Scripture Stories
Mlango wa 5: Safari ya Nyikani.


Sura ya 5

Safari ya Nyikani

Picha
ndugu wakitembea jangwani

Bwana aliwataka wana wa Lehi wawe na wake ambao wangewafundisha watoto wao injili. Alimwamuru Lehi kuwatuma wanawe kurudi Yerusalemu kuileta familia ya Ishmaeli.

Picha
Nefi akizungumza na Ishmaeli

Nefi na kaka zake walirudi Yerusalemu. Walimwambia Ishmaeli kile Bwana alichomtaka afanye. Ishmaeli aliwaamini, na yeye pamoja na familia yake waliondoka pamoja na wana wa Lehi.

Picha
Lamani na Lemueli wakiwa wamemkasirikia Nefi

Wakiwa wanasafiri nyikani, Lamani, Lemueli, na wengine wa familia ya Ishmaeli walikasirika. Walitaka kurudi Yerusalemu.

Picha
Nefi akizungumza na Lamani na Lemueli

Nefi aliwakumbusha Lamani na Lemueli kuhusu yale yote ambayo Bwana alikuwa amewatendea. Aliwaambia wawe na imani kubwa zaidi. Walimkasirikia Nefi lakini hawakurudi Yerusalemu.

Picha
wenza wakioana

Nefi, kaka zake, na Zoramu baadaye waliwaoa mabinti wa Ishmaeli.

Picha
Lehi akiwa ameishikilia Liahona

Bwana alimwambia Lehi aendelee na safari yake. Asubuhi iliyofuata Lehi aligundua mpira wa shaba ulioitwa Liahona nje ya hema lake. Uliashiria wapi pa kuelekea nyikani.

Picha
familia ikisafiri

Familia ya Lehi walikusanya chakula na nafaka na kuyapakia mahema yao. Walisafiri nyikani kwa muda wa siku nyingi, wakifuata maelekezo ya Liahona.

Picha
kuwinda

Nefi na kaka zake walitumia pinde na mishale kuwindia chakula wakiwa safirini.

Picha
upinde uliovunjika

Upinde wa Nefi uliokuwa umetengenezwa kwa chuma ulivunjika, na pinde za kaka zake zilikuwa zimelegea. Kaka zake hawakuweza kuwinda wanyama wowote, kwa hivyo kila mtu alihisi njaa. Lamani na Lemueli walikuwa na hasira.

Picha
Upinde uliotengenezwa kwa mbao

Nefi alitengeneza upinde kutokana na mbao na kumuuliza baba yake mahali ambapo angelikwenda kuwinda. Lehi alipokea maelezo katika Liahona. Nefi alifuata maelezo na akapata wanyama kadhaa.

Picha
Lehi akiwa ameishikilia Liahona

Liahona ilifanya kazi tu wakati familia ya Lehi ilikuwa aminifu, yenye bidii, na tiifu.

Picha
Nefi alirejea na chakula

Nefi alirudi na wale wanyama aliokuwa amepata. Wote walifurahia kupata chakula. Walihuzunika kwamba walikuwa na hasira, na walimshukuru Mungu kwa kuwabariki.

Picha
Mabinti wa Ishmaeli

Safari haikuwa rahisi Mara nyingi familia ya Lehi walikuwa wenye uchovu, wenye njaa, na kiu. Ishameli alifariki na mabinti zake walihuzunika. Walinung’unika dhidi ya Lehi.

Picha
Lamani na Lemueli

Lamani na Lemueli pia walinung’unika. Hawakuamini kwamba Bwana alikuwa amezungumza na Nefi. Walitaka kuwaua Lehi na Nefi ili warudi Yerusalemu.

Picha
Lamani na Lemueli

Sauti ya Bwana iliwazungumzia Lamani na Lemueli. Iliwaambia wasiwakasirikie Lehi na Nefi. Lamani na Lemueli walitubu.

Picha
Familia ya Lehi

Familia ya Lehi iliendelea na safari yao ngumu. Mungu aliwasaidia na kuwaimarisha. Watoto walizaliwa. Lehi na Saria walipata wana wawili zaidi, walioitwa Yakobo na Yusufu.

Picha
familia ikisafiri

Baada ya kusafiri nyikani kwa miaka minane, familia ya Lehi iliwasili katika eneo la pwani. Hapo walipata matunda na asali. Waliliita eneo lile Neema.

Chapisha