Sura ya 50
Wayaredi Wanaondoka Babeli
Yaredi na kaka yake walikuwa watu wenye haki ambao waliishi katika mji wa Babeli. Waliishi mamia ya miaka kabla ya Wanefi.
Wengi wa watu huko Babeli walikuwa waovu. Walijenga mnara kujaribu kufika mbinguni. Bwana alikasirika na akabadili lugha yao.
Yaredi alimuomba kaka yake kusali na kumuomba Bwana kutobadili lugha ya familia na rafiki zao.
Kaka wa Yaredi alisali, na Bwana akajibu sala yake. Yaredi, kaka yake, na familia na rafiki zao bado wangeweza kuelewana.
Bwana alimwambia kaka wa Yaredi kukusanya familia yake na rafiki zake na kuondoka katika nchi. Walichukua wanyama na kila aina ya mbegu pamoja nao.
Bwana alisema angewaongoza Wayaredi kwenda nchi ya ahadi.
Wayaredi walikamata ndege na samaki kwa ajili ya kwenda nao.
Walichukua makundi ya nyuki wa asali.
Wayaredi walisafiri nyikani. Bwana alizungumza nao kutoka katika wingu na kuwaambia njia ipi ya kupita.
Bwana alisema watu walioishi kwenye nchi ya ahadi lazima wamtumikie Mungu au sivyo wataharibiwa.
Wakati Wayaredi walipofika kwenye ufuko wa bahari, walipiga hema zao. Walikaa kwenye ufuko kwa miaka minne.