikusanyika, likishangaa kwa nini alikuwa mwenye huzuni.

Picha
Nefi akizungumza na watu

Wakati Nefi alipoona watu, aliwaambia alikuwa na huzuni kwa sababu ya uovu wao. Aliwaambia watubu.

Picha
Wanefi wakimsikiliza Nefi

Aliwaonya kwamba kama hawangetubu, maadui wao wangechukua nyumba zao na miji yao na Bwana hangewasaidia kupigana na adui zao.

Picha
Nefi akizungumza

Nefi alisema Wanefi walikuwa waovu zaidi kuliko Walamani kwa sababu Wanefi walikuwa wamefundishwa amri lakini walikuwa hawazitii.

Picha
Nefi akizungumza

Alisema kama Wanefi hawangetubu, wangeharibiwa.

Picha
Watu wamekasirika

Baadhi ya waamuzi waovu walikuwepo pale. Walitaka watu wamwadhibu Nefi kwa kuongea dhidi yao na sheria yao.

Picha
Watu wakibishana

Baadhi ya watu walikubaliana na waamuzi waovu. Wengine walimwamini Nefi; walijua alikuwa nabii na aliongea ukweli.

Picha
Nefi akizungumza

Nefi aliwaambia watu kwamba walikuwa wameasi dhidi ya Mungu na karibuni wangeadhibiwa kama hawangetubu.

Picha
Nefi akiashiria

Nefi aliwaambia watu kwenda kwa mwamuzi wao mkuu. Angekuwa amelala chini kwenye damu yake mwenyewe, akiwa ameuwawa na kaka yake aliyetaka nafasi yake.

Picha
Wanaume wakikimbia

Wanaume watano kutoka kwenye umati walikimbia kwenda kumuona mwamuzi mkuu. Hawakuamini kwamba Nefi alikuwa ni nabii wa Mungu.

Picha
Mwamuzi mkuu akiwa amekufa

Wakati walipomwona Seezoramu, mwamuzi mkuu, amelala kwenye damu yake, walianguka ardhini kwa woga. Sasa walijua kwamba Nefi alikuwa nabii.

Picha
Watu wakiashiria

Watumishi wa Seezoramu walikuwa tayari wamemuona Seezoramu na walikimbia kuwaambia watu. Walirudi na kuwakuta wanaume watano wakiwa wameanguka hapo.

Picha
Wanaume wakiwa na hasira

Watu walifikiri wale watu watano ndio waliomuua Seezoramu.

Picha
Wanaume wakiongea

Waliwatupa gerezani na kutuma waraka kote kwenye mji kwamba mwamuzi mkuu alikuwa amuwawa na kwamba wauwaji walikuwa gerezani.

Picha
Wanaume wakiongea

Siku iliyofuata watu walikwenda sehemu ambapo mwamuzi mkuu angezikwa. Waamuzi waliokuwa na Nefi bustanini waliulizia wapi walipokuwepo wale wanaume watano.

Picha
Waamuzi wakiongea

Waamuzi waliomba kuwaona watuhumiwa wa mauaji.

Picha
Wanaume mbele ya waamuzi

Watuhumiwa walikuwa ni wale watano ambao walikimbia kutoka bustani ya Nefi kwenda kwa mwamuzi mkuu.

Picha
Watu mbele ya waamuzi

Wale watu watano walisema walimkuta mwamuzi mkuu amelala kwenye damu, kama Nefi alivyosema. Kisha waamuzi walimtuhumu Nefi kwa kumtuma mtu kumuua Seezoramu.

Picha
Watu watano wakifungwa kamba

Kwa kujua kwamba Nefi alikuwa nabii, wale watano walibishana na waamuzi, lakini hawakuwasikiliza. Walimfunga Nefi kwa kamba

Picha
Mwamuzi akiongea na Nefi

Waamuzi walimuahidi Nefi fedha na maisha yake kama angesema kwamba alipanga kumuua mwamuzi mkuu.

Picha
Nefi akifungwa kamba

Nefi aliwaambia waamuzi watubu uovu wao. Kisha aliwaambia waende kwa Seantumu kaka wa Seezoramu.

Picha
Waamuzi wakiongea na Seantumu

Nefi aliwaambia wamuulize Seantumu kama yeye na Nefi walipanga kumuua Seezoramu. Nefi alisema Seantumu angejibu “hapana.”

Picha
Watu wakivuta joho la Seantumu

Kisha waamuzi walitakiwa kumuuliza Seantumu kama alimuua kaka yake. Seantumu angesema “hapana, “ lakini waamuzi watakuta damu kwenye kanzu yake.

Picha
Seantumu

Nefi alisema Seantumu kisha angetetemeka na kunyauka na hatimaye atakiri kumuua kaka yake.

Picha
Seantumu akichukuliwa

Waamuzi walikwenda kwenye nyumba ya Seantumu, na kila kitu kilitokea kama Nefi alivyosema kingetokea. Nefi na wale watano waliachiwa huru.

Picha
Nefi

Wakati watu wakiachana na Nefi, baadhi walisema alikuwa ni nabii; na wengine walisema alikuwa ni mungu. Nefi alikwenda nyumbani, akiwa bado na huzuni kuhusu uovu wao.

Chapisha