Scripture Stories
Sura ya 25: Haruni Anamfundisha Baba wa Mfalme Lamoni


Sura ya 25

Haruni Anamfundisha Baba wa Mfalme Lamoni

Picha
Haruni na wenzake wakisafiri

Roho aliwaongoza Haruni na wenzake hadi nchi ya Nefi kumfundisha baba wa Lamoni, mfalme wa Walamani wote.

Picha
Haruni anazungumza na mfalme

Haruni alimwambia mfalme kuwa alikuwa kaka yake Amoni. Mfalme alikuwa akifikiria kuhusu ukarimu wa Amoni na kuhusu kile ambacho Amoni alikuwa amemwambia.

Picha
Haruni anazungumza na mfalme

Haruni alimuuliza mfalme kama aliamini katika Mungu. Mfalme alisema hakuwa na uhakika lakini angeamini kama Haruni angesema kuna Mungu. Haruni alimhakikishia mfalme kwamba Mungu yu hai.

Picha
Haruni akimsomea mfalme maandiko

Haruni alimsomea mfalme maandiko. Alimfundisha kuhusu Uumbaji wa dunia, Anguko la Adamu, na misheni ya Yesu Kristo.

Picha
Mfalme akizungumza na Haruni.

Mfalme aliuliza kile ambacho alihitaji kufanya ili apate Roho Mtakatifu na awe tayari kuishi na Mungu. Mfalme alikuwa tayari kufanya chochote, hata kuacha ufalme wake.

Picha
Haruni anazungumza na mfalme

Haruni alimwambia mfalme kwamba alihitaji kutubu dhambi zake kikamilifu. Alihitaji kusali na kuwa na imani kwa Mungu.

Picha
mfalme akisali

Mfalme alisali aweze kujua ikiwa kweli Mungu yupo. Alisema angetubu dhambi zake zote.

Picha
mfalme akiwa sakafuni

Mfalme alianguka sakafuni na akaonekana kama amefariki. Wakati malkia alipomwona, alidhani ya kwamba Haruni na wenzake walikuwa wamemuua.

Picha
malkia akiwashurutisha watumishi

Malkia aliwashurutisha watumishi wake wawaue Haruni na wenzake, lakini watumishi waliogopa. Aliwatuma wakawatafute watu wengine ambao wangefanya hivyo.

Picha
Haruni akimuamuru mfame ainuke

Kabla ya umati mkubwa kukusanyika na kusababisha usumbufu, Haruni aliuchukua mkono wa mfalme na kumuambia asimame. Mfalme alisimama.

Picha
mfalme akimtuliza mkewe

Mfalme alimtuliza mkewe na watumishi waliokuwa wamejawa hofu na kisha akawafundisha injili. Wote waliamini katika Yesu Kristo.

Chapisha